Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Zacharie 2.3
Bible en Swahili de l’est


Vision de quatre cornes et quatre forgerons

1 Kisha nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, mtu mwenye kamba ya kupimia mkononi mwake.
Ezéchiel 40.3 Zacharie 1.16 Apocalypse 11.1 Apocalypse 21.15 Ezéchiel 40.5
2 Ndipo nikasema, Unakwenda wapi? Akaniambia, Ninakwenda kuupima Yerusalemu, nione upana wake ulivyo na urefu wake ulivyo.
Apocalypse 21.15-21.17 Jérémie 31.39 Ezéchiel 45.6 Apocalypse 11.1 Ezéchiel 40.3
3 Na tazama, yule malaika aliyesema nami akasimama karibu, na malaika mwingine akatoka ili kuonana naye;
Zacharie 1.19 Zacharie 1.8-1.11 Zacharie 1.13-1.14 Zacharie 4.1 Zacharie 5.5
4 naye akamwambia, Piga mbio, kamwambie kijana huyu, na kusema, Yerusalemu utakaliwa na watu, kama vijiji visivyo na kuta, kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo iliyomo ndani yake.
Zacharie 1.17 Michée 7.11 Esaïe 44.26 Jérémie 31.27 Ezéchiel 38.11

Vision d’un ruban à mesurer

5 Kwa maana mimi, asema Bwana, nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka pande zote, nami nitakuwa huo utukufu ndani yake.
Esaïe 4.5 Zacharie 9.8 Apocalypse 21.23 Esaïe 60.18-60.19 Luc 2.32
6 Haya! Haya! Ikimbieni nchi ya kaskazini, asema Bwana; kwa maana mimi nimewatawanya ninyi kama pepo nne za mbinguni, asema Bwana.
Ezéchiel 17.21 Esaïe 48.20 Ezéchiel 11.16 Zacharie 2.7 Genèse 19.17
7 Haya! Ee Sayuni, jiponye, wewe ukaaye pamoja na binti Babeli.
Esaïe 48.20 Esaïe 52.11 Jérémie 51.6 Jérémie 50.8 Jérémie 51.45
8 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake.
Deutéronome 32.10 Jean 15.21-15.23 Psaumes 17.8 Jean 14.26 Michée 5.6
9 Kwa maana, tazama, nitatikisa mkono wangu juu yao, nao watakuwa mateka ya hao waliowatumikia; nanyi mtajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma.
Esaïe 19.16 Esaïe 14.2 Ezéchiel 39.10 Zacharie 4.9 Esaïe 11.15
10 Imba, ufurahi, Ee binti Sayuni; maana, tazama, ninakuja, nami nitakaa kati yako, asema Bwana.
Zacharie 8.3 Lévitique 26.12 Zacharie 9.9 Sophonie 3.14-3.15 Esaïe 65.18-65.19
11 Na mataifa mengi watajiunga na Bwana katika siku ile, nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yako, nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwako.
Apocalypse 11.15 Luc 2.32 Esaïe 2.2-2.5 Actes 28.28 Psaumes 72.8-72.11
12 Na Bwana atairithi Yuda, iwe sehemu yake katika nchi takatifu, naye atachagua Yerusalemu tena.
Zacharie 1.17 Deutéronome 32.9 Jérémie 10.16 Esaïe 41.9 Jérémie 51.19
13 Nyamazeni, ninyi nyote wenye mwili, mbele za Bwana; kwa maana ameamka, na kutoka katika maskani yake takatifu.
Habakuk 2.20 Psaumes 68.5 Sophonie 1.7 Esaïe 51.9 Psaumes 78.65

Cette Bible est dans le domaine public.