Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 20.29
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 2 de Tsophar

1 Ndipo Sofari, Mnaamathi, akajibu, na kusema,
Job 2.11 Job 11.1 Job 42.9
2 Kwa hiyo mawazo yangu hunipa jawabu, Kwa ajili ya haraka niliyo nayo ndani yangu.
Jérémie 20.9 Job 32.13-32.20 Psaumes 31.22 Ecclésiaste 7.9 Proverbes 29.20
3 Nimesikia maonyo yanayonitahayarisha, Nayo roho ya ufahamu wangu hunijibu.
Job 19.3 Job 19.29 Psaumes 49.3 Job 33.3 Job 27.11
4 Je! Hujui neno hili tangu zamani za kale, Tangu wanadamu kuwekwa juu ya nchi,
Genèse 1.28 Genèse 9.1-9.3 Job 32.7 Psaumes 115.16 Job 15.10
5 Ya kuwa shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo, Na furaha ya wapotovu ni ya dakika moja tu?
Psaumes 37.35-37.36 Esther 5.11-5.12 Matthieu 7.21 Job 8.12-8.13 Jacques 4.16
6 Ujapopanda ukuu wake mpaka mbinguni, Na kichwa chake kufikilia mawinguni;
Esaïe 14.13-14.14 Abdias 1.3-1.4 Genèse 11.4 Matthieu 11.23 Daniel 4.11
7 Hata hivyo ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe; Hao waliomwona watasema, Yuko wapi?
1 Rois 14.10 Psaumes 83.10 2 Rois 9.37 Job 14.10 Jérémie 8.2
8 Ataruka mfano wa ndoto, asionekane; Naam, atafukuzwa kama maono ya usiku,
Psaumes 90.5 Psaumes 73.20 Esaïe 29.7-29.8 Psaumes 18.10 Job 18.18
9 Jicho lililomwona halitamwona tena; Wala mahali pake hapatamtazama tena.
Job 7.8 Job 7.10 Psaumes 37.36 Psaumes 37.10 Job 8.18
10 Watoto wake watataka fadhili kwa maskini, Na mikono yake itarudisha mali yake.
Job 20.18 Job 27.16-27.17 Luc 19.8 Exode 22.3 Exode 9.2
11 Mifupa yake imejaa ujana wake, Lakini utalala nchi naye mavumbini.
Job 21.26 Job 13.26 Psaumes 25.7 Jean 8.21 Jean 8.24
12 Ingawa uovu una tamu kinywani mwake, Ingawa auficha chini ya ulimi wake;
Psaumes 10.7 Job 15.16 Ecclésiaste 11.9 Proverbes 9.17-9.18 Proverbes 20.17
13 Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake. Lakini akaushika vivyo kinywani mwake;
Romains 8.13 Marc 9.43-9.49 Matthieu 5.29-5.30 Nombres 11.18-11.20
14 Hata hivyo chakula chake matumboni mwake kinabadilika, Kimekuwa ni nyongo za majoka ndani yake.
2 Samuel 12.10-12.11 Jérémie 2.19 Psaumes 51.8-51.9 Malachie 2.2 Job 20.16
15 Amemeza mali, naye atayatapika tena; Mungu atayatoa tumboni mwake.
Proverbes 23.8 Matthieu 27.3-27.4
16 Ataamwa sumu ya majoka; Na ulimi wa fira utamwua.
Deutéronome 32.24 Esaïe 30.6 Romains 3.13 Actes 28.3-28.6 Matthieu 3.7
17 Hataiangalia hiyo mito ya maji, Vile vijito vilivyojaa asali na siagi.
Deutéronome 32.13-32.14 Job 29.6 Apocalypse 22.1 Jérémie 17.6-17.8 2 Rois 7.2
18 Aliyoyataabikia kazi atayarudisha, asiyameze; Kwa mali aliyoyapata, hatafurahi.
Job 20.15 Job 20.10 Jérémie 22.13 Jacques 4.8-4.9 Amos 8.4
19 Kwa maana amewaonea na kuwaacha maskini; Amenyang’anya nyumba kwa jeuri, wala hataijenga.
Job 35.9 Proverbes 14.31 Job 24.2-24.12 Job 21.27-21.28 Job 22.6
20 Kwa sababu hakujua utulivu ndani yake, Hataponya cho chote katika hicho alichokifurahia.
Ecclésiaste 5.13-5.14 Esaïe 57.20-57.21
21 Hakikusalia kitu asichokula; Kwa hiyo kufanikiwa kwake hakutadumu.
Jérémie 17.11 Job 18.19 Luc 16.24-16.25 Job 15.29
22 Katika kujaa kwa wingi wake atakuwa katika dhiki; Mkono wa kila anayesumbuliwa utamjia.
Psaumes 39.5 Job 1.15 Job 3.17 Ecclésiaste 2.18-2.20 Esaïe 10.6
23 Hapo atakapo kulijaza tumbo lake, Mungu atamtupia ukali wa ghadhabu zake, Na kuunyesha juu yake akiwa anakula.
Psaumes 78.30-78.31 Nombres 11.33 Luc 12.17-12.20 Esaïe 21.4 Exode 9.23
24 Ataikimbia silaha ya chuma, Na uta wa shaba utamchoma kwa pili.
Amos 5.19 Esaïe 24.18 2 Samuel 22.35 Amos 9.1-9.3 Proverbes 7.23
25 Yeye autoa, nao watoka mwilini mwake; Naam, ncha ing’aayo yatoka katika nyongo yake; Vitisho viko juu yake.
Job 16.13 Job 18.11 Deutéronome 32.41 Job 27.20 Job 15.21
26 Giza lote linawekwa kwa ajili ya hazina zake; Moto ambao haukuvuviwa na mtu utamla; Utayateketeza yaliyosalia hemani mwake.
Psaumes 21.9 Esaïe 30.33 Job 18.18-18.19 Matthieu 8.12 Esaïe 8.22
27 Mbingu zitafunua wazi uovu wake, Nayo nchi itainuka kinyume chake.
Esaïe 26.21 Job 16.18 Luc 12.2-12.3 Job 18.18 1 Corinthiens 4.5
28 Maongeo ya nyumba yake yataondoka, Yatamwagika mbali katika siku ya ghadhabu zake.
2 Rois 20.17 Job 20.10 Deutéronome 28.31 Jacques 5.1-5.3 Job 20.18-20.22
29 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu itokayo kwa Mungu, Na urithi aliowekewa na Mungu.
Job 27.13 Job 31.2-31.3 Job 18.21 Matthieu 24.51 Psaumes 11.5-11.6

Cette Bible est dans le domaine public.