Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lamentations 1.18
Bible en Swahili de l’est


Le malheur de Jérusalem

1 Jinsi mji huu ukaavyo ukiwa, Huo uliokuwa umejaa watu! Jinsi alivyokuwa kama mjane, Yeye aliyekuwa mkuu kati ya mataifa! Binti mfalme kati ya majimbo, Jinsi alivyoshikwa shokoa!
1 Rois 4.21 Esdras 4.20 Esaïe 3.26 2 Rois 23.35 Esaïe 22.2
2 Hulia sana wakati wa usiku, Na machozi yake yapo mashavuni; Miongoni mwa wote waliompenda Hakuna hata mmoja amfarijiye; Rafiki zake wote wamemtenda hila, Wamekuwa adui zake.
Psaumes 6.6 Michée 7.5 Lamentations 1.19 Psaumes 77.2-77.6 Psaumes 31.11
3 Yuda amehamishwa kwa sababu ya kuonewa, Na kwa sababu ya utumwa mkuu; Anakaa kati ya makafiri, Haoni raha iwayo yote; Wote waliomfuata wamempata Katika dhiki yake.
Deutéronome 28.64-28.67 Lamentations 2.9 2 Rois 25.11 Jérémie 39.9 Jérémie 13.19
4 Njia za Sayuni zaomboleza, Kwa kuwa hakuna ajaye kwa sikukuu; Malango yake yote yamekuwa ukiwa, Makuhani wake hupiga kite; Wanawali wake wanahuzunika; Na yeye mwenyewe huona uchungu.
Joël 1.8-1.13 Jérémie 9.11 Jérémie 14.2 Lamentations 2.6-2.7 Esaïe 24.4-24.6
5 Watesi wake wamekuwa kichwa, Adui zake hufanikiwa; Kwa kuwa Bwana amemtesa Kwa sababu ya wingi wa makosa yake; Watoto wake wadogo wamechukuliwa mateka Mbele yake huyo mtesi.
Jérémie 39.9 Ezéchiel 8.17-8.18 Ezéchiel 9.9 Jérémie 30.14-30.15 Psaumes 90.7-90.8
6 Naye huyo binti Sayuni Enzi yake yote imemwacha; Wakuu wake wamekuwa kama ayala Wasioona malisho; Nao wamekwenda zao hawana nguvu Mbele yake anayewafuatia.
Ezéchiel 24.25 2 Rois 19.21 Jérémie 52.7-52.8 Jérémie 29.4 Lévitique 26.36-26.37
7 Siku za mateso na misiba yake, Yerusalemu huyakumbuka matamaniko yake yote Yaliyokuwa tangu siku za kale; Hapo watu wake walipoanguka mikononi mwa mtesi, Wala hakuna hata mmoja wa kumsaidia; Hao watesi wake walimwona, Wakafanya sabato zake kuwa mzaha.
Psaumes 77.5-77.9 Psaumes 79.4 Psaumes 42.4 Psaumes 147.19-147.20 Deutéronome 4.7-4.8
8 Yerusalemu amefanya dhambi sana; Kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote waliomheshimu wanamdharau, Kwa sababu wameuona uchi wake; Naam, yeye anaugua, Na kujigeuza aende nyuma.
Lamentations 1.20-1.22 Esaïe 59.2-59.13 Lamentations 1.4-1.5 Jérémie 13.22 Jérémie 13.26
9 Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, Bwana, teso langu; Maana huyo adui amejitukuza.
Deutéronome 32.29 Esaïe 47.7 Lamentations 1.17 Psaumes 25.18 Ecclésiaste 4.1
10 Huyo mtesi amenyosha mkono wake Juu ya matamaniko yake yote; Maana ameona ya kuwa makafiri wameingia Ndani ya patakatifu pake; Ambao kwa habari zao wewe uliamuru Wasiingie katika kusanyiko lako.
Deutéronome 23.3 Jérémie 51.51 Néhémie 13.1 Psaumes 74.4-74.8 Lamentations 1.7
11 Watu wake wote hupiga kite, Wanatafuta chakula; Wameyatoa matamaniko yao wapate chakula Cha kuihuisha nafsi; Ee Bwana, tazama, uangalie; Kwa maana mimi nimekuwa mnyonge.
