Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Malachie 4.5
Bible en Swahili de l’est


1 Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuru; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema Bwana wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.
2 Pierre 3.7 Abdias 1.18 Malachie 3.2 2 Thessaloniciens 1.8 Esaïe 47.14
2 Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini.
Esaïe 30.26 Luc 1.78 Jean 8.12 Jérémie 33.6 2 Samuel 23.4
3 Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema Bwana wa majeshi.
Job 40.12 Esaïe 26.6 Michée 5.8 Zacharie 10.5 Daniel 7.27
4 Ikumbukeni torati ya Musa, mtumishi wangu, niliyomwamuru huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote, naam, amri na hukumu.
Deutéronome 4.10 Romains 3.31 Luc 10.25-10.28 Matthieu 22.36-22.40 Esaïe 8.20
5 Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya.
Luc 1.17 Marc 9.11-9.13 Matthieu 17.10-17.13 Malachie 3.1 Apocalypse 6.17
6 Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.
Esaïe 11.4 Luc 1.16-1.17 Esaïe 65.15 Hébreux 10.26-10.31 Zacharie 5.3

Cette Bible est dans le domaine public.