Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 3.3
Bible en Swahili de l’est


Dialogue entre Job et ses amis

Intervention n° 1 de Job

1 Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.
Jérémie 20.14-20.15 Psaumes 106.33 Psaumes 39.2-39.3 Job 1.22 Job 35.16
2 Ayubu akajibu, na kusema;
Juges 18.14
3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.
Jérémie 20.14-20.18 Job 10.18-10.19 Jérémie 15.10
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.
Joël 2.2 Deutéronome 11.12 Apocalypse 16.10 Actes 27.20 Exode 10.22-10.23
5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.
Job 10.21-10.22 Psaumes 23.4 Job 28.3 Esaïe 9.2 Jérémie 13.16
6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe.
Esaïe 13.20-13.22 Apocalypse 18.22-18.23 Jérémie 7.34 Esaïe 24.8
8 Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani.
Job 41.1 Job 41.10 Amos 5.16 Job 41.25 2 Chroniques 35.25
9 Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza; Na utafute mwanga lakini usiupate; Wala usiyaone makope ya asubuhi;
Job 41.18 Job 30.26 Jérémie 13.16 Jérémie 8.15
10 Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu. Wala kunifichia taabu machoni.
1 Samuel 1.5 Job 6.2-6.3 Genèse 29.31 Job 23.2 Genèse 20.18
11 Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni?
Job 10.18-10.19 Osée 9.14 Psaumes 71.6 Psaumes 139.13-139.16 Jérémie 15.10
12 Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya?
Genèse 30.3 Esaïe 66.12 Genèse 50.23 Ezéchiel 16.4-16.5
13 Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;
Job 21.13 Job 10.22 Job 7.8-7.10 Job 19.27 Job 14.10-14.12
14 Pamoja na wafalme na washauri wa dunia, Hao waliojijengea maganjoni;
Job 15.28 Esaïe 14.10-14.16 Psaumes 49.6-49.10 Job 30.23 Ezéchiel 27.18-27.32
15 Au pamoja na wakuu wenye dhahabu, Waliozijaza fedha nyumba zao;
Nombres 22.18 1 Rois 10.27 Job 27.16-27.17 Zacharie 9.3 Sophonie 1.18
16 Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako; Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa.
Psaumes 58.8 1 Corinthiens 15.8 Ecclésiaste 6.3
17 Huko waovu huacha kusumbua; Huko nako hao waliochoka wapumzika
Job 17.16 Apocalypse 14.13 Hébreux 4.9 Job 14.13 2 Thessaloniciens 1.6-1.7
18 Huko wafungwa waona raha pamoja; Hawaisikii sauti yake msimamizi.
Job 39.7 Exode 5.6-5.8 Esaïe 14.3-14.4 Juges 4.3 Exode 5.15-5.19
19 Wakuu na wadogo wako huko; Mtumishi yu huru kwa bwana wake.
Ecclésiaste 12.7 Job 30.23 Psaumes 49.6-49.10 Psaumes 49.14-49.20 Ecclésiaste 12.5
20 Mbona yeye aliye mashakani kupewa mwanga, Na hao wenye uchungu rohoni kupewa uhai;
Jérémie 20.18 Job 7.15-7.16 Proverbes 31.6 1 Samuel 1.10 Job 6.9
21 Ambao wangojea mauti, lakini hawayapati; Na kuyachimbulia zaidi ya kutafuta hazina iliyostirika;
Apocalypse 9.6 Proverbes 2.4 1 Rois 19.4 Jonas 4.8 Jonas 4.3
22 Ambao wafurahi mno, Na kushangilia watakapoliona kaburi?
23 Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukingo?
Job 19.8 Lamentations 3.7 Esaïe 40.27 Job 19.6 Job 12.14
24 Kwani kuugua kwangu kwaja kana kwamba ni chakula, Na kunguruma kwangu kumemiminika kama maji.
Psaumes 102.9 Psaumes 42.3-42.4 Psaumes 80.5 Psaumes 38.8 Psaumes 22.1-22.2
25 Maana jambo hilo nichalo hunipata, Nalo linitialo hofu hunijilia.
Job 1.5 Job 30.15 Job 31.23
26 Mimi sioni raha, wala situlii, wala kupumzika; Lakini huja taabu.
Job 7.14 Psaumes 143.11 Job 27.9

Cette Bible est dans le domaine public.