Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Jean 1.2
Bible en Swahili de l’est


Salutation et louange

1 Mzee, kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuao ile kweli;
Jean 8.32 1 Pierre 1.22-1.23 2 Jean 1.5 1 Timothée 2.4 1 Jean 3.18
2 kwa ajili ya hiyo kweli ikaayo ndani yetu, nayo itakuwa pamoja nasi hata milele.
1 Jean 1.8 Colossiens 3.16 1 Pierre 1.23-1.25 2 Timothée 1.5 2 Corinthiens 4.5
3 Neema, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.
Romains 1.7 1 Timothée 1.2 1 Jean 2.23-2.24 Zacharie 8.19 2 Timothée 1.13
4 Nalifurahi mno kwa kuwa nimewaona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile tulivyopokea amri kwa Baba.
3 Jean 1.3-1.4 Ephésiens 5.8 Galates 2.14 1 Jean 2.6 Philippiens 4.10

Appel à un amour doublé de vigilance

5 Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.
1 Jean 3.11 Jean 15.12 Jean 13.34-13.35 Galates 5.22 1 Pierre 1.22-1.23
6 Na huu ndio upendo: tuenende kwa kuzifuata amri zake. Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende katika hiyo.
1 Jean 5.3 1 Jean 2.24 Jean 15.10 1 Jean 2.5 Jean 14.15
7 Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea duniani, wasiokiri ya kuwa Yesu Kristo yuaja katika mwili. Huyo ndiye yule mdanganyifu na mpinga Kristo.
1 Jean 2.26 1 Jean 4.1-4.3 1 Jean 2.18-2.22 2 Pierre 2.1-2.3 Apocalypse 12.9
8 Jiangalieni nafsi zenu msiyapoteze mliyoyatenda, bali mpokee thawabu timilifu.
Apocalypse 3.11 Hébreux 10.35 1 Corinthiens 3.8 Galates 3.4 Marc 13.9
9 Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia.
1 Jean 2.22-2.24 Jean 15.6 Jean 7.16-7.17 1 Jean 1.3 Hébreux 6.1
10 Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.
Tite 3.10 Galates 1.8-1.9 2 Timothée 3.5-3.6 2 Thessaloniciens 3.6 Romains 16.17-16.18
11 Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.
1 Timothée 5.22 Ephésiens 5.11 Apocalypse 18.4 Psaumes 50.18
12 Kwa kuwa ninayo mambo mengi, sitaki kuyaandika kwa karatasi na wino; lakini nataraji kuja kwenu, na kusema nanyi uso kwa uso, ili furaha yetu iwe imetimizwa.
Jean 16.24 Jean 15.11 1 Jean 1.4 3 Jean 1.13-1.14 Jean 17.13
13 Watoto wa ndugu yako aliye mteule, wakusalimu.
1 Pierre 5.13 2 Jean 1.1-1.13

Cette Bible est dans le domaine public.