Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 10.20
Bible en Swahili de l’est


1 Ole wao wawekao amri zisizo za haki, na waandishi waandikao maneno ya ushupavu;
Luc 11.52 Habakuk 2.6 Michée 3.1-3.4 Esaïe 5.8 Psaumes 94.20-94.21
2 ili kumpotosha mhitaji asipate haki yake, na kuwanyang’anya maskini wa watu wangu haki yao; ili wajane wawe mateka yao, na kuwafanya yatima waliofiwa na baba zao kuwa mawindo yao!
Malachie 3.5 Esaïe 3.14 Ezéchiel 22.7 Esaïe 5.23 Esaïe 1.23
3 Nanyi mtafanya nini siku ya kujiliwa, na wakati wa uangamivu, utakaokuja kutoka mbali sana? Je! Mtamkimbilia nani mpate msaada? Na utukufu wenu mtauacha wapi?
Osée 9.7 Luc 19.44 Esaïe 20.6 Job 31.14 Esaïe 5.26
4 Watainama chini ya wafungwa tu, wataanguka chini yao waliouawa. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa.
Esaïe 5.25 Esaïe 9.12 Esaïe 24.22 Deutéronome 31.15-31.18 Esaïe 34.3

Jugement de l’Assyrie

5 Ole wake Ashuru! Fimbo ya hasira yangu, ambaye gongo lililo mkononi mwake ni ghadhabu yangu!
Esaïe 66.14 Esaïe 14.25 Jérémie 51.20-51.24 Sophonie 2.13 Esaïe 30.30
6 Nitamtuma juu ya taifa lenye kukufuru, nitampa maagizo juu ya watu wa ghadhabu yangu, ateke nyara, na kuchukua mateka, na kuwakanyaga kama matope ya njiani.
Esaïe 9.17 Esaïe 41.25 Jérémie 34.22 Esaïe 29.13 Esaïe 33.14
7 Lakini hivyo sivyo akusudiavyo mwenyewe, wala sivyo moyo wake uwazavyo; maana katika moyo wake akusudia kuharibu, na kukatilia mbali mataifa, wala si mataifa machache.
Genèse 50.20 Michée 4.11-4.12 Actes 2.23 Esaïe 37.11-37.13 Actes 13.27-13.30
8 Maana asema, Je! Wakuu wangu si wote wafalme?
2 Rois 18.24 Daniel 2.37 Esaïe 36.8 Ezéchiel 26.7 2 Rois 19.10
9 Je! Kalno si kama Karkemishi? Hamathi si kama Arpadi? Samaria si kama Dameski?
2 Rois 16.9 2 Chroniques 35.20 Jérémie 46.2 Genèse 10.10 2 Rois 17.5-17.6
10 Kama vile mkono wangu ulivyofikilia falme za sanamu, ambazo sanamu zao za kuchongwa zilikuwa bora kuliko sanamu za Yerusalemu na za Samaria;
Esaïe 10.14 2 Rois 19.12-19.13 2 Chroniques 32.12-32.16 2 Chroniques 32.19 2 Rois 18.33-18.35
11 je! Sitautenda Yerusalemu na sanamu zake vile vile kama nilivyoutenda Samaria na sanamu zake?
Esaïe 36.19-36.20 Esaïe 2.8 Esaïe 37.10-37.13
12 Basi, itakuwa, Bwana atakapokuwa ameitimiza kazi yake yote juu ya mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitayaadhibu matunda ya kiburi cha moyo wake mfalme wa Ashuru, na majivuno ya macho yake.
Jérémie 50.18 2 Rois 19.31 Esaïe 28.21-28.22 Esaïe 37.36-37.38 Psaumes 18.27
13 Kwa maana amesema, Kwa nguvu za mkono wangu nimetenda jambo hili, na kwa hekima yangu; maana mimi nina busara; nami nimeiondoa mipaka ya watu, nikaziteka akiba zao, nikawaangusha waketio juu ya viti vya enzi kama afanyavyo shujaa.
Daniel 4.30 2 Rois 17.24 2 Rois 18.32 Amos 6.13 Amos 5.27-6.2
14 Na mkono wangu umezitoa mali za mataifa kama katika kioto cha ndege; na kama vile watu wakusanyavyo mayai yaliyoachwa, ndivyo nilivyokusanya dunia yote; wala hapana aliyetikisa bawa, wala kufumbua kinywa, wala kulia.
Job 31.25 Jérémie 49.16 Nahum 2.9-3.1 Proverbes 18.12 Esaïe 5.8
15 Je! Shoka lijisifu juu yake alitumiaye? Je! Msumeno ujitukuze juu yake auvutaye? Ingekuwa kana kwamba bakora ingewatikisa waiinuao, au fimbo ingemwinua yeye ambaye si mti.
Esaïe 10.5 Romains 9.20-9.21 Esaïe 45.9 Jérémie 51.20-51.23 Esaïe 29.16
16 Kwa hiyo Bwana, Bwana wa majeshi, atawapelekea kukonda watu wake walionona; na badala ya utukufu wake kutawashwa kuteketea kama kuteketea kwa moto.
