Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 25.6
Bible en Swahili de l’est


Parabole des dix jeunes filles

1 Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.
Luc 12.35-12.36 Apocalypse 19.7 Matthieu 13.24 Apocalypse 21.2 Matthieu 22.2
2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.
Jérémie 24.2 Matthieu 7.24-7.27 1 Jean 2.19 Jude 1.5 1 Corinthiens 10.1-10.5
3 Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;
Esaïe 48.1-48.2 Esaïe 58.2 Hébreux 12.15 Apocalypse 3.1 Matthieu 23.25-23.26
4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.
Jean 3.34 1 Jean 2.20 1 Jean 2.27 Romains 8.9 2 Corinthiens 1.22
5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.
Matthieu 25.19 Matthieu 24.48 Habakuk 2.3 Jonas 1.5-1.6 Luc 12.45
6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.
2 Thessaloniciens 1.7-1.10 Marc 13.33-13.37 Matthieu 25.1 2 Pierre 3.10 Jude 1.14-1.15
7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
Apocalypse 3.19-3.20 Luc 12.35 Apocalypse 3.2 Apocalypse 2.4-2.5 2 Pierre 3.14
8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.
Luc 12.35 Matthieu 13.20-13.21 Hébreux 4.1 Proverbes 4.18-4.19 Proverbes 20.20
9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.
Ezéchiel 14.20 Psaumes 49.7-49.9 Esaïe 55.1-55.3 Esaïe 55.6-55.7 Actes 8.22
10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
Luc 13.25 Apocalypse 22.20 Apocalypse 22.11-22.12 Psaumes 95.11 Matthieu 25.6
11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.
Matthieu 7.21-7.23 Hébreux 12.16-12.17
12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.
2 Timothée 2.19 Luc 13.26-13.30 Psaumes 5.5 Jean 10.27 Galates 4.9
13 Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.
Marc 13.33-13.37 Matthieu 24.42-24.44 1 Corinthiens 16.13 1 Thessaloniciens 5.6 1 Pierre 5.8

Parabole des serviteurs et des récompenses

14 Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake.
Matthieu 21.33 1 Corinthiens 3.5 1 Pierre 4.9-4.11 Marc 13.34 Luc 19.12-19.27
15 Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri.
Matthieu 18.24 Luc 19.13-19.14 Luc 12.48
16 Mara yule aliyepokea talanta tano akaenda, akafanya biashara nazo, akachuma faida talanta nyingine tano.
Esaïe 23.18 2 Chroniques 31.20-31.21 Esaïe 60.5-60.16 Néhémie 5.14-5.19 2 Chroniques 1.9-1.10
17 Vile vile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida.
Job 29.11-29.17 2 Samuel 19.32 Colossiens 4.17 Hébreux 6.10-6.11 2 Corinthiens 8.12
18 Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake.
Aggée 1.2-1.4 Proverbes 18.9 Malachie 1.10 2 Pierre 1.8 Hébreux 6.12
19 Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.
Matthieu 25.5 Luc 16.1-16.2 Jacques 3.1 Matthieu 24.48 Romains 14.7-14.12
20 Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida.
Luc 19.16-19.17 Jacques 2.18 1 Corinthiens 15.10 2 Timothée 4.1-4.8 Colossiens 1.29
21 Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.
Luc 16.10 Matthieu 25.23 Jean 12.26 2 Timothée 2.12 Apocalypse 3.21
22 Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida.
2 Corinthiens 8.12 Romains 12.6-12.8 Luc 19.18-19.19 2 Corinthiens 8.7-8.8 2 Corinthiens 8.1-8.3
23 Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.
Matthieu 25.21 Marc 14.8-14.9 Marc 12.41-12.44
24 Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;
Jérémie 44.16-44.18 Matthieu 20.12 Matthieu 7.21 Job 21.14-21.15 Ezéchiel 18.25-18.29
25 basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako.
Apocalypse 21.8 Romains 8.15 Proverbes 26.13 2 Samuel 6.9-6.10 2 Timothée 1.6-1.7
26 Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;
Matthieu 18.32 Job 15.5-15.6
27 basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.
Romains 3.19 Deutéronome 23.19-23.20 Luc 19.22-19.23 Jude 1.15
28 Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.
Luc 10.42 Luc 19.24
29 Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa.
Matthieu 13.12 Marc 4.25 Luc 8.18 Jean 15.2 Jean 11.48
30 Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Matthieu 8.12 Matthieu 22.13 Hébreux 6.7-6.8 Apocalypse 3.15-3.16 Matthieu 13.50

Jugement des nations

31 Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;
Matthieu 19.28 Marc 8.38 1 Thessaloniciens 4.16 Matthieu 16.27 2 Thessaloniciens 1.7-1.8
32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;
Matthieu 13.49 Malachie 3.18 2 Corinthiens 5.10 Psaumes 98.9 Ezéchiel 34.17-34.22
33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.
Psaumes 100.3 Psaumes 45.9 Ephésiens 1.20 Psaumes 95.7 Jean 10.26-10.28
34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;
Apocalypse 21.7 Jacques 2.5 Luc 12.32 Apocalypse 13.8 Galates 5.21
35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;
Ezéchiel 18.7 1 Jean 3.16-3.19 Ezéchiel 18.16 Romains 12.13 Deutéronome 15.7-15.11
36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.
Jacques 1.27 Jacques 5.14-5.15 Hébreux 13.3 Hébreux 10.34 Actes 20.35
37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?
1 Pierre 5.5-5.6 Matthieu 6.3 1 Corinthiens 15.10 1 Chroniques 29.14 Esaïe 64.6
38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?
39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?
40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.
Proverbes 19.17 Matthieu 10.42 Proverbes 14.31 Marc 9.41 1 Jean 4.7-4.12
41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;
Jude 1.6-1.7 Matthieu 13.40 2 Pierre 2.4 Matthieu 7.23 Matthieu 3.12
42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;
Matthieu 10.37-10.38 2 Thessaloniciens 1.8 Jean 14.21 1 Corinthiens 16.22 1 Jean 4.20
43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.
44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?
Malachie 2.17 Matthieu 25.24-25.27 Matthieu 7.22 1 Samuel 15.20-15.21 Luc 10.29
45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.
Matthieu 25.40 Proverbes 14.31 Proverbes 17.5 Psaumes 105.15 Actes 9.5
46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.
Jean 3.36 Daniel 12.2 Romains 6.23 Jean 5.29 Apocalypse 21.8

Cette Bible est dans le domaine public.