Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Thessaloniciens 1.9
Bible en Swahili de l’est


Salutation et louange

1 Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba, na katika Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani.
Romains 1.7 2 Thessaloniciens 1.1 2 Corinthiens 1.19 Actes 18.5 1 Pierre 5.12
2 Twamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu nyote, tukiwataja katika maombi yetu.
Romains 1.8-1.9 Ephésiens 1.15-1.16 Colossiens 1.3 1 Corinthiens 1.4 Philémon 1.4
3 Wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya upendo, na saburi yenu ya tumaini lililo katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele za Mungu Baba yetu.
1 Corinthiens 13.13 2 Thessaloniciens 1.11 Apocalypse 2.19 Galates 5.6 Romains 8.24-8.25
4 Kwa maana, ndugu mnaopendwa na Mungu, twajua uteule wenu;
2 Thessaloniciens 2.13 2 Pierre 1.10 Tite 3.4-3.5 1 Thessaloniciens 1.3 Ephésiens 2.4-2.5
5 ya kwamba injili yetu haikuwafikia katika maneno tu, bali na katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu, na uthibitifu mwingi; kama vile mnavyojua jinsi zilivyokuwa tabia zetu kwenu, kwa ajili yenu.
2 Thessaloniciens 2.14 Colossiens 2.2 1 Pierre 1.12 Philippiens 4.9 1 Pierre 1.3
6 Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, mkiisha kulipokea neno katika dhiki nyingi, pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu.
Actes 13.52 Galates 5.22 1 Corinthiens 11.1 Actes 17.5-17.10 1 Corinthiens 4.16
7 Hata mkawa kielelezo kwa watu wote waaminio katika Makedonia, na katika Akaya.
Tite 2.7 1 Timothée 4.12 2 Corinthiens 9.2 1 Pierre 5.3 1 Thessaloniciens 1.8
8 Maana kutoka kwenu neno la Mungu limevuma, si katika Makedonia na Akaya tu, ila na kila mahali imani yenu mliyo nayo kwa Mungu imeenea; hata hatuna haja sisi kunena lo lote.
Romains 1.8 2 Thessaloniciens 1.4 2 Thessaloniciens 3.1 Esaïe 52.7 1 Corinthiens 14.36
9 Kwa kuwa wao wenyewe wanatangaza habari zetu, jinsi kulivyokuwa kuingia kwetu kwenu; na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaziacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai, wa kweli;
1 Timothée 4.10 Galates 4.8-4.9 1 Corinthiens 12.2 Actes 14.15 Jérémie 10.10
10 na kumngojea Mwanawe kutoka mbinguni, ambaye alimfufua katika wafu, naye ni Yesu, mwenye kutuokoa na ghadhabu itakayokuja.
1 Thessaloniciens 5.9 Matthieu 3.7 Actes 2.24 1 Corinthiens 1.7 Romains 4.25

Cette Bible est dans le domaine public.