Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 32.45
Bible en Swahili de l’est


1 Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitanena; Na nchi isikie maneno ya kinywa changu.
Deutéronome 4.26 Esaïe 1.2 Deutéronome 31.28 Jérémie 6.19 Deutéronome 30.19
2 Mafundisho yangu yatadondoka kama mvua, Maneno yangu yatatona-tona kama umande; Kama manyunyu juu ya majani mabichi; Kama matone ya mvua juu ya mimea.
Esaïe 55.10-55.11 Psaumes 72.6 Michée 5.7 Job 29.22-29.23 Osée 6.4
3 Maana nitalitangaza Jina la Bwana; Mpeni ukuu Mungu wetu.
Jérémie 10.6 Deutéronome 3.24 Ephésiens 1.19 Jean 17.26 Psaumes 105.1-105.5
4 Yeye Mwamba, kazi yake ni kamilifu; Maana, njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, Yeye ndiye mwenye haki na adili.
Psaumes 18.30-18.31 Psaumes 92.15 Deutéronome 32.18 Daniel 4.37 Genèse 18.25
5 Wametenda mambo ya uharibifu, Hawawi watoto wake, hii ndiyo ila yao; Wao ni kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka.
Esaïe 1.4 Deutéronome 31.29 Matthieu 17.17 Luc 9.41 Philippiens 2.15
6 Je! Mnamlipa Bwana hivi, Enyi watu wapumbavu na ujinga? Je! Yeye siye baba yako aliyekununua? Amekufanya, na kukuweka imara.
Esaïe 63.16 Psaumes 74.2 1 Jean 3.1 Esaïe 44.2 Romains 8.15
7 Kumbuka siku za kale, Tafakari miaka ya vizazi vingi; Mwulize baba yako, naye atakuonyesha; Wazee wako, nao watakuambia.
Psaumes 44.1 Psaumes 78.3-78.4 Job 8.8-8.10 Exode 13.14 Psaumes 119.52
8 Yeye Aliye Juu alipowapa mataifa urithi wao, Alipowabagua wanadamu, Aliweka mipaka ya watu Kwa kadiri ya hesabu ya wana wa Israeli.
Actes 17.26 Genèse 10.15 Psaumes 91.1 Genèse 15.18-15.21 Genèse 11.8-11.9
9 Maana, sehemu ya Bwana ni watu wake, Yakobo ni kura ya urithi wake.
Jérémie 10.16 1 Pierre 2.9-2.10 1 Samuel 10.1 Jérémie 51.19 Exode 19.5-19.6
10 Alimkuta katika nchi ya ukame, Na katika jangwa tupu litishalo; Alimzunguka, akamtunza; Akamhifadhi kama mboni ya jicho;
Psaumes 17.8 Zacharie 2.8 Proverbes 7.2 Jérémie 2.6 Osée 13.5
11 Mfano wa tai ataharikishaye kioto chake; Na kupapatika juu ya makinda yake, Alikunjua mbawa zake, akawatwaa, Akawachukua juu ya mbawa zake;
Exode 19.4 Esaïe 31.5 Esaïe 40.31 Esaïe 46.4 Esaïe 63.9
12 Bwana peke yake alimwongoza, Wala hapakuwa na mungu mgeni pamoja naye.
Psaumes 78.52-78.53 Psaumes 78.14 Deutéronome 32.39 Esaïe 46.4 Deutéronome 1.31
13 Alimpandisha mahali pa nchi palipoinuka, Naye akala mazao ya mashamba; Akamnyonyesha asali iliyotoka jabalini, Na mafuta yaliyotoka katika mwamba wa gumegume;
Job 29.6 Esaïe 58.14 Psaumes 81.16 Ezéchiel 36.2 Deutéronome 33.26
14 Siagi ya ng’ombe, na maziwa ya kondoo, Pamoja na mafuta ya wana-kondoo, Kondoo waume wa Kibashani, na mbuzi, Na unono wa ngano iliyo nzuri; Ukanywa divai, damu ya mizabibu.
Genèse 49.11 Psaumes 81.16 Psaumes 147.14 Psaumes 22.12 Matthieu 26.28-26.29
15 Lakini Yeshuruni alinenepa, akapiga teke; Umenenepa, umekuwa mnene, umewanda; Ndipo akamwacha Mungu aliyemfanya, Akamdharau Mwamba wa wokovu wake.
Deutéronome 31.20 Deutéronome 32.4 Psaumes 89.26 Osée 13.6 Deutéronome 31.16
16 Wakamtia wivu kwa miungu migeni, Wakamkasirisha kwa machukizo.
1 Corinthiens 10.22 Psaumes 78.58 Deutéronome 7.25 1 Rois 14.22 Lévitique 18.27
17 Walitoa sadaka kwa pepo, si Mungu, Kwa miungu wasiyoijua, Kwa miungu mipya iliyotokea siku zilizo karibu, Ambayo baba zenu hawakuiogopa.
