Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 12.14
Bible en Swahili de l’est


Liste des rois vaincus

1 Basi hawa ndio wafalme wa nchi, ambao wana wa Israeli waliwapiga na kuimiliki nchi yao ng’ambo ya pili ya Yordani, upande wa maawio ya jua, kutoka bonde la Amoni mpaka mlima wa Hermoni, na nchi yote ya Araba upande wa mashariki;
Deutéronome 3.8-3.9 Nombres 21.13 Nombres 21.24 Deutéronome 4.48 Josué 11.17
2 Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekaa huko Heshboni, naye ndiye aliyetawala toka Aroeri, ulioko kando ya bonde la Arnoni, na toka huo mji ulio katikati ya bonde, na nusu ya Gileadi, hata kuufikilia mto wa Yaboki, mpaka wa hao wana wa Amoni;
Genèse 32.22 Néhémie 9.22 Juges 11.13 Juges 11.22 Deutéronome 2.24-2.37
3 na nchi ya Araba mpaka bahari ya Kinerethi, kuelekea mashariki, tena mpaka bahari ya Ataba, mpaka Bahari ya Chumvi, kwendea mashariki, njia ya kwendea Beth-yeshimothi; tena upande wa kusini, chini ya matelemko ya Pisga;
Deutéronome 3.17 Josué 13.20 Josué 11.2 Deutéronome 4.49 Genèse 19.25
4 tena mpaka wa Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa wa hayo mabaki ya hao Warefai, aliyekaa Ashtarothi na Edrei,
Deutéronome 1.4 Deutéronome 3.10-3.11 Josué 13.12 Nombres 21.33-21.35 Deutéronome 3.1-3.7
5 naye alitawala katika mlima wa Hermoni, na katika Saleka, na katika Bashani yote, hata mpaka wa Wageshuri, na Wamaaka, na nusu ya Gileadi, mpaka wa huyo Sihoni mfalme wa Heshboni.
Deutéronome 3.14 Josué 13.11 1 Samuel 27.8 Deutéronome 3.8-3.10 Deutéronome 4.47-4.48
6 Musa mtumishi wa Bwana na wana wa Israeli wakawapiga; naye Musa mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, na Wagadi, na nusu ya kabila ya Manase iwe urithi wao.
Nombres 32.33 Nombres 21.24-21.35 Josué 13.8-13.32 Deutéronome 3.11-3.17 Luc 22.29-22.42
7 Hawa ni wafalme wa hiyo nchi ambao Yoshua na wana wa Israeli waliwapiga ng’ambo ya pili ya Yordani upande wa magharibi, kutoka Baal-gadi katika bonde la Lebanoni mpaka kilima cha Halaki, kilichoelekea Seiri; Yoshua naye akawapa kabila za Israeli iwe milki yao sawasawa na magawanyo yao;
Josué 11.17 Josué 11.23-12.1 Genèse 36.20 Genèse 36.30 Josué 3.17
8 katika nchi ya vilima, na katika Shefela, na katika nchi ya Araba, na katika matelemko, na katika bara, na katika Negebu; nchi ya Mhiti, na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi;
Josué 11.16 Josué 10.40 Josué 9.1 Exode 23.23 Deutéronome 9.1
9 mfalme wa Yeriko, mmoja; mfalme wa Ai, ulio karibu na Betheli, mmoja;
Josué 8.17 Josué 8.29-8.35 Josué 8.1 Josué 6.2-6.21
10 mfalme wa Yerusalemu, mmoja; mfalme wa Hebroni, mmoja;
Josué 10.23 Josué 10.3 Josué 10.36-10.37
11 mfalme wa Yarmuthi, mmoja; na mfalme wa Lakishi, mmoja;
Josué 10.3-10.23 Josué 10.31-10.32
12 mfalme wa Egloni, mmoja; na mfalme wa Gezeri, mmoja;
Josué 10.33 Josué 15.39 Josué 10.3 Josué 10.23
13 mfalme wa Debiri, mmoja; na mfalme wa Gederi, mmoja;
Josué 10.38 Josué 10.3 Josué 15.36
14 mfalme wa Horma, mmoja; na mfalme wa Aradi, mmoja;
Nombres 21.1 Nombres 14.45 Nombres 21.3
15 mfalme wa Libna, mmoja; na mfalme wa Adulamu, mmoja;
Josué 10.29-10.30 1 Samuel 22.1
16 mfalme wa Makeda, mmoja; na mfalme wa Betheli, mmoja;
Josué 10.28 Josué 8.17 Juges 1.22 Genèse 28.19 Genèse 12.8
17 mfalme wa Tapua, mmoja; na mfalme wa Heferi, mmoja;
1 Rois 4.10 Josué 19.13 Josué 15.34
18 mfalme wa Afeka, mmoja; na mfalme wa Lasharoni, mmoja;
Esaïe 33.9 Josué 13.4 1 Samuel 4.1 Josué 19.30
19 mfalme wa Madoni, mmoja; na mfalme wa Hazori, mmoja;
Josué 11.1 Juges 4.2 Josué 11.10-11.11
20 mfalme wa Shimron-meroni, mmoja; na mfalme wa Akshafu, mmoja;
Josué 11.1 Josué 19.25 Josué 19.15
21 mfalme wa Taanaki, mmoja; na mfalme wa Megido, mmoja;
Josué 17.11 2 Rois 23.29-23.30 Juges 5.19 1 Rois 4.12
22 na mfalme wa Kedeshi, mmoja; mfalme wa Yokneamu wa Karmeli, mmoja;
Josué 19.37 Josué 21.32 Josué 15.55 Josué 15.23 Esaïe 35.2
23 mfalme wa Dori katika kilima cha Dori, mmoja; na mfalme wa makabila katika Gilgali, mmoja;
Josué 11.2 Genèse 14.1-14.2 Esaïe 9.1 Josué 4.19 Josué 17.11
24 na mfalme wa Tirsa, mmoja; wafalme hao wote walikuwa ni thelathini na mmoja.
Deutéronome 7.24 2 Rois 15.14 1 Rois 16.23

Cette Bible est dans le domaine public.