Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 5.7
Bible en Swahili de l’est


La justice et la bonté de Dieu

1 Ee Bwana, uyasikilize maneno yangu, Ukuangalie kutafakari kwangu.
Psaumes 54.2 1 Jean 5.14-5.15 Psaumes 55.1-55.2 Psaumes 19.14 Psaumes 64.1
2 Uisikie sauti ya kilio changu, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, Kwa maana Wewe ndiwe nikuombaye.
Psaumes 3.4 Psaumes 65.2 Psaumes 84.3 Psaumes 47.6-47.7 Psaumes 44.4
3 Bwana, asubuhi utaisikia sauti yangu, Asubuhi nitakupangia dua yangu na kutazamia.
Psaumes 88.13 Psaumes 119.147 Psaumes 130.6 Psaumes 55.17 Marc 1.35
4 Maana huwi Mungu apendezwaye na ubaya; Mtu mwovu hatakaa kwako;
Malachie 2.17 Hébreux 12.14 Apocalypse 21.27 Psaumes 101.7 2 Pierre 3.13
5 Wajivunao hawatasimama mbele za macho yako; Unawachukia wote watendao ubatili.
Psaumes 1.5 Psaumes 11.5 Osée 9.15 Lévitique 20.23 Habakuk 1.13
6 Utawaharibu wasemao uongo; Bwana humzira mwuaji na mwenye hila
Psaumes 55.23 Apocalypse 21.8 Apocalypse 22.15 Psaumes 4.2 Esaïe 26.21
7 Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, Nitaingia nyumbani mwako; Na kusujudu kwa kicho, Nikilielekea hekalu lako takatifu.
Psaumes 138.2 Psaumes 132.7 Psaumes 69.13 1 Rois 8.29-8.30 1 Pierre 1.17-1.19
8 Bwana, uniongoze kwa haki yako, Kwa sababu yao wanaoniotea. Uisawazishe njia yako mbele ya uso wangu,
Psaumes 27.11 Psaumes 25.4-25.5 Proverbes 3.5-3.6 Psaumes 143.8-143.10 Psaumes 119.64
9 Maana vinywani mwao hamna uaminifu; Mtima wao ni shimo tupu, koo lao ni kaburi wazi, Ulimi wao hujipendekeza.
Romains 3.13 Psaumes 62.4 Luc 11.44 Michée 6.12 Psaumes 52.2
10 Wewe, Mungu, uwapatilize, Na waanguke kwa mashauri yao. Uwatoe nje kwa ajili ya wingi wa makosa yao, Kwa maana wamekuasi Wewe.
2 Samuel 17.14 2 Samuel 17.23 2 Samuel 15.31 Lamentations 1.5 Psaumes 144.6-144.7
11 Nao wote wanaokukimbilia watafurahi; Watapiga daima kelele za furaha. Kwa kuwa Wewe unawahifadhi, Walipendao jina lako watakufurahia.
Psaumes 2.12 Psaumes 65.13 Juges 5.31 Esaïe 65.13-65.16 Psaumes 69.36-70.4
12 Kwa maana Wewe utambariki mwenye haki; Bwana, utamzungushia radhi kama ngao.
Psaumes 32.10 Psaumes 84.11 Psaumes 29.11 Psaumes 32.7 Psaumes 115.13

Cette Bible est dans le domaine public.