Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 1.23
Bible en Swahili de l’est


Une justice obtenue par la foi

Salutation et louange

1 Paulo, mtumwa wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa aihubiri Injili ya Mungu;
Romains 15.16 Actes 9.15 1 Corinthiens 1.1 2 Corinthiens 1.1 Romains 1.9
2 ambayo Mungu amekwisha kuiahidi kwa kinywa cha manabii wake katika maandiko matakatifu;
Tite 1.2 Luc 1.70 Romains 3.21 Romains 3.2 Romains 16.26
3 yaani, habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili,
Matthieu 1.1 Galates 4.4 Jean 1.14 Jérémie 23.5-23.6 Romains 9.5
4 na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu;
1 Pierre 1.11 Hébreux 9.14 Hébreux 5.5-5.6 2 Corinthiens 13.4 Ephésiens 1.19-1.23
5 ambaye katika yeye tulipokea neema na utume ili mataifa yote wapate kujitiisha kwa imani, kwa ajili ya jina lake;
Actes 6.7 Romains 16.26 Actes 9.15 Romains 12.3 1 Corinthiens 15.10
6 ambao katika hao ninyi mmekuwa wateule wa Yesu Kristo;
Apocalypse 17.14 Hébreux 3.1 2 Pierre 1.10 1 Pierre 2.21 2 Thessaloniciens 2.14
7 kwa wote walioko Rumi, wapendwao na Mungu, walioitwa kuwa watakatifu. Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.
Colossiens 1.2 Ephésiens 1.2 2 Corinthiens 13.14 Jude 1.1-1.2 1 Thessaloniciens 1.1
8 Kwanza namshukuru Mungu wangu katika Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa kuwa imani yenu inahubiriwa katika dunia nzima.
Romains 16.19 1 Corinthiens 1.4 Philippiens 1.3 Romains 6.17 1 Pierre 4.11
9 Kwa maana Mungu, nimwabuduye kwa roho yangu katika Injili ya Mwana wake, ni shahidi wangu jinsi niwatajavyo pasipo kukoma,
2 Timothée 1.3 Romains 9.1 2 Corinthiens 1.23 Ephésiens 6.18 1 Thessaloniciens 5.17
10 siku zote katika sala zangu, nikiomba nije kwenu hivi karibu, Mungu akipenda kuifanikisha safari yangu.
Actes 18.21 1 Thessaloniciens 2.18 Actes 19.21 1 Thessaloniciens 3.10-3.11 Romains 15.22-15.24
11 Kwa maana ninatamani sana kuwaona, nipate kuwapa karama ya rohoni, ili mfanywe imara;
Romains 15.23 Actes 19.6 Romains 15.29 Actes 8.15-8.19 Romains 16.25
12 yaani, tufarijiane mimi na ninyi, kila mtu kwa imani ya mwenzake, yenu na yangu.
1 Thessaloniciens 3.7-3.10 Romains 15.32 3 Jean 1.3-1.4 2 Pierre 1.1 Actes 11.23
13 Lakini, ndugu zangu, sipendi msiwe na habari, ya kuwa mara nyingi nalikusudia kuja kwenu, nikazuiliwa hata sasa, ili nipate kuwa na matunda kwenu ninyi pia kama nilivyo nayo katika Mataifa wengine.
Actes 19.21 Philippiens 4.17 Jean 4.36 1 Thessaloniciens 2.18 1 Corinthiens 10.1
14 Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani, nawiwa na wenye hekima na wasio na hekima.
Colossiens 3.11 1 Corinthiens 9.16-9.23 1 Corinthiens 14.11 Ephésiens 5.15-5.17 1 Corinthiens 3.18
15 Kwa hiyo, kwa upande wangu, mimi ni tayari kuihubiri Injili hata na kwenu ninyi mnaokaa Rumi.
Jean 4.34 Esaïe 6.8 1 Corinthiens 9.17 Romains 15.20 Actes 21.13
16 Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
Marc 8.38 2 Timothée 1.8 Psaumes 40.9-40.10 2 Timothée 1.12 1 Pierre 4.16
17 Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani.
Galates 3.11 Habakuk 2.4 Romains 3.21 Philippiens 3.9 Hébreux 10.38

Culpabilité des non-Juifs

18 Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.
Ephésiens 5.6 Colossiens 3.6 Romains 1.32 2 Thessaloniciens 2.10 1 Timothée 4.1-4.2
19 Kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu aliwadhihirishia.
Actes 14.16-14.17 Romains 1.20 Actes 17.23-17.30 Psaumes 19.1-19.6 Esaïe 40.26
20 Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru;
Esaïe 40.26 Psaumes 19.1-19.6 1 Timothée 1.17 Romains 1.19 Psaumes 8.3
21 kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.
Jérémie 2.5 Ephésiens 4.17-4.18 2 Rois 17.15 Apocalypse 15.4 Psaumes 50.23
22 Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika;
Jérémie 10.14 1 Corinthiens 3.18-3.19 1 Corinthiens 1.19-1.21 Proverbes 25.14 Esaïe 47.10
23 wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo.
Jérémie 2.11 Psaumes 106.20 Actes 17.29 Esaïe 44.13 Apocalypse 9.20
24 Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.
Ephésiens 4.18-4.19 1 Thessaloniciens 4.4 Romains 1.26-1.28 Romains 6.12 2 Timothée 2.20-2.22
25 Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina.
Esaïe 44.20 Romains 9.5 Habakuk 2.18 Amos 2.4 Jérémie 16.19
26 Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili;
Jude 1.7 Genèse 19.5 1 Timothée 1.10 Lévitique 18.22-18.28 1 Corinthiens 6.9
27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.
Lévitique 20.13 Lévitique 18.22 Romains 1.23-1.24
28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.
Romains 1.21 Jérémie 9.6 Romains 1.24 2 Thessaloniciens 2.10-2.12 Tite 1.16
29 Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,
2 Corinthiens 12.20 Romains 3.10 Proverbes 16.28 Psaumes 41.7 Proverbes 26.20
30 wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao,
2 Timothée 3.2 Luc 21.16 Jacques 3.5 Matthieu 15.4 1 Rois 20.11
31 wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;
2 Timothée 3.3 Esaïe 27.11 Jérémie 4.22 Proverbes 18.2 Matthieu 15.16
32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.
Romains 6.21 Romains 1.21 Romains 1.18 Psaumes 50.18 Actes 22.20

Cette Bible est dans le domaine public.