Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 23.15
Bible en Swahili de l’est


1 Aliyejeruhika konde, au aliyekatika tupu yake, asiingie mtu huyo katika mkutano wa Bwana.
Galates 3.28 Néhémie 13.1-13.3 Esaïe 56.3-56.4 Deutéronome 23.2-23.3 Deutéronome 23.8

Cas d’exclusion de l’assemblée

2 Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa Bwana.
Zacharie 9.6 Esaïe 57.3 Hébreux 12.8 Jean 8.41
3 Mwamoni wala Mmoabi wasiingie katika mkutano wa Bwana; wala hata kizazi cha kumi mtu wao asiingie katika mkutano wa Bwana milele;
Néhémie 13.1-13.2 Esaïe 56.3 Ruth 4.6 Néhémie 4.3 Ruth 4.10-4.22
4 kwa sababu hapo mlipotoka Misri hawakuwalaki na chakula wala maji njiani; na kwa kuwa walimwajiri juu yako Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyo Mesopotamia, aje akuapize.
2 Pierre 2.15 Néhémie 13.2 Nombres 22.17 Genèse 14.17-14.18 Actes 9.4
5 Lakini Bwana, Mungu wako, hakukubali kumsikiza huyo Balaamu; Bwana, Mungu wako, aliyageuza yale maapizo kuwa ni baraka, kwa vile alivyokupenda Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 7.7-7.8 Romains 8.31 Ephésiens 2.4-2.5 2 Corinthiens 4.17 Nombres 23.5-23.12
6 Usitafute amani yao wala heri yao siku zako zote, milele.
Esdras 9.12 Néhémie 13.23-13.25 2 Samuel 8.2 2 Samuel 12.31
7 Usimchukie Mwedomi; kwa kuwa ni ndugu yako; usimchukie Mmisri, kwa kuwa ulikuwa mgeni katika nchi yake.
Deutéronome 10.19 Exode 22.21 Lévitique 19.34 Exode 23.9 Genèse 25.24-25.26
8 Wana wao watakaozaliwa kizazi cha tatu na waingie katika mkutano wa Bwana.
Deutéronome 23.1-23.3 Exode 20.5-20.6 Romains 3.29-3.30 Ephésiens 2.12-2.13
9 Utakapotoka kwenda juu ya adui zako nawe u katika marago, jilinde na kila neno baya.
Josué 6.18 Juges 20.26 2 Chroniques 31.20-32.22 Josué 7.11-7.13 2 Chroniques 19.4

Règles liées à la pureté

10 Akiwa kwenu mtu awaye yote asiyekuwa ni tohara kwa ajili ya yaliyomtukia usiku, na atoke nje ya kituo, wala asiingie ndani ya kituo;
Lévitique 15.16 Nombres 5.2-5.3 1 Corinthiens 5.11-5.13
11 lakini na iwe ikaribiapo jioni, yeye ataoga maji; na jua likiisha kuchwa ataingia ndani ya kituo.
Ephésiens 5.26-5.27 Lévitique 14.9 Lévitique 15.5 Hébreux 10.22 Luc 11.38-11.39
12 Tena uwe na mahali nje ya kituo, kwa kutokea nje;
13 nawe uwe na jembe dogo katika silaha zako; napo uotamapo nje uchimbe kwa lile jembe, na kugeuka na kukifunika kikutokacho;
Ezéchiel 24.6-24.8
14 kwa kuwa Bwana. Mungu wako, yuatembea katika kituo akuokoe, na kukutolea adui zako mbele yako; kwa hiyo na kiwe kitakatifu kituo chako; asije akaona kitu kwako kisichokuwa safi, akageuka na kukuacha.
Lévitique 26.12 Genèse 17.1 2 Corinthiens 6.16 Exode 3.5
15 Usimrudishe kwa bwana wake mtumwa aliyejiponya kutoka kwa bwana wake kuja kwako;
1 Samuel 30.15 Abdias 1.14
16 na akae nawe, katikati yako, ndani ya malango yako mojawapo, mahali atakapochagua palipo pema machoni pake; usimwonee.
Exode 22.21 Exode 23.9 Luc 15.15-15.24 Malachie 3.5 Jérémie 7.6
17 Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume.
2 Rois 23.7 Lévitique 19.29 1 Rois 14.24 1 Timothée 1.10 Deutéronome 22.21
18 Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.
Deutéronome 23.21 Apocalypse 22.15 Lévitique 18.22 Matthieu 7.6 Philippiens 3.2
19 Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;
Exode 22.25 Psaumes 15.5 Lévitique 25.35-25.37 Luc 6.34-6.35 Néhémie 5.1-5.7
20 mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki.
Deutéronome 15.10 Deutéronome 15.3 Deutéronome 14.21 1 Corinthiens 15.58 Deutéronome 28.12
21 Utakapoweka nadhiri kwa Bwana, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako.
Ecclésiaste 5.4-5.5 Deutéronome 23.18 Psaumes 76.11 Psaumes 66.13-66.14 Jonas 1.16

Les vœux

22 Lakini ukijizuia usiweke nadhiri, haitakuwa dhambi kwako.
23 Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako.
Juges 11.35 Ecclésiaste 5.4-5.5 1 Samuel 14.24 Jérémie 44.25-44.27 Actes 23.21
24 Uingiapo katika shamba la mizabibu la jirani yako, utaweza kula zabibu za kukushibisha, kama upendavyo; ila usitie katika chombo chako.
1 Corinthiens 10.26 Hébreux 13.5 Romains 12.13
25 Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako.
Marc 2.23 Luc 6.1-6.2 Matthieu 12.1-12.2

Cette Bible est dans le domaine public.