Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 53.8
Bible en Swahili de l’est


1 Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?
Jean 12.38 Esaïe 51.9 Romains 10.16-10.17 Ephésiens 1.18-1.19 Romains 1.16-1.18
2 Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.
Esaïe 52.14 Esaïe 11.1 Philippiens 2.6-2.7 Marc 6.3 1 Pierre 2.14
3 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.
Esaïe 49.7 Jean 1.10-1.11 Esaïe 53.10 Marc 14.34 Zacharie 11.8
4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
1 Pierre 2.24 Matthieu 8.17 Galates 3.13 1 Jean 2.2 Esaïe 53.5-53.6
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
1 Pierre 2.24-2.25 1 Pierre 3.18 Romains 5.6-5.10 Matthieu 20.28 Romains 4.25
6 Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.
1 Pierre 2.25 1 Pierre 3.18 Psaumes 119.176 Romains 4.25 Romains 3.10-3.19
7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.
Actes 8.32-8.33 Matthieu 26.63 Marc 14.61 1 Pierre 2.23 Jean 19.9
8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
Actes 8.33 Daniel 9.26 Jean 11.49-11.52 Matthieu 1.1 Esaïe 53.12
9 Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
Matthieu 27.57-27.60 1 Pierre 2.22 Hébreux 4.15 1 Jean 3.5 Marc 15.43-15.46
10 Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake;
Esaïe 53.3-53.6 Esaïe 9.7 Hébreux 13.10-13.12 Matthieu 17.5 Zacharie 13.7
11 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.
Romains 5.18-5.19 Esaïe 53.12 1 Jean 2.1 Jean 16.21 Esaïe 53.4-53.6
12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, Na kuwaombea wakosaji.
Luc 22.37 Marc 15.27 Psaumes 2.8 Colossiens 2.15 Esaïe 53.6

Cette Bible est dans le domaine public.