Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ruth 1.10
Bible en Swahili de l’est


Attachement de Ruth pour Naomi

1 Ikawa zamani za Waamuzi walipoamua, kulikuwa na njaa katika nchi. Akaondoka mtu mmoja wa Bethlehemu ya Yuda, akaenda kukaa katika nchi ya Moabu, yeye na mkewe na wanawe wawili.
Genèse 12.10 Genèse 26.1 Psaumes 105.16 Juges 17.8 Ezéchiel 14.13
2 Na jina la mtu huyo aliitwa Elimeleki, na jina la mkewe Naomi, na majina ya wanawe wawili Maloni na Kilioni, Waefrathi wa Bethlehemu ya Yuda. Wakafika nchi ya Moabu, wakakaa huko.
Genèse 35.19 Michée 5.2 1 Samuel 17.21 1 Samuel 1.1
3 Akafa Elimeleki, mumewe Naomi; na yule mwanamke akasalia na wanawe wawili.
Hébreux 12.10-12.11 Hébreux 12.6 2 Rois 4.1 Psaumes 34.19
4 Nao wakaoa wake katika wanawake wa Moabu; na jina la mmoja aliitwa Orpa, na jina la wa pili Ruthuu. Wakakaa huko yapata miaka kumi.
Matthieu 1.5 Deutéronome 23.3 1 Rois 11.1-11.2 Deutéronome 7.3
5 Wakafa na Maloni na Kilioni wote wawili; na huyo mwanamke akawa amefiwa na wanawe wawili, na mumewe pia.
Luc 7.12 Psaumes 89.30-89.32 Matthieu 22.25-22.27 Jérémie 2.19 Deutéronome 32.39
6 Ndipo alipoondoka, yeye na wakweze, ili kurudi kutoka nchi ya Moabu; maana huko katika nchi ya Moabu amesikia ya kwamba Bwana amewajilia watu wake na kuwapa chakula.
Psaumes 132.15 Exode 4.31 Matthieu 6.11 Exode 3.16 Luc 1.68
7 Basi akatoka pale alipokuwapo, na wakweze wawili pamoja naye; wakashika njia ili kurudi mpaka nchi ya Yuda.
2 Rois 8.3 Exode 18.27 Ruth 1.14 Ruth 1.10
8 Kisha Naomi akawaambia wakweze wawili, Nendeni sasa mkarejee kila mmoja nyumbani kwa mamaye; Bwana na awatendee mema ninyi, kama ninyi mlivyowatendea mema hao waliofariki na mimi pia.
Ruth 2.20 Ruth 1.5 Ephésiens 5.22 Philippiens 4.18-4.19 Josué 24.15-24.28
9 Bwana na awajalie kuona raha kila mmoja nyumbani kwa mumewe. Kisha akawabusu; nao wakapaza sauti zao wakalia.
Ruth 3.1 Genèse 27.27 Genèse 29.11 Genèse 45.15 Actes 20.37
10 Wakamwambia, La, sivyo; lakini tutarudi pamoja nawe kwa watu wako.
Psaumes 119.63 Psaumes 16.3 Zacharie 8.23
11 Naye Naomi akasema, Enyi wanangu, mrejee; kwani kufuatana na mimi? Je! Mimi ninao watoto wa kiume tena tumboni mwangu, hata wawe waume zenu?
Deutéronome 25.5 Genèse 38.11
12 Enyi wanangu, mrejee; nendeni zenu; kwa kuwa mimi ni mzee, siwezi kupata mume tena. Kama ningesema, Natumaini; kama ningepata mume hata usiku huu, na kuzaa watoto wa kiume;
Genèse 17.17 1 Timothée 5.9
13 je! Mngesubiri hata watakapokuwa watu wazima? Mngejizuia msiwe na waume? La, sivyo, wanangu; maana ni vigumu kwangu kuliko kwenu, kwa sababu mkono wa Bwana umetoka juu yangu.
Job 19.21 Psaumes 32.4 Juges 2.15 Psaumes 38.2 Psaumes 39.9-39.10
14 Nao wakapaza sauti zao, wakalia tena, na Orpa akambusu mkwewe, lakini Ruthuu akaambatana naye.
Proverbes 18.24 Proverbes 17.17 2 Timothée 4.10 Matthieu 10.37 Genèse 31.55
15 Naye akasema, Tazama, shemeji yako amerejea kwa watu wake, na kwa mungu wake; basi urejee wewe umfuate shemeji yako.
Juges 11.24 Josué 24.15 2 Rois 2.2 2 Samuel 15.19-15.20 Sophonie 1.6
16 Naye Ruthuu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu;
Ruth 2.11-2.12 Esaïe 14.1 2 Corinthiens 6.16-6.18 Jean 13.37 1 Thessaloniciens 1.9
17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe nami.
1 Samuel 3.17 1 Samuel 25.22 2 Samuel 19.13 2 Rois 6.31 1 Rois 2.23
18 Basi alipomwona kuwa amekaza nia yake kufuatana naye, aliacha kusema naye.
Actes 21.14 Ephésiens 6.10 Actes 2.42
19 Hivyo hao wakaendelea wote wawili hata walipofika Bethlehemu. Na ikawa walipofika Bethlehemu, mji wote ulitaharuki kwa habari zao. Nao wanawake wakasema, Je! Huyu ni Naomi?
Matthieu 21.10 Esaïe 23.7 Lamentations 2.15
20 Akawaambia, Msiniite Naomi niiteni Mara,kwa sababu Mwenyezi Mungu amenitenda mambo machungu sana.
Job 6.4 Lamentations 3.1-3.20 Exode 6.3 Psaumes 73.14 Genèse 17.1
21 Mimi nalitoka hali nimejaa, naye Bwana amenirudisha sina kitu, kwani kuniita Naomi, ikiwa Bwana ameshuhudia juu yangu, na Mwenyezi Mungu amenitesa?
Job 1.21 1 Samuel 2.7-2.8 Job 13.26 Job 10.17 Malachie 3.5
22 Basi Naomi akarudi; pamoja na Ruthuu Mmoabi, mkwewe; ambao walirudi kutoka nchi ya Moabu; nao wakafika Bethlehemu mwanzo wa mavuno ya shayiri.
Ruth 2.23 2 Samuel 21.9 Exode 9.31-9.32

Cette Bible est dans le domaine public.