Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 22.4
Bible en Swahili de l’est


1 Umwonapo ng’ombe wa nduguyo au kondoo wake akipotea, usijifiche kama usiyemwona; sharti utamrudisha kwa nduguyo.
Exode 23.4-23.5 Deutéronome 22.3-22.4 Esaïe 8.17 Esaïe 58.7 Matthieu 10.6
2 Na kwamba yule nduguyo hayupo karibu nawe, au ukiwa humjui, umchukue kwenu nyumbani kwako, uwe naye hata aje nduguyo kumtafuta, nawe mrudishie.
1 Thessaloniciens 4.6 Matthieu 7.12
3 Tena fanya vivyo kwa punda wake; tena fanya vivyo kwa mavazi yake; tena fanya vivyo kwa kila kitu kilichopotea cha nduguyo, kilichompotea ukakiona wewe; usijifiche kama usiyekiona.
4 Umwonapo punda wa nduguyo, au ng’ombe wake, ameanguka kando ya njia, usijifiche kama usiyemwona; sharti umsaidie kumwinua tena.
Matthieu 5.44 Galates 6.1-6.2 Romains 15.1 Luc 10.29-10.37 1 Thessaloniciens 5.14
5 Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako.
1 Corinthiens 11.4-11.15 Deutéronome 18.12
6 Kiota cha ndege kikitukia kuwa mbele yako njiani, katika mti wo wote, au chini, chenye makinda au mayai, naye koo ameatamia juu ya makinda, au juu ya mayai, usimtwae yule koo pamoja na makinda;
Lévitique 22.28 Genèse 32.11 Luc 12.6 Proverbes 12.10 Genèse 8.17
7 sharti umwache yule koo aende zake, lakini makinda waweza kuyatwaa uwe nayo; ili upate kufanikiwa, ufanye siku zako kuwa nyingi.
Deutéronome 4.40 Proverbes 22.4
8 Utakapojenga nyumba mpya, fanya ukuta kando-kando ya dari lako, usije ukaleta damu juu ya nyumba yako, mtu akianguka huko.
Actes 10.9 Jérémie 19.13 2 Samuel 11.2 Matthieu 10.27 Marc 2.4
9 Usipande shamba lako la mizabibu aina mbili za mbegu; yasije yakaondolewa matunda yote, mbegu ulizopanda na maongeo ya mizabibu yako.
Lévitique 19.19 2 Corinthiens 11.3 2 Corinthiens 1.12 Romains 11.6 Jacques 3.10
10 Usilime kwa ng’ombe na punda wakikokota jembe pamoja.
2 Corinthiens 6.14-6.16
11 Usivae nguo iliyochanganyikana sufu na kitani pamoja.
Lévitique 19.19
12 Ujifanyizie vishada katika pembe nne za mavazi yako ya kujifunika.
Matthieu 23.5 Nombres 15.37-15.41
13 Mtu akitwaa mke, akamwingilia na kumchukia,
Genèse 29.21 Juges 15.1-15.2 Ephésiens 5.28-5.29 Deutéronome 24.1 Genèse 29.23
14 kisha akamshitaki mambo ya aibu kumzushia jina baya, akasema, Nimemtwaa mwanamke huyu, nami nilipomkaribia sikuona kwake alama za ubikira;
Proverbes 18.8 1 Timothée 5.14 Deutéronome 22.19 Exode 20.16 Proverbes 18.21
15 ndipo babaye yule kijana na mamaye watakapotwaa alama za yule kijana za ubikira, wawatolee wazee wa mji langoni;
16 na baba yake yule kijana awaambie wazee, Mwanamume huyu nilimpa binti yangu awe mkewe, naye amchukia;
17 angalieni, amemwekea mambo ya aibu, asema, Sikuona kwa binti yako alama za ubikira, nazo hizi ndizo alama za binti yangu za ubikira. Na wayakunjue yale mavazi mbele ya wazee wa mji.
18 Basi wazee wa mji ule na wamtwae yule mtu mume na kumrudi,
Exode 18.21
19 wamtoze shekeli mia za fedha, wampe babaye yule kijana, kwa kuwa amemzulia jina baya mwanamwali wa Israeli; naye awe mkewe; hana ruhusa ya kumwacha siku zake zote.
Matthieu 19.8-19.9 Deutéronome 22.29 Deutéronome 24.1-24.4
20 Lakini likiwa ni kweli neno hili, la kutoonekana kwake yule kijana alama za ubikira;
21 na wamtoe nje yule kijana mlangoni pa nyumba ya baba yake, na waume wa mji wake wampige kwa mawe hata afe; kwa vile alivyofanya upumbavu katika Israeli, kwa kufanya ukahaba katika nyumba ya baba yake; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.
Genèse 34.7 Deutéronome 13.5 Juges 20.6 Lévitique 21.9 Deutéronome 17.7
22 Akifumaniwa mtu mume amelala na mwanamke aliyeolewa na mume, na wafe wote wawili, mtu mume aliyelala na mwanamke, na yule mwanamke naye; ndivyo utakavyoondoa uovu katika Israeli.
Lévitique 20.10 Hébreux 13.4 Ezéchiel 16.38 Ezéchiel 23.45-23.47 Jean 8.4-8.5
23 Pakiwa na kijana aliye mwanamwali ameposwa na mume, na mwanamume akimkuta mjini, akalala naye;
Matthieu 1.18-1.19 Deutéronome 20.7
24 watoeni nje katika lango la mji ule, mkawapige kwa mawe hata wafe; yule kijana, kwa kuwa hakupiga ukelele, naye yu ndani ya mji; na yule mume, kwa kuwa amemtweza mke wa mwenzake; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.
1 Corinthiens 5.13 Deutéronome 21.14 Deutéronome 22.21-22.22 Genèse 29.21 Deutéronome 13.5
25 Lakini yule mtu mume kama akimkuta kondeni kijana aliyeposwa, naye mume akamtenza nguvu, akalala naye; yule mtu mume aliyelala naye na afe pekee;
2 Samuel 13.14
26 lakini yule kijana usimfanye neno; hana dhambi yule kijana ipasayo kuuawa, kwa kuwa ni mfano wa mtu kumwondokea mwenzake akamwua, ni vivyo lilivyo jambo hili;
Deutéronome 21.22
27 kwani alimkuta kondeni; yule kijana aliyeposwa akalia, pasiwe na mtu wa kumwokoa.
1 Corinthiens 13.7
28 Mtu mume akimwona kijana aliye mwanamwali ambaye hajaposwa, akamshika na kulala naye, wakaonekana;
Exode 22.16-22.17
29 yule mtu mume aliyelala naye na ampe baba yake yule kijana shekeli hamsini za fedha, kisha na awe mkewe, kwa kuwa amemtweza; hana ruhusa ya kumwacha siku zake zote.
Deutéronome 22.19 Deutéronome 22.24 Deutéronome 21.14
30 Mtu mume asimtwae mke wa baba yake, wala asifunue ncha ya mavazi ya baba yake.
Deutéronome 27.20 Lévitique 18.8 1 Corinthiens 5.1 Lévitique 20.11 Ruth 3.9

Cette Bible est dans le domaine public.