Psaumes 106.15 Esaïe 33.10-33.14 Esaïe 37.29 Esaïe 29.5-29.8 Esaïe 30.30-30.33
17 Na mwanga wa Israeli utakuwa ni moto, na Mtakatifu wake atakuwa mwali wa moto; nao utateketeza na kula mbigili zake na miiba yake katika siku moja.
Esaïe 27.4 Nombres 11.1-11.3 Jérémie 7.20 Jérémie 4.4 Esaïe 37.23
18 Naye atauteketeza utukufu wa msitu wake, na wa shamba lake linalositawi, tangu nafsi hata nyama ya mwili, itakuwa kama vile afapo mtu aliye mgonjwa.
Esaïe 10.33-10.34 2 Rois 19.23 Esaïe 9.18 2 Rois 19.28 Ezéchiel 20.47-20.48
19 Na miti ya msitu wake itakayosalia itakuwa michache, hata mtoto ataweza kuihesabu.
Esaïe 21.17 Esaïe 37.36
20 Tena itakuwa katika siku hiyo mabaki ya Israeli, na hao waliopona wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, bali watamtegemea Bwana, Mtakatifu wa Israeli, kwa kweli.
2 Rois 16.7 2 Chroniques 28.20 Esaïe 50.10 Esaïe 1.9 Esaïe 37.31-37.32
21 Mabaki, nao ni mabaki ya Yakobo, watamrudia Mungu, aliye mwenye nguvu.
Esaïe 9.6 2 Corinthiens 3.14-3.16 Osée 7.10 Esaïe 7.3 Esaïe 9.13
22 Maana watu wako, Ee Israeli, wajapokuwa wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki tu watakaorudi; kuangamiza kumekusudiwa, kunakofurika kwa haki.
Romains 9.27-9.28 Esaïe 6.13 Apocalypse 20.8 Romains 11.5-11.6 Daniel 9.27
23 Kwa maana Bwana, Bwana wa majeshi, atayatimiza maangamizo yaliyokusudiwa katika nchi yote.
Esaïe 14.26-14.27 Esaïe 28.22 Romains 9.28 Daniel 4.35 Esaïe 24.1-24.23
24 Kwa hiyo Bwana, Bwana wa majeshi, asema hivi, Enyi watu wangu mkaao katika Sayuni, msiogope Ashuru, ingawa akupiga kwa fimbo, na kuliinua gongo lake juu yako, kwa namna ya Kimisri.
Esaïe 37.6 Esaïe 61.3 Exode 14.21-14.31 Esaïe 46.13 Exode 5.14
25 Maana bado kitambo kidogo tu ghadhabu itakoma, na hasira yangu itageukia kuwaangamiza.
Daniel 11.36 Esaïe 54.7 Psaumes 37.10 Hébreux 10.37 Esaïe 30.30-30.33
26 Na Bwana wa majeshi ataamsha mjeledi juu yake, kama vile alivyopiga Midiani karibu na jabali la Orebu; na fimbo yake itakuwa juu ya bahari, naye ataiinua kwa namna ya Kimisri.
Esaïe 9.4 Juges 7.25 2 Rois 19.35 Esaïe 37.36-37.38 Esaïe 10.16-10.19
27 Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako, na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa, kwa sababu ya kutiwa mafuta.
Esaïe 9.4 Psaumes 105.15 Esaïe 14.25 Luc 4.18 1 Jean 2.27
28 Amefika Ayathi; amepita kati ya Migroni; ameweka mizigo yake huko Mikmashi;
1 Samuel 14.2 1 Samuel 13.2 1 Samuel 13.5 Néhémie 11.31 1 Samuel 14.31
29 wamevuka kivuko; wamekwenda kulala katika Geba; Rama unatetemeka; Gibea wa Sauli umekimbia.
1 Samuel 7.17 1 Samuel 13.23 1 Samuel 11.4 Josué 21.17 1 Rois 15.23
30 Piga kelele sana, Ee binti Galimu; sikiliza, Ee Laisha; ole wako, maskini Anathothi!
1 Samuel 25.44 Jérémie 1.1 Josué 21.18 Juges 18.29 Juges 18.7
31 Madmena ni mkimbizi; wenyeji wa Gebimu wamejikusanya wakimbie;
Josué 15.31
32 siku hii ya leo atasimama huko Nobu; anatikisa mkono wake juu ya mlima wa binti Sayuni, mlima wa Yerusalemu.
1 Samuel 21.1 1 Samuel 22.19 Zacharie 2.9 Esaïe 19.16 Esaïe 37.22
33 Angalia, Bwana, Bwana wa majeshi, atayakata matawi kwa nguvu za kutisha; nao walio warefu wa kimo watakatwa; na hao walioinuka wataangushwa chini;
Amos 2.9 Esaïe 37.38 Esaïe 2.11-2.17 Daniel 4.37 2 Chroniques 32.21
34 naye atavikata vichaka vya msitu kwa chuma; na Lebanoni utaanguka kwa mkono wake aliye mwenye uweza.
Esaïe 37.24 Jérémie 48.2 Esaïe 31.8 Esaïe 37.36 Jérémie 46.22-46.23

Cette Bible est dans le domaine public.