Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 1.31
Bible en Swahili de l’est


L’organisation d’Israël dans le désert

Recensement des Israélites

1 Bwana akanena na Musa katika bara ya Sinai, hemani mwa kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya kutoka kwao nchi ya Misri, akamwambia,
Exode 19.1 Exode 25.22 Nombres 10.11-10.12 Exode 40.17
2 Fanyeni hesabu ya mkutano wote wa wana wa Israeli, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina ilivyo, kila mtu mume kichwa kwa kichwa;
Exode 30.12 Exode 38.26 Nombres 1.18 Nombres 1.22 Nombres 26.2-26.4
3 tangu mwenye miaka ishirini umri wake, na zaidi, wote wawezao kutoka kwenenda vitani katika Israeli; wewe na Haruni mtawahesabu kwa kuandama majeshi yao.
Exode 30.14 Nombres 14.29 Deutéronome 3.18 Nombres 26.2 2 Chroniques 17.13-17.18
4 Tena mtu mume mmoja wa kila kabila atakuwa pamoja nanyi; kila mmoja aliye kichwa cha nyumba ya baba zake.
Nombres 1.16 Exode 18.25 Josué 22.14 Exode 18.21 Nombres 10.14-10.27
5 Na majina ya hao waume watakaosimama pamoja nanyi ni haya; Wa Reubeni; Elisuri mwana wa Shedeuri.
Nombres 7.30 Deutéronome 33.1-33.29 Nombres 2.10 Genèse 30.5-30.20 Genèse 46.8-46.24
6 Wa Simeoni; Shelumieli mwana wa Suri-shadai.
Nombres 7.36 Nombres 2.12
7 Wa Yuda; Nashoni mwana wa Aminadabu.
Luc 3.32 1 Chroniques 2.10-2.11 Matthieu 1.2-1.5 Nombres 7.12 Nombres 10.14
8 Wa Isakari; Nethaneli mwana wa Suari.
Nombres 7.18 Nombres 2.5 Nombres 10.15
9 Wa Zabuloni; Eliabu mwana wa Heloni.
Nombres 7.24 Nombres 10.16 Nombres 2.7
10 Katika wana wa Yusufu; wa Efraimu, Elishama mwana wa Amihudi; na wa Manase; Gamalieli mwana wa Pedasuri.
Nombres 7.48 Nombres 7.54 Nombres 2.18 Nombres 2.20 Nombres 10.22-10.23
11 Wa Benyamini Abidani mwana wa Gideoni.
Nombres 7.60 Nombres 2.22 Nombres 10.24
12 Wa Dani; Ahiezeri mwana wa Amishadai.
Nombres 7.66 Nombres 2.25 Nombres 10.25
13 Wa Asheri; Pagieli mwana wa Okirani.
Nombres 7.72 Nombres 2.27 Nombres 10.26
14 Wa Gadi; Eliasafu mwana wa Deueli.
Nombres 2.14 Nombres 7.42 Nombres 10.20
15 Wa Naftali; Ahira mwana wa Enani.
Nombres 7.78 Nombres 10.27 Nombres 2.29
16 Hao ndio walioitwa wa mkutano, wakuu wa kabila za baba zao; nao ndio vichwa vya wale maelfu ya Israeli.
Nombres 7.2 Exode 18.25 Exode 18.21 Nombres 26.9 Nombres 16.2
17 Basi Musa na Haruni wakawatwaa hao watu waume waliotajwa majina yao;
Nombres 1.5-1.15 Apocalypse 7.4-7.17 Jean 10.3
18 nao waliukutanisha mkutano mzima, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, nao wakaonyesha ukoo wa vizazi vyao kwa kuandama jamaa zao, kwa nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, kichwa kwa kichwa.
Esdras 2.59 Hébreux 7.3 Hébreux 7.6 Néhémie 7.61 Nombres 1.1
19 Kama Bwana alivyomwagiza Musa, ndivyo alivyowahesabu huko katika bara ya Sinai.
2 Samuel 24.1-24.10 Nombres 26.1-26.2 Nombres 1.2
20 Na wana wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, kichwa kwa kichwa, kila mtu mume tangu umri wa miaka ishirini na zaidi wote walioweza kwenda vitani;
Nombres 26.5-26.7 Nombres 2.10-2.11 Genèse 49.3-49.4 Genèse 29.32 Genèse 46.9
21 wale waliohesabiwa katika kabila ya Reubeni, walikuwa watu arobaini na sita elfu na mia tano (46,500).
Nombres 26.7 Nombres 2.10-2.11
22 Katika wana wa Simeoni, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, wale waliohesabiwa kama hesabu ya majina, kichwa kwa kichwa, kila mume tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Nombres 26.12-26.14 Genèse 29.33 Genèse 49.5-49.6 Genèse 42.24 Genèse 46.10
23 wale waliohesabiwa katika kabila ya Simeoni, walikuwa watu hamsini na kenda elfu na mia tatu (59,300).
Nombres 26.14 Nombres 2.13 Nombres 25.8-25.9 Nombres 25.14