Jérémie 52.6 Jérémie 38.9 Lamentations 2.12 1 Samuel 30.11-30.12 Lamentations 1.9
12 Je! Si kitu kwenu, enyi nyote mpitao njia, Angalieni, mtazame Kama kuna majonzi yo yote mfano wa majonzi yangu, Niliyotendwa mimi, Ambayo Bwana amenihuzunisha kwa hayo Siku ya hasira yake iwakayo.
Luc 23.28-23.31 Daniel 9.12 Matthieu 24.21 Esaïe 13.13 Jérémie 30.24
13 Toka juu amepeleka moto mifupani mwangu, Nao umeishinda; Ametandika wavu aninase miguu, Amenirudisha nyuma; Amenifanya kuwa mtu wa pekee, Na mgonjwa mchana kutwa.
Habakuk 3.16 Job 30.30 Psaumes 22.14 Ezéchiel 17.20 Job 19.6
14 Kongwa la makosa yangu limefungwa na mkono wake; Hayo yameshikamana; Yamepanda juu shingoni mwangu; Amezikomesha nguvu zangu;
Esaïe 47.6 Deutéronome 28.48 Jérémie 28.14 Ezéchiel 25.7 Ezéchiel 25.4
15 Bwana amenitia mikononi mwao, Ambao siwezi kupingamana nao. Bwana amewafanya mashujaa wangu wote Kuwa si kitu kati yangu; Ameita mkutano mkuu kinyume changu Ili kuwaponda vijana wangu; Bwana amemkanyaga kama shinikizoni Huyo bikira binti Yuda.
Esaïe 28.18 Esaïe 63.3 Malachie 4.3 Deutéronome 28.33 Luc 21.24
16 Mimi ninayalilia mambo hayo; Jicho langu, jicho langu linachuruzika maji; Kwa kuwa mfariji yu mbali nami, Ambaye ilimpasa kunihuisha nafsi; Watoto wangu wameachwa peke yao, Kwa sababu huyo adui ameshinda.
Lamentations 1.2 Lamentations 2.18 Jérémie 13.17 Lamentations 3.48-3.49 Jérémie 14.17
17 Sayuni huinyosha mikono yake; Hakuna hata mmoja wa kumfariji; Bwana ametoa amri juu ya Yakobo, Kwamba wamzungukao wawe watesi wake; Yerusalemu amekuwa kati yao Kama kitu kichafu.
Jérémie 4.31 Lamentations 1.9 Esaïe 1.15 2 Rois 24.2-24.4 Lamentations 1.16
18 Bwana ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka.
1 Samuel 12.14-12.15 Lamentations 1.12 Jérémie 12.1 Psaumes 119.75 Jérémie 49.12
19 Naliwaita hao walionipenda Lakini walinidanganya; Makuhani wangu na wazee wangu Walifariki mjini; Hapo walipokuwa wakitafuta chakula ili kuzihuisha nafsi zao.
Lamentations 1.2 Lamentations 2.20 Lamentations 1.11 Job 19.13-19.19 Lamentations 4.7-4.9
20 Angalia, Ee Bwana; maana mimi ni katika dhiki; Mtima wangu umetaabika; Moyo wangu umegeuka ndani yangu; Maana nimeasi vibaya sana; Huko nje upanga hufisha watu; Nyumbani mna kama mauti.
Lamentations 2.11 Deutéronome 32.25 Esaïe 16.11 Ezéchiel 7.15 Job 30.27
21 Wamesikia kwamba napiga kite; Hakuna hata mmoja wa kunifariji; Adui zangu wote wamesikia habari ya mashaka yaliyonipata; Hufurahi kwa kuwa umeyafanya hayo; Utaileta siku ile uliyoitangaza, Nao watakuwa kama mimi.
Lamentations 1.8 Lamentations 1.16 Jérémie 50.11 Lamentations 2.15 Lamentations 1.22
22 Huo uovu wao wote Na uje mbele zako wewe; Ukawatende wao kama ulivyonitenda mimi Kwa dhambi zangu zote; Kwa maana mauguzi yangu ni mengi sana, Na moyo wangu umezimia.
Psaumes 109.14-109.15 Néhémie 4.4-4.5 Jérémie 8.18 Jérémie 10.25 Luc 23.31

Cette Bible est dans le domaine public.