Juges 5.8 Deutéronome 28.64 Lévitique 17.7 Apocalypse 9.20 1 Timothée 4.1
18 Humkumbuki Mwamba aliyekuzaa, Mungu aliyekuzaa umemsahau.
Esaïe 17.10 Osée 8.14 Jérémie 2.32 Psaumes 106.21 Deutéronome 32.4
19 Bwana akaona, akawachukia, Kwa sababu ya kukasirishwa na wanawe na binti zake.
Psaumes 106.40 Juges 2.14 Esaïe 1.2 Psaumes 78.59 Lamentations 2.6
20 Akasema, Nitawaficha uso wangu, Nitaona mwisho wao utakuwaje; Maana, ni kizazi cha ukaidi mwingi, Watoto wasio imani ndani yao.
Deutéronome 32.5 Luc 7.31-7.32 Deutéronome 31.17-31.18 Esaïe 30.9 Jérémie 18.17
21 Wamenitia wivu kwa kisicho Mungu; Wamenikasirisha kwa ubatili wao; Nami nitawatia wivu kwa wasio watu, Nami nitawakasirisha kwa taifa lipumbaalo.
Romains 10.19 1 Rois 16.26 1 Rois 16.13 Osée 1.10 Psaumes 31.6
22 Maana, moto umewashwa kwa hasira yangu, Unateketea hata chini ya kuzimu, Unakula dunia pamoja na mazao yake, Unaunguza misingi ya milima.
Lamentations 4.11 Jérémie 15.14 Esaïe 24.19-24.20 Nombres 16.35 Jérémie 17.4
23 Nitaweka madhara juu yao chunguchungu; Nitawapiga kwa mishale yangu hata ikaishe;
Ezéchiel 5.16 Lamentations 3.13 Psaumes 7.12-7.13 Esaïe 24.17-24.18 Lévitique 26.18
24 Watakonda kwa njaa, wataliwa na makaa ya moto, Na uharibifu mkali; Nitawapelekea meno ya wanyama wakali, Pamoja na sumu ya wadudu watambaao mavumbini.
Lévitique 26.22 Ezéchiel 5.17 Amos 9.3 Esaïe 65.25 Lamentations 5.10
25 Nje upanga utawafifiliza Na ndani ya vyumba, utisho; Utaangamiza mvulana na msichana, Anyonyaye pamoja na mwenye mvi,
Ezéchiel 7.15 Lamentations 1.20 Jérémie 9.21 Esaïe 30.16 2 Corinthiens 7.5
26 Nalisema, Ningewatawanyia mbali, Ningekomesha kumbukumbu lao kati ya wanadamu;
Deutéronome 28.64 Esaïe 63.16 Psaumes 34.16 Lévitique 26.33 Lévitique 26.38
27 Isipokuwa naliogopa makamio ya adui, Adui zao wasije wakafikiri uongo, Wasije wakasema, Mkono wetu umetukuka, Wala Bwana hakuyafanya haya yote.
Psaumes 140.8 Esaïe 37.10 Lamentations 1.9 Zacharie 1.14-1.15 Ezéchiel 20.13-20.14
28 Maana hawa ni taifa wasio shauri, Wala fahamu hamna ndani yao.
Jérémie 4.22 Esaïe 27.11 Deutéronome 32.6 Matthieu 13.14-13.15 Psaumes 81.12
29 Laiti wangekuwa na akili, hata wakafahamu haya, Ili watafakari mwisho wao.
Deutéronome 5.29 Psaumes 81.13 Lamentations 1.9 Esaïe 47.7 Jérémie 17.11
30 Mmoja angefukuzaje watu elfu, Wawili wangekimbizaje elfu kumi, Kama Mwamba wao asingaliwauza, Kama Bwana asingaliwatoa?
Lévitique 26.8 Josué 23.10 Psaumes 44.12 Esaïe 30.17 Juges 2.14
31 Maana, Mwamba wao si kama Mwamba wetu, Hata adui zetu wenyewe ndivyo wahukumuvyo.
Exode 14.25 1 Samuel 2.2 1 Samuel 4.8 Esdras 1.3 Daniel 2.47
32 Maana, mzabibu wao ni mzabibu wa Sodoma, Nao ni wa mashamba ya Gomora; Zabibu zao ni zabibu za uchungu, Vichala vyao ni vichungu.
Deutéronome 29.18 Esaïe 1.10 Ezéchiel 16.45-16.51 Hébreux 12.15 Esaïe 5.4
33 Mvinyo yao ni sumu ya majoka, Uchungu mkali wa nyoka.
Psaumes 58.4 Jérémie 8.14 Job 20.14-20.16 Romains 3.13 Psaumes 140.3
34 Je! Haya hayakuwekwa akiba kwangu? Na kutiwa muhuri kati ya hazina yangu?
Job 14.17 Osée 13.12 Jérémie 2.22 Romains 2.5 Apocalypse 20.12-20.13
35 Kisasi ni changu mimi, na kulipa, Wakati itakapoteleza miguu yao; Maana siku ya msiba wao imekaribia, Na mambo yatakayowapata yatafanya haraka.
