Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 64.3
Bible en Swahili de l’est


Punition des méchants

1 Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu; Unilinde uhai wangu na hofu ya adui.
Psaumes 17.8-17.9 Psaumes 141.1 Psaumes 143.1-143.3 Actes 27.24 Psaumes 31.13-31.15
2 Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya, Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;
Jérémie 11.19 Psaumes 56.6 Esaïe 32.2 Psaumes 59.2 Actes 25.3
3 Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,
Psaumes 58.7 Psaumes 57.4 Psaumes 11.2 Proverbes 12.18 Jacques 3.6-3.8
4 Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.
Psaumes 55.19 Psaumes 64.7 Psaumes 59.3-59.4 1 Samuel 19.10 Néhémie 4.11
5 Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona?
Psaumes 10.11 Psaumes 140.5 Esaïe 41.6 Matthieu 23.15 Nombres 22.6
6 Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili; Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao, Na moyo wake, huwa siri kabisa.
Matthieu 26.59 Jérémie 17.9-17.10 Jean 18.29-18.30 1 Samuel 22.9 Psaumes 5.9
7 Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha, Kwa mshale mara watapigwa.
Psaumes 7.12-7.13 Matthieu 24.40 Psaumes 64.4 1 Thessaloniciens 5.2-5.3 Psaumes 73.19
8 Ndivyo watakavyokwazwa, Ulimi wao wenyewe ukishindana nao. Wote wawaonao watatikisa kichwa.
Proverbes 18.7 Proverbes 12.13 Matthieu 21.41 Jérémie 48.27 Psaumes 140.9
9 Na watu wote wataogopa, Wataitangaza kazi ya Mungu, Na kuyafahamu matendo yake.
Jérémie 51.10 Psaumes 40.3 Jérémie 50.28 Psaumes 107.42-107.43 Ezéchiel 14.23
10 Mwenye haki atamfurahia Bwana na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watajisifu.
Psaumes 25.20 Psaumes 112.2 Psaumes 97.11 Psaumes 11.1 Psaumes 32.11-33.1

Cette Bible est dans le domaine public.