Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Sophonie 1.6
Bible en Swahili de l’est


Jugement imminent de Juda

1 Neno la Bwana lililomjia Sefania, mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia; katika siku za Yosia, mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda.
Jérémie 1.2 2 Chroniques 34.1-34.33 Ezéchiel 1.3 Jérémie 25.3 2 Timothée 3.16
2 Nitavikomesha kabisa vitu vyote, visionekane juu ya uso wa nchi, asema Bwana.
2 Rois 22.16-22.17 Michée 7.13 Genèse 6.7 Esaïe 6.11 Jérémie 6.8-6.9
3 Nitamkomesha mwanadamu na mnyama; nitakomesha ndege wa angani, na samaki wa baharini, na hayo makwazo pamoja na wabaya; nami nitamkatilia mbali mwanadamu, asionekane juu ya uso wa nchi, asema Bwana.
Ezéchiel 7.19 Osée 4.3 Zacharie 13.2 Jérémie 12.4 Jérémie 4.23-4.29
4 Nami nitaunyosha mkono wangu juu ya Yuda, na juu ya watu wote wakaao Yerusalemu; nami nitayakatilia mbali mabaki ya Baali, yasionekane mahali hapa, na hilo jina la Wakemari pamoja na makuhani;
Osée 10.5 2 Rois 23.4-23.5 2 Chroniques 34.4 Exode 15.12 Esaïe 14.26-14.27
5 na wale walisujudiao jeshi la mbinguni juu ya dari za nyumba; na hao waabuduo, waapao kwa Bwana na kuapa pia kwa Malkamu;
1 Rois 11.33 Jérémie 19.13 1 Rois 18.21 2 Rois 23.12 2 Rois 17.41
6 na hao waliorudi nyuma, na kuacha kumfuata Bwana; na hao wasiomtafuta Bwana, wala kumwulizia.
Esaïe 1.4 Jérémie 2.13 Jérémie 2.17 Jérémie 15.6 Esaïe 9.13
7 Nyamaza kimya mbele za Bwana MUNGU; Kwa maana siku ya Bwana i karibu; Kwa kuwa Bwana ameweka tayari dhabihu, Amewatakasa wageni wake.
Jérémie 46.10 Sophonie 1.14 Habakuk 2.20 Esaïe 34.6 1 Samuel 16.5
8 Na itakuwa, katika siku ile ya dhabihu ya Bwana, nitawaadhibu wakuu, na wana wa mfalme, na watu wote waliovaa mavazi ya kigeni.
Esaïe 24.21 Jérémie 39.6-39.7 Jérémie 22.24-22.30 2 Rois 23.30-23.34 Esaïe 3.18-3.24
9 Na katika siku ile nitawaadhibu hao wote warukao juu ya kizingiti, waijazao nyumba ya bwana wao udhalimu na udanganyifu.
1 Samuel 5.5 Proverbes 29.12 2 Rois 5.20-5.27 1 Samuel 2.15-2.16 Néhémie 5.15
10 Na katika siku ile, asema Bwana kutakuwako sauti ya kilio kutoka lango la samaki, na mlio mkuu katika mtaa wa pili, na mshindo mkuu kutoka milimani.
2 Chroniques 33.14 Néhémie 3.3 2 Rois 22.14 Sophonie 1.15 Jérémie 39.2
11 Haya! Lieni, ninyi mkaao katika Makteshi, maana wafanya biashara wote wameangamia; hao wote waliokuwa na mizigo ya fedha wamekatiliwa mbali.
Jacques 5.1 Jérémie 4.8 Jérémie 25.34 Néhémie 3.31-3.32 Joël 1.13
12 Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami nitawaadhibu watu walioganda juu ya sira zao; wasemao katika mioyo yao, Bwana hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.
Jérémie 48.11 Ezéchiel 8.12 Amos 6.1 Ezéchiel 9.9 Malachie 3.14-3.15
13 Na huko utajiri wao utakuwa mateka, na nyumba zao zitakuwa ukiwa; naam, watajenga nyumba, lakini hawatakaa ndani yake; nao watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.
Amos 5.11 Michée 6.15 Deutéronome 28.39 Deutéronome 28.30 Ezéchiel 22.31
14 Hiyo siku ya Bwana iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya Bwana; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko!
Sophonie 1.7 Joël 2.11 Ezéchiel 7.12 Ezéchiel 30.3 Jérémie 30.7
15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,
Joël 2.2 Esaïe 22.5 Amos 5.18-5.20 Romains 2.5 Apocalypse 6.17
16 Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.
Esaïe 2.12-2.15 Osée 5.8 Jérémie 8.16 Osée 8.1 Jérémie 6.1
17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.
Psaumes 83.10 Lamentations 5.16-5.17 Esaïe 59.12-59.15 Michée 3.9-3.12 Michée 7.13
18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha.
Sophonie 3.8 Ezéchiel 7.19 Sophonie 1.2-1.3 Proverbes 11.4 Psaumes 78.58

Cette Bible est dans le domaine public.