24 Katika wana wa Gadi, kwa kuandama vizazi vyao, jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Nombres 26.15-26.18 Genèse 46.16 Genèse 49.19 Nombres 2.14-2.15 Genèse 30.10-30.11
25 wale waliohesabiwa katika kabila ya Gadi, walikuwa watu arobaini na tano elfu na mia sita na hamsini (45,650).
Nombres 26.18 Nombres 2.15
26 Katika wana wa Yuda, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Genèse 29.35 Nombres 26.19-26.22 2 Samuel 24.9 2 Chroniques 17.14-17.16 Nombres 2.3-2.4
27 wale waliohesabiwa katika kabila ya Yuda, walikuwa watu sabini na nne elfu na mia sita (74,600).
Nombres 26.22 2 Samuel 24.9 Nombres 2.3-2.4 2 Chroniques 17.14-17.16
28 Katika wana wa Isakari, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kwa hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Genèse 30.18 Nombres 2.5-2.6 Nombres 26.23-26.25 Nombres 23.23-23.25 Genèse 46.13
29 wale waliohesabiwa katika kabila ya Isakari, walikuwa watu hamsini na nne elfu na mia nne (54,400).
Nombres 26.25 Nombres 2.6
30 Katika wana wa Zabuloni, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Nombres 26.26-26.27 Nombres 2.7-2.8 Genèse 49.13 Genèse 30.20 Genèse 46.14
31 wale waliohesabiwa katika kabila ya Zabuloni, walikuwa watu hamsini na saba elfu na mia nne (57,400).
Nombres 26.27 Nombres 2.8
32 Katika wana wa Yusufu, maana katika wana wa Efraimu, vizazi vyao kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani,
Nombres 26.35-26.37 Deutéronome 33.17 Genèse 46.20 Genèse 49.22-49.26 Genèse 39.1-39.23
33 wale waliohesabiwa katika kabila ya Efraimu, walikuwa watu arobaini elfu na mia tano (40,500).
Nombres 26.37 Deutéronome 33.17 Nombres 2.19 Genèse 48.5
34 Katika wana wa Manase, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Nombres 26.28-26.34
35 wale waliohesabiwa katika kabila ya Manase, walikuwa watu thelathini na mbili elfu na mia mbili (32,200).
Nombres 26.34 Genèse 48.19-48.20 Nombres 2.21
36 Katika wana wa Benyamini, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Genèse 49.27 Genèse 35.16-35.18 2 Chroniques 17.17 Apocalypse 7.8 Nombres 26.38-26.41
37 wale waliohesabiwa katika kabila ya Benyamini, walikuwa watu thelathini na tano elfu na mia nne (35,400).
Nombres 26.41 2 Chroniques 17.17 Juges 20.44-20.46 Nombres 2.23
38 Katika wana wa Dani, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Genèse 46.23 Nombres 26.42-26.43 Genèse 49.16-49.17 Genèse 30.5-30.6
39 wale waliohesabiwa katika kabila ya Dani, walikuwa watu sitini na mbili elfu na mia saba (62,700).
Nombres 26.43 Nombres 2.26
40 Katika wana wa Asheri, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Genèse 30.12-30.13 Genèse 49.20 Genèse 46.27 Nombres 26.44-26.47
41 wale waliohesabiwa katika kabila ya Asheri, walikuwa watu arobaini na moja elfu na mia tano (41,500).
Nombres 26.47 Nombres 2.28
42 Katika wana wa Naftali, vizazi vyao, kwa kuandama jamaa zao, na nyumba za baba zao, kama hesabu ya majina, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, wote walioweza kwenda vitani;
Genèse 30.7-30.8 Nombres 26.48-26.50 Genèse 46.24 Genèse 49.21
43 wale waliohesabiwa katika kabila ya Naftali, walikuwa watu hamsini na tatu elfu na mia nne (53,400).
Nombres 26.50 Nombres 2.30
44 Hao ndio waliohesabiwa, ambao Musa na Haruni na wale wakuu wa Israeli watu kumi na wawili waliwahesabu; walikuwa kila mmoja kwa ajili ya nyumba ya baba zake.
Nombres 26.64 Nombres 1.2-1.16
45 Basi hao wote waliohesabiwa katika wana wa israeli kwa kuandama nyumba za baba zao tangu umri wa miaka ishirini na zaidi; wote walioweza kwenda vitani katika Israeli;
46 hao wote waliohesabiwa walikuwa ni watu waume mia sita na tatu elfu na mia tano na hamsini (603,550).
Exode 38.26 Exode 12.37 Nombres 26.51 Nombres 2.32 Apocalypse 7.4-7.9

