Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 8.6
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 1 de Bildad

1 Ndipo Bildadi huyo Mshuhi akajibu, na kusema,
Job 2.11
2 Wewe utanena maneno haya hata lini? Maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo mkuu hata lini?
Job 6.26 1 Rois 19.11 Job 15.2 Exode 10.7 Exode 10.3
3 Je! Mungu hupotosha hukumu? Au, huyo Mwenyezi hupotosha yaliyo ya haki?
2 Chroniques 19.7 Deutéronome 32.4 Genèse 18.25 Job 34.10-34.12 Romains 3.4-3.6
4 Kwamba watoto wako wamemfanyia dhambi, Naye amewatia mkononi mwa kosa lao;
Job 1.5 Job 1.18-1.19 Genèse 13.13 Job 5.4 Job 18.16-18.19
5 Wewe ukimtafuta Mungu kwa bidii, Na kumsihi huyo Mwenyezi;
Job 11.13 Hébreux 3.7-3.8 Matthieu 7.7-7.8 Jacques 4.7-4.10 Esaïe 55.6-55.7
6 Ukiwa wewe u safi na mwelekevu; Hakika yeye sasa angeamka kwa ajili yako, Na kuyafanya makazi ya haki yako kufanikiwa.
1 Jean 3.19-3.22 Psaumes 7.6 Job 1.8 Proverbes 15.8 Job 22.23-22.30
7 Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, Lakini mwisho wako ungeongezeka sana.
Job 42.12-42.13 Zacharie 4.10 Proverbes 4.18 Matthieu 13.31-13.32 Proverbes 19.20
8 Basi, uwaulize, tafadhali, vizazi vya zamani, Ujitie kuyaangalia yale baba zao waliyoyatafuta;
Job 15.18 Deutéronome 4.32 Deutéronome 32.7 Psaumes 78.3-78.4 Romains 15.4
9 (Kwani sisi tu wa jana tu, wala hatujui neno, Kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli tu;)
1 Chroniques 29.15 Job 14.2 Psaumes 144.4 Psaumes 102.11 Genèse 47.9
10 Je! Hawatakufunza wao, na kukueleza, Na kutamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
Job 12.7-12.8 Hébreux 11.4 Proverbes 18.15 Deutéronome 6.7 Proverbes 16.23
11 Je! Hayo mafunjo yamea pasipo matope Na makangaga kumea pasipo maji?
Esaïe 19.5-19.7 Exode 2.3
12 Yakiwa yakali mabichi bado, wala hayakukatwa, Hunyauka mbele ya majani mengine.
Jérémie 17.6 Jacques 1.10-1.11 Psaumes 129.6-129.7 1 Pierre 1.24 Matthieu 13.20
13 Ndivyo ulivyo mwisho wa hao wamsahauo Mungu; Na matumaini yake huyo mbaya huangamia;
Psaumes 9.17 Job 15.34 Job 13.16 Job 11.20 Proverbes 10.28
14 Uthabiti wake utavunjika, Na matumaini yake huwa ni nyuzi za buibui.
Esaïe 59.5-59.6
15 Ataitegemea nyumba yake, isisimame; Atashikamana nayo, isidumu.
Job 27.18 Matthieu 7.24-7.27 Luc 6.47-6.49 Psaumes 52.5-52.7 Proverbes 10.28
16 Yeye huwa mti mbichi mbele ya jua, Nayo machipukizi yake huenea katika bustani yake.
Psaumes 80.11 Psaumes 37.35-37.36 Job 5.3 Job 21.7-21.15 Psaumes 73.3-73.12
17 Mizizi yake huzonga-zonga chuguu, Huangalia mahali penye mawe.
Job 29.19 Esaïe 40.24 Jérémie 12.1-12.2 Job 18.16 Jude 1.12
18 Lakini, aking’olewa mahali pake, Ndipo patamkana, na kusema, Mimi sikukuona.
Job 7.10 Psaumes 37.36 Job 7.8 Job 20.9 Psaumes 73.18-73.19
19 Tazama, furaha ya njia yake ni hii, Na wengine watachipuka kutoka katika nchi.
Job 20.5 1 Samuel 2.8 Psaumes 113.7 Matthieu 13.20-13.21 Ezéchiel 17.24
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu mkamilifu, Wala hatawathibitisha watendao uovu.
Job 4.7 Job 9.22 Psaumes 94.14 Job 21.30 Psaumes 37.37
21 Bado atakijaza kinywa chako kicheko, Na midomo yako ataijaza shangwe.
Psaumes 126.2 Genèse 21.6 Psaumes 98.4 Luc 6.21 Job 5.22
22 Hao wakuchukiao watavikwa aibu; Nayo hema yake mwovu haitakuwako tena.
Psaumes 35.26 Psaumes 132.18 Psaumes 109.29 Job 18.14 Job 7.21

Cette Bible est dans le domaine public.