Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jonas 1.10
Bible en Swahili de l’est


Mission et fuite de Jonas

1 Basi neno la Bwana lilimjia Yona, mwana wa Amitai, kusema,
Luc 11.32 2 Rois 14.25 Luc 11.29-11.30 Matthieu 12.39-12.41 Matthieu 16.4
2 Ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa, ukapige kelele juu yake; kwa maana uovu wao umepanda juu mbele zangu.
Genèse 10.11 Nahum 1.1 Esaïe 58.1 Sophonie 2.13-2.15 Jonas 4.11
3 Lakini Yona akaondoka akimbilie Tarshishi, apate kujiepusha na uso wa Bwana; akatelemka hata Yafa, akaona merikebu inayokwenda Tarshishi; basi, akatoa nauli, akapanda merikebuni, aende pamoja nao Tarshishi, ajiepushe na uso wa Bwana.
Josué 19.46 Genèse 4.16 Actes 9.36 Esaïe 23.1 Esaïe 23.10
4 Lakini Bwana alituma upepo mkuu baharini, ikawa tufani kubwa baharini, hata merikebu ikawa karibu na kuvunjika.
Psaumes 107.23-107.31 Matthieu 8.24-8.27 Psaumes 135.7 Amos 4.13 Actes 27.13-27.20
5 Basi wale mabaharia wakaogopa, kila mtu akamwomba mungu wake; nao wakatupa baharini shehena iliyokuwa merikebuni, ili kuupunguza uzito wake. Lakini Yona alikuwa ameshuka hata pande za ndani za merikebu; akajilaza, akapata usingizi.
Actes 27.18-27.19 Actes 27.38 1 Rois 18.26 Esaïe 45.20 Jonas 1.14
6 Basi nahodha akamwendea, akamwambia, Una nini, Ewe ulalaye usingizi? Amka, ukamwombe Mungu wako; labda Mungu huyo atatukumbuka, tusipotee.
Jonas 3.9 Amos 5.15 2 Samuel 12.22 Esaïe 3.15 Joël 2.11
7 Wakasemezana kila mtu na mwenzake, Haya, na mpige kura, mpate kujua mabaya haya yametupata kwa sababu ya nani. Basi wakapiga kura, nayo kura ikamwangukia Yona.
Proverbes 16.33 Josué 7.10 1 Samuel 10.20-10.21 Josué 7.13-7.18 Nombres 32.23
8 Ndipo wakamwambia, Tafadhali utuambie, wewe ambaye mabaya haya yametupata kwa sababu yako; kazi yako ni kazi gani? Nawe umetoka wapi? Nchi yako ni nchi ipi? Nawe u mtu wa kabila gani?
1 Samuel 30.13 Genèse 47.3 1 Samuel 14.43 Josué 7.19 Jacques 5.16
9 Akawaambia, Mimi ni Mwebrania; nami namcha Bwana, Mungu wa mbingu, aliyeziumba bahari na nchi kavu.
Esdras 1.2 Psaumes 136.26 Néhémie 9.6 2 Rois 17.25 Genèse 14.13
10 Ndipo watu wale wakaogopa mno, wakamwambia, Ni jambo gani hili ulilolitenda! Kwa maana watu wale walijua ya kuwa amekimbia, ajiepushe na uso wa Bwana, kwa sababu alikuwa amewajulisha.
Jonas 1.3 Job 27.22 Josué 7.25 Jean 19.8 Daniel 5.6-5.9
11 Basi wakamwambia, Tukutende nini, ili bahari itulie? Kwa maana bahari ilikuwa inazidi kuchafuka.
2 Samuel 21.1-21.6 2 Samuel 24.11-24.13 1 Samuel 6.2-6.3 Michée 6.6-6.7
12 Naye akawaambia, Nikamateni, mnitupe baharini; basi bahari itatulia; kwa maana najua ya kuwa ni kwa ajili yangu tufani hii imewapata.
2 Samuel 24.17 1 Chroniques 21.17 Josué 7.20-7.21 Ecclésiaste 9.18 Jean 11.50
13 Lakini wale watu wakavuta makasia kwa nguvu, ili wapate kurudi pwani, wasiweze; kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia sana.
Proverbes 21.30 Job 34.29
14 Basi wakamlilia Bwana, wakasema, Twakuomba, Ee Bwana, twakuomba, tusiangamie kwa ajili ya uhai wa mtu huyu, wala usitupatilize kwa ajili ya damu isiyo na hatia; kwa maana wewe, Bwana, umefanya kama ulivyopenda.
Psaumes 115.3 Deutéronome 21.8 Psaumes 135.6 Daniel 4.34-4.35 Jonas 1.16
15 Basi wakamkamata Yona, wakamtupa baharini, nayo bahari ikaacha kuchafuka.
Psaumes 107.29 Luc 8.24 Psaumes 93.3-93.4 Psaumes 65.7 Matthieu 8.26
16 Ndipo wale watu wakamwogopa Bwana mno, wakamtolea Bwana sadaka, na kuweka nadhiri.
Psaumes 107.22 Genèse 8.20 Psaumes 50.14 Esaïe 60.5-60.7 Genèse 28.20
17 Bwana akaweka tayari samaki mkubwa ili ammeze Yona, naye Yona akawa ndani ya tumbo la samaki yule muda wa siku tatu, mchana na usiku.
Matthieu 12.40 Matthieu 16.4 Luc 11.30 Habakuk 3.2 Genèse 1.21

Cette Bible est dans le domaine public.