Responsabilités des Lévites

47 Lakini Walawi kwa kuiandama kabila ya baba zao hawakuhesabiwa katika watu hao.
Nombres 2.33 Nombres 3.1-4.49 Nombres 26.57-26.62 1 Chroniques 6.1-6.81 1 Chroniques 21.6
48 Kwa kuwa Bwana alinena na Musa, na kumwambia,
49 Hiyo kabila ya Lawi tu usiihesabu, wala usiitie hesabu yao katika wana wa Israeli;
Nombres 26.62 Nombres 2.33
50 lakini uwaweke Walawi wawe juu ya maskani ya ushahidi, na juu ya vyombo vyake vyote, na juu ya vitu vyake vyote; wao wataichukua hiyo maskani, na vyombo vyake vyote; nao wataitumikia, na kupanga hema zao kwa kuizunguka maskani pande zote.
Exode 38.21 Exode 31.18 Nombres 4.15 Nombres 3.23-3.38 Nombres 4.25-4.33
51 Tena hapo maskani itakapokwenda mbele, Walawi wataishusha; tena hapo maskani itakaposimamishwa, Walawi wataisimamisha; na mgeni atakayekaribia atauawa.
Nombres 3.38 Nombres 3.10 Nombres 18.22 1 Samuel 6.19 2 Samuel 6.7
52 Na wana wa Israeli watazipanga hema zao, kila mtu katika marago yake mwenyewe, kila mtu hapo ilipo beramu yake mwenyewe, kama majeshi yao yalivyo.
Nombres 2.2 Nombres 2.34 Nombres 10.1-10.36 Nombres 24.2
53 Lakini Walawi watapanga hema zao kuizunguka maskani ya ushahidi pande zote, ili zisiwe hasira juu ya mkutano wa wana wa Israeli; kisha Walawi wataulinda ulinzi wa hiyo maskani ya ushahidi.
Nombres 16.46 1 Chroniques 23.32 Lévitique 10.6 Nombres 31.47 Nombres 3.7-3.8
54 Ndivyo walivyofanya wana wa Israeli; kama yote Bwana aliyomwagiza Musa, ndivyo walivyofanya.
Exode 23.21-23.22 Nombres 2.34 Exode 40.32 Exode 39.43 1 Samuel 15.22

Cette Bible est dans le domaine public.