Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 27.13
Bible en Swahili de l’est


Bénédictions et malédictions

La loi au mont Ébal

1 Musa na wazee wa Israeli wakawaagiza wale watu wakawaambia, Shikeni maagizo yote niwaagizayo leo.
Deutéronome 4.1-4.3 Deutéronome 26.16 Jean 15.14 Deutéronome 11.32 1 Thessaloniciens 4.1-4.2
2 Na iwe, siku mtakayovuka Yordani kwenda nchi akupayo Bwana, Mungu wako, ujisimamishie mawe makubwa, ukayatalize matalizo,
Josué 4.1 Deutéronome 11.31 Deutéronome 27.3 Deutéronome 6.1 Ezéchiel 36.26
3 uyaandike maneno yote ya torati hii juu yake, utakapokwisha kuvuka; ili upate kuingia nchi akupayo Bwana, Mungu wako, nchi imiminikayo maziwa na asali, kama alivyokuahidi Bwana, Mungu wa baba zako.
Deutéronome 26.9 Josué 8.32 Jérémie 31.31-31.33 Deutéronome 6.8 2 Corinthiens 3.2-3.3
4 Na iwe, mtakapokwisha vuka Yordani myasimamishe mawe haya, niwaagizayo hivi leo, katika mlima Ebali, nawe yatalize matalizo.
Josué 8.30-8.33 Deutéronome 11.29-11.30
5 Na huko umjengee madhabahu Bwana, Mungu wako, madhabahu ya mawe, usitumie chombo cha chuma juu yake.
Exode 20.25 Exode 24.4 1 Rois 18.31-18.32 Josué 8.30-8.31
6 Jenga hiyo madhabahu ya Bwana, Mungu wako, kwa mawe yasiyochongwa; ukamtolee Bwana, Mungu wako, sadaka za kuteketezwa juu yake;
Ephésiens 5.2 Lévitique 1.1-1.17
7 ufanye na sadaka za amani, ukale huko; nawe furahi mbele za Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 12.7 Colossiens 1.20 Actes 10.36 Psaumes 100.1-100.2 Deutéronome 12.12
8 Kisha, andika juu ya mawe hayo maneno ya torati hii yote, waziwazi sana.
Habakuk 2.2 2 Corinthiens 3.12 Jean 16.25
9 Musa na makuhani Walawi wakawaambia Israeli wote wakasema, Nyamaza, usikize, Ee Israeli; leo umekuwa watu wa Bwana, Mungu wako.
Ephésiens 5.8-5.9 Deutéronome 26.16-26.18 Romains 6.17-6.18 1 Corinthiens 6.9-6.11 1 Pierre 2.10-2.11
10 Basi isikize sauti ya Bwana, Mungu wako, ufanye maagizo yake na amri zake nikuagizavyo leo.
Deutéronome 11.7-11.8 Deutéronome 11.1 Michée 6.8 Lévitique 19.2 1 Pierre 4.1-4.3

Bénédictions et malédictions

11 Musa akawaagiza wale watu siku iyo hiyo, akasema,
12 Hawa na wasimame juu ya mlima wa Gerizimu kwa kuwabarikia watu, mkiisha vuka Yordani; Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Yusufu, na Benyamini;
Juges 9.7 Josué 8.33-8.35 Deutéronome 11.26-11.29 Genèse 35.18 Genèse 30.24
13 na hawa na wasimame juu ya mlima wa Ebali kwa laana; Reubeni, na Gadi, na Asheri, na Zabuloni, na Dani, na Naftali.
Genèse 49.3-49.4 Deutéronome 11.29 Genèse 29.32 Deutéronome 27.4 Genèse 30.6-30.13
14 Kisha Walawi na wajibu, wawaambie watu wote wa Israeli kwa sauti kuu,
Daniel 9.11 Josué 8.33 Deutéronome 33.9-33.10 Malachie 2.7-2.9 Néhémie 8.7-8.8
15 Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina.
Exode 20.4 Exode 34.17 Lévitique 26.1 Lévitique 19.4 Deutéronome 5.8
16 Na alaaniwe amdharauye baba yake au mama yake. Na watu wote waseme, Amina.
Exode 21.17 Lévitique 19.3 Exode 20.12 Ezéchiel 22.7 Deutéronome 21.18-21.21
17 Na alaaniwe aondoaye mpaka wa jirani yake. Na watu wote waseme, Amina.
Deutéronome 19.14 Proverbes 22.28 Proverbes 23.10-23.11
18 Na alaaniwe ampotezaye kipofu akakosa njia. Na watu wote waseme, Amina.
Lévitique 19.14 Job 29.15 Matthieu 15.14 Proverbes 28.10 Esaïe 56.10
19 Na alaaniwe apotoaye hukumu ya mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe. Na watu wote waseme, Amina.
Deutéronome 10.18 Deutéronome 24.17 Michée 3.9 Psaumes 82.2-82.4 Exode 23.2
20 Na alaaniwe alalaye na mke wa baba yake, kwa kuwa amefunua mavazi ya babaye. Na watu wote waseme, Amina.
Deutéronome 22.30 Lévitique 18.8 Lévitique 20.11 1 Corinthiens 5.1 Genèse 35.22
21 Na alaaniwe alalaye na mnyama wa aina yo yote. Na watu wote waseme, Amina.
Lévitique 18.23 Lévitique 20.15 Exode 22.19
22 Na alaaniwe alalaye na umbu lake, binti ya babaye, au binti ya mamaye. Na watu wote waseme, Amina.
Lévitique 20.17 Lévitique 18.9 Ezéchiel 22.11 2 Samuel 13.8-13.14 2 Samuel 13.1
23 Na alaaniwe alalaye na mkwewe, mamaye mkewe. Na watu wote waseme, Amina.
Lévitique 20.14 Lévitique 18.17
24 Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri. Na watu wote waseme Amina.
Nombres 35.31 Lévitique 24.17 2 Samuel 20.9-20.10 Exode 21.12-21.14 2 Samuel 12.9-12.12
25 Na alaaniwe atwaaye ujira wa kumwua asiye makosa. Na watu wote waseme, Amina.
Exode 23.7-23.8 Deutéronome 10.17 Deutéronome 16.19 Psaumes 15.5 Michée 7.2-7.3
26 Na alaaniwe asiyeyaweka imara maneno ya torati hii kwa kuyafanya. Na watu wote waseme, Amina.
Galates 3.10 Psaumes 119.21 Romains 3.19-3.20 Jérémie 11.3-11.5 1 Corinthiens 16.22

Cette Bible est dans le domaine public.