Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 11.11
Bible en Swahili de l’est


Révoltes d’Israël dans le désert

Le feu de l’Éternel à Tabeéra

1 Kisha hao watu walikuwa kama wanung’unikao, wakinena maovu masikioni mwa Bwana; Bwana aliposikia hayo, hasira zake zikawaka; na moto wa Bwana ukawaka kati yao, ukateketeza katika mipaka ya mwisho wa marago.
Lévitique 10.2 Deutéronome 9.22 Nombres 21.5 Nombres 16.35 Psaumes 78.21
2 Ndipo watu wakamlilia Musa; naye Musa akamwomba Bwana, na ule moto ukakoma.
Nombres 21.7 Jacques 5.16 Nombres 16.45-16.48 Genèse 18.23-18.33 Jérémie 42.2
3 Jina la mahali hapo likaitwa Tabera; kwa sababu huo moto wa Bwana ukawaka kati yao.
Deutéronome 9.22

Israël réclame de la viande

4 Kisha mkutano wa wafuasi waliokuwa kati yao, wakashikwa na tamaa; wana wa Israeli nao wakalia tena, wakasema, N’nani atakayetupa nyama tule?
Exode 12.38 1 Corinthiens 10.6 Psaumes 106.14 Romains 13.14 Néhémie 13.3
5 Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu;
Exode 16.3 Psaumes 17.14 Philippiens 3.19
6 lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu cho chote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hii mana tu.
Nombres 21.5 2 Samuel 13.4
7 Na hiyo mana ilikuwa mfano wa chembe za mtama na kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwake bedola.
Exode 16.31 Genèse 2.12 1 Corinthiens 1.23-1.24 Apocalypse 2.17 Exode 16.14-16.15
8 Watu wakazunguka-zunguka na kuikusanya, kisha wakaisaga kwa mawe ya kusagia, au kuitwanga katika vinu, kisha wakaitokosa nyunguni, na kuandaa mikate; na tamu yake ilikuwa kama tamu ya mafuta mapya.
Exode 16.16-16.18 Exode 16.31 Jean 6.27 Jean 6.33-6.58 Exode 16.23
9 Umande ulipoyaangukia marago wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao.
Exode 16.13-16.14 Psaumes 105.40 Deutéronome 32.2 Psaumes 78.23-78.25
10 Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za Bwana zikawaka sana; Musa naye akakasirika.
Psaumes 139.21 Deutéronome 32.22 Marc 10.14 Nombres 14.1-14.2 Psaumes 78.59
11 Musa akamwambia Bwana, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu?
Deutéronome 1.12 2 Corinthiens 11.28 Exode 17.4 Lamentations 3.39-3.40 Malachie 3.14
12 Je! Ni mimi niliyewatungisha mimba watu hawa wote je! Ni mimi niliyewazaa, hata ikawa wewe kuniambia, Haya, wachukue kifuani mwako, mfano wa baba mwenye kulea achukuavyo mtoto anyonyaye, uende nao mpaka nchi uliyowaapia baba zao?
Exode 13.5 Esaïe 49.23 Esaïe 40.11 1 Thessaloniciens 2.7 Genèse 50.24
13 Nipate wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? Kwani wanililia, wakisema Tupe nyama, tupate kula.
Matthieu 15.33 Marc 8.4 Marc 9.23 Jean 6.5-6.9
14 Mimi siwezi kuwachukua watu hawa wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda.
Exode 18.18 Esaïe 9.6 Deutéronome 1.9-1.12 2 Corinthiens 2.16 Psaumes 89.19
15 Na kama ukinitenda hivi, nakuomba uniulie mbali, kwamba nimepata fadhili mbele ya macho yako; nami nisiyaone haya mashaka yangu.
Jonas 4.3 1 Rois 19.4 Sophonie 3.15 Jonas 4.8-4.9 Job 7.15
16 Kisha Bwana akamwambia Musa, Nikusanyie watu sabini, miongoni mwa wazee wa israeli, ambao wewe wawajua kuwa ndio wazee wa watu hawa, na maakida juu yao; ukawalete hata hema ya kukutania, wasimame huko pamoja nawe.
Exode 24.1 Exode 24.9 Deutéronome 1.15 Deutéronome 16.18 Luc 10.17
17 Nami nitashuka niseme nawe huko, nami nitatwaa sehemu ya roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao; nao watachukua mzigo wa watu hawa pamoja nawe, ili usiuchukue wewe peke yako.
Nombres 11.25 2 Rois 2.9 1 Samuel 10.6 Joël 2.28 Romains 8.9
18 Kisha uwaambie watu hawa, Jitakaseni nafsi zenu kabla ya kesho, nanyi mtakula nyama; kwa maana mmelia masikioni mwa Bwana, mkisema, Ni nani atakayetupa nyama, tule? Maana huko Misri tulikuwa na uheri. Basi kwa sababu hiyo Bwana atawapa nyama, nanyi mtakula.
