Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 3.14
Bible en Swahili de l’est


Jugement des habitants de Jérusalem

1 Kwa maana, tazama, Bwana, Bwana wa majeshi, awaondolea Yerusalemu na Yuda egemeo na tegemeo; tegemeo lote la chakula na tegemeo lote la maji;
Lévitique 26.26 Esaïe 1.24 Psaumes 105.16 Ezéchiel 4.16-4.17 Ezéchiel 14.13
2 mtu hodari na mtu wa vita; mwamuzi na nabii; mpiga ramli na mzee;
Ezéchiel 17.13 Esaïe 2.13-2.15 Lamentations 5.12-5.14 Ezéchiel 9.5 Esaïe 9.14-9.15
3 jemadari aliye juu ya watu hamsini, na mtu mstahifu, na mshauri, na fundi aliye mstadi, na mganga ajuaye uganga sana.
Exode 18.21 Juges 8.18 Exode 4.14-4.16 1 Samuel 8.12 Deutéronome 1.15
4 Nami nitawapa watoto kuwamiliki, na watoto wachanga kuwatawala.
Ecclésiaste 10.16 2 Chroniques 36.2 2 Chroniques 33.1 2 Chroniques 36.9 2 Chroniques 34.1
5 Nao watu wataonewa, kila mtu na mwenziwe, na kila mtu na jirani yake; mtoto atajivuna mbele ya mzee, na mtu mnyonge mbele ya mtu mwenye heshima.
Jérémie 9.3-9.8 Ezéchiel 22.6-22.7 Lévitique 19.32 Luc 22.64 Jacques 5.4
6 Mtu atakapomshika ndugu yake ndani ya nyumba ya baba yake, akisema, Wewe una nguo, ututawale wewe; na mahali hapa palipobomoka pawe chini ya mkono wako;
Esaïe 4.1 Juges 11.6-11.8 Jean 6.15
7 basi, siku ile atainua sauti yake, akisema, Mimi sitakuwa mponya watu; kwa maana ndani ya nyumba yangu hamna chakula wala mavazi; wala hamtanifanya kuwa mtawala juu ya watu hawa.
Osée 5.13 Apocalypse 10.5-10.6 Jérémie 14.19 Genèse 14.22 Lamentations 2.13
8 Kwa maana Yerusalemu umebomolewa na Yuda wameanguka, kwa sababu ulimi wao na matendo yao ni kinyume cha Bwana, hata wayachukize macho ya utukufu wake.
Esaïe 5.18-5.19 Psaumes 73.8-73.11 Matthieu 12.36-12.37 Michée 3.12 Ezéchiel 8.4-8.6
9 Kuonekana kwa nyuso zao kwashuhudia juu yao, wafunua dhambi yao kama Sodoma, hawaifichi. Ole wa nafsi zao, kwa maana wamejilipa nafsi zao uovu.
Genèse 13.13 Romains 6.23 Ezéchiel 23.16 Genèse 19.5-19.9 Jérémie 44.16-44.17
10 Waambieni wenye haki ya kuwa watakuwa heri, kwa maana watakula matunda ya matendo yao
Deutéronome 28.1-28.14 Ecclésiaste 8.12 Psaumes 18.23-18.24 Psaumes 128.1-128.2 Ezéchiel 18.9-18.19
11 Ole wake mtu mbaya; shari itakuwa kwake, kwa maana atapewa ijara ya mikono yake.
Deutéronome 28.15-28.68 Psaumes 1.3-1.5 Esaïe 48.22 Esaïe 65.13-65.15 Ecclésiaste 8.13
12 Katika habari za watu wangu, watoto ndio wanaowaonea, na wanawake ndio wanaowatawala. Enyi watu wangu, wakuongozao wakukosesha, waiharibu njia ya mapito yako.
Esaïe 3.4 Matthieu 23.13 Esaïe 28.14-28.15 2 Rois 11.1 Esaïe 9.15-9.16
13 Bwana asimama ili atete, asimama ili awahukumu watu.
Michée 6.2 Osée 4.1-4.2 Proverbes 23.10-23.11 Psaumes 12.5 Proverbes 22.22-22.23
14 Bwana ataingia katika kuwahukumu wazee wa watu wake na wakuu wao; Ninyi ndinyi mliokula shamba la mizabibu; vitu mlivyowateka maskini vi ndani ya nyumba zenu.
Job 22.4 Psaumes 143.2 Jérémie 5.27 Job 24.9 Job 34.23
15 Ni nini maana yake, ninyi kuwaonea watu wangu, na kuseta nyuso za maskini? Asema Bwana, Bwana wa majeshi.
Psaumes 94.5 Amos 8.4-8.6 Amos 2.6-2.7 Exode 5.14 Ezéchiel 18.2
16 Bwana akasema tena, Kwa sababu binti za Sayuni wana kiburi, na kuenenda na shingo zilizonyoshwa, na macho ya kutamani, wakienenda kwa hatua za madaha, na kuliza njuga kwa miguu yao;
Esaïe 4.4 Esaïe 32.9-32.11 Matthieu 21.5 Cantique 3.11 Ezéchiel 16.49-16.50
17 Basi, kwa hiyo, Bwana atawapiga binti za Sayuni kwa pele za utosini, na Bwana ataifunua aibu yao.
Jérémie 13.22 Deutéronome 28.27 Esaïe 20.4 Ezéchiel 23.25-23.29 Ezéchiel 16.36-16.37
18 Siku hiyo Bwana atawaondolea uzuri wa njuga zao, na kaya zao;
Juges 8.21 Juges 8.26
19 na pete za masikio, na vikuku, na taji zao;
Nombres 31.50 Genèse 24.22 Genèse 24.30 Genèse 38.25 Genèse 38.18
20 na dusumali, na mafurungu, na vitambi, na vibweta vya marashi, na matalasimu;
Exode 39.28 Ezéchiel 16.12 Exode 32.2 Osée 2.13 Genèse 35.4
21 na pete, na azama,
Genèse 24.47 1 Timothée 2.9-2.10 1 Pierre 3.3-3.4 Esther 8.12 Jacques 2.2
22 na mavazi ya sikukuu, na debwani; na shali, na vifuko;
23 na vioo vidogo, na kitani nzuri, na vilemba, na utaji.
1 Chroniques 15.27 Genèse 24.65 Apocalypse 19.14 Ezéchiel 16.10 Cantique 5.7
24 Hata itakuwa ya kuwa badala ya manukato mazuri kutakuwa uvundo, na badala ya mishipi, kamba; na badala ya nywele zilizosukwa vizuri, upaa; na badala ya kisibau, mavazi ya kigunia; na kutiwa alama mwilini kwa moto badala ya uzuri.
Ezéchiel 27.31 Lamentations 2.10 Esaïe 22.12 Esaïe 15.3 Amos 8.10
25 Watu wako waume wataanguka kwa upanga, na mashujaa wako vitani.
Jérémie 21.9 Amos 9.10 2 Chroniques 29.9 Jérémie 18.21 Esaïe 1.20
26 Na malango yake yatalia na kuomboleza, naye atakuwa ukiwa, atakaa chini.
Lamentations 2.10 Jérémie 14.2 Lamentations 1.4 Job 2.13 Job 2.8

Cette Bible est dans le domaine public.