Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 12.13
Bible en Swahili de l’est


Israël et son ancêtre Jacob

1 Efraimu hujilisha upepo, na kuandamana na upepo wa mashariki; haachi kuongeza uongo na uharibifu; nao wafanya agano na Ashuru, na mafuta huchukuliwa kwenda Misri.
Osée 5.13 Jérémie 22.22 Osée 11.12 Osée 8.7 Esaïe 30.6-30.7
2 Bwana naye ana mateto na Yuda, naye atamwadhibu Yakobo kwa kadiri ya njia zake; kwa kadiri ya matendo yake atamlipa.
Michée 6.2 Osée 4.1 Ezéchiel 23.31-23.32 Jérémie 3.8-3.11 Osée 8.13
3 Tumboni alimshika ndugu yake kisigino; Na alipokuwa mtu mzima alikuwa na uwezo kwa Mungu;
Genèse 25.26 Genèse 32.24-32.28 Romains 9.11 Jacques 5.16-5.18
4 Naam, alikuwa na uwezo juu ya malaika Akashinda; alilia, na kumsihi; Alimwona huko Betheli, naye akasema nasi huko;
Genèse 35.15 Exode 3.2-3.5 Hébreux 5.7 Genèse 32.29 Genèse 48.15
5 Naam, Bwana, Mungu wa majeshi; Bwana ndilo kumbukumbu lake.
Exode 3.15 Psaumes 135.13 Genèse 28.16 Esaïe 42.8 Genèse 32.30
6 Basi, mrudie Mungu wako; shika fadhili na hukumu; ukamngojee Mungu wako daima.
Michée 6.8 Joël 2.13 Osée 14.1 Osée 6.1-6.3 Zacharie 7.9
7 Ni mchuuzi, mizani ya udanganyifu i mkononi mwake; anapenda kudhulumu.
Proverbes 11.1 Zacharie 14.21 Michée 3.1-3.3 Ezéchiel 22.29 Malachie 3.5
8 Naye Efraimu alisema, Kweli nimekuwa tajiri, nimejipatia mali nyingi; katika kazi zangu zote hawataona kwangu uovu wo wote uliokuwa dhambi.
Apocalypse 3.17 Psaumes 62.10 Zacharie 11.5 1 Timothée 6.5 Deutéronome 8.17
9 Lakini mimi ni Bwana, Mungu wako tangu ulipotoka katika nchi ya Misri; nitakukalisha tena katika hema, kama siku za karamu ya idi.
Lévitique 23.40-23.43 Néhémie 8.15-8.17 Osée 13.4 Michée 6.4 Hébreux 11.9-11.13
10 Tena nimenena na hao manabii, nami nimeongeza maono, na kwa utumishi wa manabii nimetumia mifano.
2 Rois 17.13 Ezéchiel 20.49 Joël 2.28 Néhémie 9.30 2 Corinthiens 12.7
11 Je! Gileadi ni uovu? Wamekuwa ubatili tu; huko Gilgali hutoa dhabihu za ng’ombe; naam, madhabahu zao zimekuwa kama chungu katika matuta ya mashamba.
Osée 4.15 Osée 8.11 Osée 6.8 Osée 9.15 Osée 10.1
12 Na Yakobo alikimbia mpaka Padan-Aramu, Na Israeli alitumika apate mke; Ili apate mke alichunga kondoo.
Genèse 27.43 Genèse 29.18-29.28 Genèse 32.27-32.28 Deutéronome 26.5 Genèse 31.41
13 Na kwa nabii Bwana alimtoa Israeli katika Misri, Na kwa mkono wa nabii alihifadhiwa.
Exode 12.50-12.51 Actes 3.22-3.23 Psaumes 77.20 Exode 13.3 Esaïe 63.11-63.14
14 Efraimu amenitia hasira kali sana; kwa sababu hiyo damu yake itaachwa juu yake, na Bwana wake atamrudishia lawama yake.
Daniel 11.18 Ezéchiel 18.13 2 Rois 17.7-17.18 Deutéronome 28.37 1 Rois 2.33-2.34

Cette Bible est dans le domaine public.