Exode 19.10 Actes 7.39 Nombres 11.1 Genèse 35.2 Juges 21.2
19 Hamtakula siku moja, wala siku mbili, wala siku tano, wala siku kumi, wala siku ishirini;
20 lakini mtakula muda wa mwezi mzima, hata hapo nyama hiyo itakapotoka katika mianzi ya pua zenu, nanyi mtaikinai, kwa sababu mmemkataa Bwana aliye kati yenu, na kulia mbele zake, mkisema, Tulitoka Misri kwa maana gani?
Psaumes 106.15 Nombres 21.5 Actes 13.41 Exode 16.13 Josué 24.27
21 Musa akasema, Watu hawa ambao mimi ni kati yao, ni watu sita mia elfu waendao kwa miguu; nawe umesema, Nitawapa nyama, ili wale muda wa mwezi mzima.
Exode 12.37 Nombres 1.46 Exode 38.26 Genèse 12.2 Nombres 2.32
22 Je! Makundi ya kondoo na ng’ombe yatachinjwa kwa ajili yao, ili kuwatosha? Au samaki wote wa baharini watakusanywa pamoja kwa ajili yao, ili kuwatosha?
Matthieu 15.33 Jean 6.6-6.7 Luc 1.18 Luc 1.34 Marc 8.4
23 Bwana akamwambia Musa, Je! Mkono wa Bwana umepungua urefu wake? Sasa utaona kwamba neno langu litatimizwa kwako, au sivyo.
Esaïe 59.1 Esaïe 50.2 Ezéchiel 12.25 Ezéchiel 24.14 Nombres 23.19
24 Musa akatoka, akawaambia watu maneno ya Bwana; akawakutanisha watu sabini miongoni mwa wazee wa watu, akawaweka kuizunguka Hema.
Nombres 11.16 Nombres 11.26
25 Ndipo Bwana akashuka ndani ya wingu, akanena naye, akatwaa sehemu ya roho iliyokuwa juu ya Musa, akaitia juu ya wale wazee sabini; ikawa, roho hiyo ilipowashukia, wakatabiri, lakini hawakufanya hivyo tena.
Nombres 11.17 Nombres 12.5 1 Samuel 10.10 1 Samuel 19.20-19.24 2 Rois 2.15
26 Lakini watu wawili walisalia kambini, jina la mmoja aliitwa Eldadi, na jina la wa pili aliitwa Medadi; na roho ile ikawashukia; nao walikuwa miongoni mwao walioandikwa, lakini walikuwa hawakutoka kwenda hemani; nao wakatabiri kambini.
Jérémie 36.5 1 Samuel 10.22 Exode 4.13-4.14 Exode 3.11 Jérémie 1.6
27 Mtu mmoja kijana akapiga mbio, akaenda akamwambia Musa, akasema, Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.
28 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa tangu ujana wake, akajibu akasema, Ee bwana wangu Musa, uwakataze.
Jean 3.26 Luc 9.49-9.50 Josué 1.1 Marc 9.38-9.40 Exode 33.11
29 Musa akamwambia, Je! Umekuwa na wivu kwa ajili yangu; ingekuwa heri kama watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kama Bwana angewatia roho yake.
1 Corinthiens 14.5 Jacques 5.9 Philippiens 2.3 1 Corinthiens 3.3 Matthieu 9.37-9.38
30 Kisha Musa akaenda akaingia kambini, yeye na wale wazee wa Israeli.
31 Kisha upepo ukavuma kutoka kwa Bwana, nao ukaleta kware kutoka pande za baharini, nao ukawaacha wakaanguka karibu na kambi, kama kiasi cha mwendo wa siku moja upande huu, na kama kiasi cha mwendo wa siku moja upande huu, kuizunguka, nao wakafikilia kiasi cha dhiraa mbili juu ya uso wa nchi.
Exode 16.13 Psaumes 105.40 Psaumes 78.26-78.29 Psaumes 135.7 Exode 10.13
32 Watu wakaondoka mchana huo wote, na usiku huo wote, na siku ya pili yote, kuwakusanya hao kware; yeye aliyepata ya upungufu kuliko wenziwe alipata kiasi cha homeri kumi; nao wakawaanika wote kando-kando ya kambi kuizunguka pande zote.
Ezéchiel 45.11 Exode 16.36
33 Kisha hapo hiyo nyama ilipokuwa ikali kati ya meno yao, hawajaitafuna bado, hasira za Bwana ziliwaka juu ya watu, Bwana akawapiga watu kwa pigo kuu mno.
Psaumes 78.30-78.31 Psaumes 106.14-106.15 Nombres 25.9 Nombres 16.49 Deutéronome 28.27
34 Jina la mahali pale likaitwa Kibroth-hataava; maana, ni hapo walipowazika hao watu waliotamani.
Deutéronome 9.22 1 Corinthiens 10.6 Nombres 33.16
35 Kutoka hapo Kibroth-hataava watu wakasafiri kwenda Haserothi; wakakaa huko Haserothi.
Nombres 33.17 Nombres 12.16 Deutéronome 1.1

Cette Bible est dans le domaine public.