Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Thessaloniciens 1.2
Bible en Swahili de l’est


Salutation et louange

1 Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba yetu, na Bwana Yesu Kristo.
2 Corinthiens 1.19 Actes 16.1 1 Thessaloniciens 1.1-1.10
2 Neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba, na kwa Bwana Yesu Kristo.
Romains 1.7 1 Corinthiens 1.8 1 Corinthiens 1.3
3 Ndugu, imetupasa kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, kama ilivyo wajibu, kwa kuwa imani yenu inazidi sana, na upendo wa kila mtu kwenu kwa mwenzake umekuwa mwingi.
2 Thessaloniciens 2.13 1 Thessaloniciens 4.1 1 Pierre 1.22 Romains 1.8 2 Pierre 1.5-1.10
4 Hata na sisi wenyewe twaona fahari juu yenu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya saburi yenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na dhiki mnazostahimili.
1 Thessaloniciens 2.14 1 Thessaloniciens 2.19 2 Corinthiens 7.14 1 Thessaloniciens 1.3 1 Corinthiens 7.17
5 Ndiyo ishara hasa ya hukumu iliyo haki ya Mungu, ili mhesabiwe kuwa mwastahili kuuingia ufalme wa Mungu, ambao kwa ajili yake mnateswa.
Philippiens 1.28 Luc 20.35 Apocalypse 19.2 Actes 14.22 2 Thessaloniciens 1.11
6 Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi;
Apocalypse 6.10 Deutéronome 32.41-32.43 Apocalypse 16.5-16.6 Apocalypse 15.4 Psaumes 74.22-74.23
7 na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake
Apocalypse 14.13 Apocalypse 22.16 Jude 1.14-1.15 Apocalypse 22.9 Ephésiens 1.2
8 katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu;
Galates 4.8 Hébreux 10.27 Apocalypse 20.14-20.15 1 Pierre 4.17 2 Pierre 3.10-3.12
9 watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake;
Matthieu 25.41 2 Thessaloniciens 2.8 Philippiens 3.19 Esaïe 2.21 Apocalypse 21.8
10 yeye atakapokuja ili kutukuzwa katika watakatifu wake, na kustaajabiwa katika wote waliosadiki katika siku ile, (kwa sababu ushuhuda wetu ulisadikiwa kwenu).
Jean 17.10 Esaïe 49.3 Psaumes 89.7 1 Corinthiens 1.6 1 Corinthiens 3.13
11 Kwa hiyo twawaombea ninyi sikuzote, ili Mungu wetu awahesabu kuwa mmekustahili kuitwa kwenu, akatimiza kila haja ya wema na kila kazi ya imani kwa nguvu;
2 Thessaloniciens 1.5 1 Thessaloniciens 1.3 1 Thessaloniciens 2.12-2.13 Colossiens 1.9-1.13 Philippiens 2.13
12 jina la Bwana wetu Yesu litukuzwe ndani yenu, nanyi ndani yake, kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
2 Thessaloniciens 1.10 Jean 17.10 1 Corinthiens 1.4 2 Corinthiens 8.9 Colossiens 2.9-2.10

Cette Bible est dans le domaine public.