Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

3 Jean 1.9
Bible en Swahili de l’est


Salutation et louange

1 Mzee, kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli.
1 Jean 3.18 1 Corinthiens 1.14 Romains 16.23 Actes 20.4 2 Jean 1.1-1.13
2 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.
2 Pierre 1.3-1.9 Jacques 5.12 2 Pierre 3.18 Psaumes 20.1-20.5 Colossiens 1.4-1.6
3 Maana nalifurahi mno walipokuja ndugu na kuishuhudia kweli yako, kama uendavyo katika kweli.
2 Jean 1.4 Ephésiens 1.15-1.16 2 Jean 1.2 Romains 1.8-1.9 1 Thessaloniciens 3.6-3.9
4 Sina furaha iliyo kuu kuliko hii, kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli.
Galates 4.19 Philémon 1.10 2 Rois 20.3 1 Rois 3.6 2 Timothée 1.2
5 Mpenzi, kazi ile ni ya uaminifu uwatendeayo hao ndugu na hao wageni nao,
2 Corinthiens 4.1-4.3 Luc 12.42 1 Pierre 4.10-4.11 Luc 16.10-16.12 Galates 6.10
6 waliokushuhudia upendo wako mbele ya kanisa; utafanya vizuri ukiwasafirisha kama ipasavyo kwa Mungu.
1 Thessaloniciens 2.12 Actes 15.3 Tite 3.13 Colossiens 1.10 Actes 15.29
7 Kwa maana, kwa ajili ya Jina hilo, walitoka, wasipokee kitu kwa Mataifa.
2 Corinthiens 12.13 2 Corinthiens 4.5 1 Corinthiens 9.18 Actes 8.4 Apocalypse 2.3
8 Basi imetupasa sisi kuwakaribisha watu kama hao, ili tuwe watenda kazi pamoja na kweli.
Colossiens 4.11 1 Corinthiens 3.5-3.9 1 Thessaloniciens 3.2 2 Corinthiens 6.1 Matthieu 10.14

Diotrèphe et Démétrius

9 Naliliandikia kanisa neno, lakini Diotrefe, apendaye kuwa wa kwanza kati yao, hatukubali.
Matthieu 20.20-20.28 Luc 22.24-22.27 Tite 1.7-1.16 Matthieu 23.4-23.8 Marc 9.34
10 Kwa hiyo, nikija, nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na hayo, ila yeye mwenyewe hawakaribishi hao ndugu, na wale watakao kuwakaribisha, huwazuia, na kuwatoa katika kanisa.
3 Jean 1.5 2 Corinthiens 13.2 Esaïe 66.5 Luc 6.22 Jean 9.34-9.35
11 Mpenzi, usiuige ubaya, bali uige wema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu, bali yeye atendaye mabaya hakumwona Mungu.
Esaïe 1.16-1.17 Psaumes 37.27 1 Jean 2.29 2 Timothée 3.10 1 Pierre 3.13
12 Demetrio ameshuhudiwa na watu wote, tena na ile kweli yenyewe. Nasi pia twashuhudia, nawe wajua ya kwamba ushuhuda wetu ni kweli.
1 Timothée 3.7 Jean 21.24 Jean 19.35 Actes 10.22 1 Thessaloniciens 4.12
13 Nalikuwa na mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa wino na kalamu.
2 Jean 1.12
14 Lakini nataraji kukuona karibu, nasi tutasema uso kwa uso. [15] Amani kwako. Rafiki zetu wakusalimu. Wasalimu hao rafiki zetu, kila mtu kwa jina lake.
Romains 16.1-16.16 Genèse 43.23 1 Pierre 5.14 Galates 5.16 Ephésiens 6.23

Cette Bible est dans le domaine public.