Romains 12.19 2 Pierre 2.3 Hébreux 10.30 Nahum 1.2 2 Pierre 3.8-3.10
36 Kwa kuwa Bwana atawaamua watu wake, Atawahurumia watumwa wake, Aonapo ya kuwa nguvu zao zimeondoka, Na ya kuwa habaki mtu, aliyefungwa wala asiyefungwa,
Psaumes 135.14 Psaumes 90.13 Psaumes 106.45 2 Rois 9.8 2 Rois 14.26
37 Naye atasema, Iko wapi miungu yao, Mwamba ule walioutumaini;
Jérémie 2.28 Juges 10.14 2 Rois 3.13
38 Uliokula shahamu za sadaka zao, Na kunywa divai ya sadaka zao za kinywaji? Na waondoke na kuwasaidia ninyi; Na wawe hao himaya yenu.
Ezéchiel 16.18-16.19 Sophonie 2.11 Osée 2.8 Psaumes 50.13 Juges 10.14
39 Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam, Mimi ndiye, Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi; Naua Mimi, nahuisha Mimi, Nimejeruhi, tena naponya; Wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu,
Osée 6.1 1 Samuel 2.6 Esaïe 45.5 Esaïe 45.22 Job 5.18
40 Maana, nainua mkono wangu mbinguni, Na kusema, Kama Mimi niishivyo milele,
Genèse 14.22 Hébreux 6.17-6.18 Jérémie 4.2 Apocalypse 10.5-10.6 Nombres 14.28-14.30
41 Nikiunoa upanga wangu wa umeme, Mkono wangu ukishika hukumu, Nitawatoza kisasi adui zangu, Nitawalipa wanaonichukia.
Esaïe 66.16 Esaïe 34.5-34.6 Esaïe 27.1 Psaumes 7.12 Exode 20.5
42 Nitailevya mishale yangu kwa damu, Na upanga wangu utakula nyama; Pamoja na damu ya waliouawa na waliotekwa nyara, Katika vichwa vya wakuu wa adui.
Deutéronome 32.23 Jérémie 46.10 Jérémie 46.14 Lamentations 2.5 Ezéchiel 35.6-35.8
43 Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake; Kwa maana atatwaa kisasi kwa damu ya watumwa wake, Atawatoza kisasi adui zake, Tena atafanya kafara kwa nchi yake, na watu wake.
Apocalypse 19.2 Psaumes 85.1 Apocalypse 6.10 2 Rois 9.7 Romains 12.19
44 Musa akaja akasema maneno haya yote ya wimbo huu masikioni mwa watu, yeye na Yoshua, mwana wa Nuni.
Nombres 13.8 Nombres 13.16 Deutéronome 31.30 Deutéronome 31.22
45 Musa akamaliza kuwaambia Israeli wote maneno haya yote;
46 akawaambia, Yawekeni mioyoni mwenu maneno yote ambayo nashuhudia kwenu hivi leo; nayo waamuruni watoto wenu, wayatunze na kuyafanya maneno yote ya torati hii.
Ezéchiel 40.4 1 Chroniques 22.19 Proverbes 3.1-3.4 Deutéronome 11.18 Luc 9.44
47 Kwa maana si jambo lisilofaa kwenu; maana, ni maisha yenu, na kwa jambo hili mtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu ya nchi mwivukiayo Yordani kuimiliki.
Proverbes 4.22 Lévitique 18.5 Esaïe 45.19 1 Timothée 4.8 1 Timothée 6.6-6.8

Ordre à Moïse de gravir le mont Nebo

48 Bwana akasema na Musa siku iyo hiyo, akamwambia,
Nombres 27.12-27.13
49 Kwea katika mlima huu wa Abarimu, mpaka kilima cha Nebo, kilicho katika nchi ya Moabu, kuelekea Yeriko; ukaangalie nchi ya Kanaani niwapayo wana wa Israeli kuimiliki;
Nombres 27.12 Nombres 33.47-33.48 Esaïe 33.17 2 Corinthiens 5.1 Deutéronome 34.1-34.5
50 ukafe katika kilima, huko ukweako, ukusanywe uwe pamoja na jamaa zako; kama alivyokufa nduguyo Haruni katika mlima wa Hori, akakusanywa awe pamoja na watu wake;
Genèse 25.8 Nombres 33.38 Genèse 15.15 Nombres 20.24-20.29 Genèse 49.33
51 kwa sababu mlinikosa ninyi juu yangu katikati ya wana wa Israeli katika maji ya Meriba huko Kadeshi, katika bara ya Sini; kwa kuwa hamkunitakasa katikati ya wana wa Israeli.
Nombres 27.14 1 Pierre 4.17 Esaïe 8.13 Nombres 20.11-20.14 Lévitique 10.3
52 Kwani utaiona hiyo nchi mbele yako, lakini hutakwenda huko kuingia hiyo nchi niwapayo wana wa Israeli.
Deutéronome 34.1-34.4 Hébreux 11.13 Deutéronome 3.27 Hébreux 11.39 Deutéronome 32.49

Cette Bible est dans le domaine public.