Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 1.23
Bible en Swahili de l’est


Prophéties sur Israël

Péchés de Juda et punition

1 Haya ni maono ya Isaya, mwana wa Amozi, aliyoyaona katika habari za Yuda na Yerusalemu, siku za Uzia na Yothamu na Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.
Esaïe 2.1 2 Rois 18.1-20.21 Esaïe 7.1 Psaumes 89.19 Nombres 24.16
2 Sikieni, enyi mbingu, tega sikio, Ee nchi, kwa maana Bwana amenena; Nimewalisha watoto na kuwalea, nao wameniasi.
Michée 1.2 Deutéronome 32.1 Deutéronome 4.26 Deutéronome 30.19 Michée 6.1-6.2
3 Ng’ombe amjua bwana wake, Na punda ajua kibanda cha bwana wake; Bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri.
Jérémie 8.7 Esaïe 44.18 Esaïe 5.12 Romains 1.28 Proverbes 6.6
4 Ole wake, taifa lenye dhambi, watu wanaochukua mzigo wa uovu, wazao wa watenda mabaya, watoto wanaoharibu; wamemwacha Bwana, wamemdharau yeye aliye Mtakatifu wa Israeli, wamefarakana naye na kurudi nyuma.
Esaïe 5.24 Jérémie 2.17 Jérémie 2.13 Jérémie 7.19 Esaïe 5.19
5 Mbona mnataka kupigwa hata sasa, hata mkazidi kuasi? Kichwa chote ni kigonjwa, moyo wote umezimia.
Jérémie 5.3 Esaïe 9.13 Esaïe 31.6 Daniel 9.8-9.11 Esaïe 1.23
6 Tangu wayo wa mguu hata kichwani hamna uzima ndani yake; bali jeraha na machubuko na vidonda vitokavyo usaha; havikufungwa, havikuzongwa-zongwa, wala havikulainishwa kwa mafuta.
Jérémie 6.14 Matthieu 9.12 Luc 10.34 Osée 5.12-5.13 Psaumes 77.2
7 Nchi yenu ni ukiwa; miji yenu imeteketezwa kwa moto; nchi yenu, wageni wameila mbele ya macho yenu; nayo ni ukiwa, kana kwamba imeangamizwa na wageni.
Esaïe 6.11 Lévitique 26.34 Esaïe 5.9 Esaïe 5.17 Esaïe 24.10-24.12
8 Na binti Sayuni ameachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kipenu katika shamba la matango, kama mji uliohusuriwa.
Zacharie 9.9 Jean 12.15 Zacharie 2.10 Esaïe 10.32 Job 27.18
9 Kama Bwana wa majeshi asingalituachia mabaki machache sana, tungalikuwa kama Sodoma, tungalifanana na Gomora.
Romains 9.29 Genèse 19.24 Esaïe 37.31-37.32 Lamentations 3.22 Esaïe 37.4
10 Lisikieni neno la Bwana, enyi waamuzi wa Sodoma; tegeni masikio msikie sheria ya Mungu wetu, enyi watu wa Gomora.
Apocalypse 11.8 Amos 3.1 Ezéchiel 16.46 Ezéchiel 16.49 Deutéronome 32.32
11 Huu wingi wa sadaka zenu mnazonitolea una faida gani? Asema Bwana. Nimejaa mafuta ya kafara za kondoo waume, na mafuta ya wanyama walionona; nami siifurahii damu ya ng’ombe wala ya wana-kondoo wala ya mbuzi waume.
Psaumes 50.8 Jérémie 6.20 1 Samuel 15.22 Malachie 1.10 Esaïe 66.3
12 Mjapo ili kuonekana mbele zangu, ni nani aliyetaka neno hili mikononi mwenu, kuzikanyaga nyua zangu?
Exode 23.17 Matthieu 23.5 Psaumes 40.6 Ecclésiaste 5.1 Esaïe 58.1-58.2
13 Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada.
Esaïe 66.3 Luc 11.42 Joël 2.15 Lévitique 23.1-23.44 Ezéchiel 20.39
14 Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua.
Esaïe 43.24 Amos 5.21 Zacharie 11.8 Esaïe 61.8 Malachie 2.17
15 Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.
Michée 3.4 Esaïe 59.2-59.3 1 Rois 8.22 Proverbes 1.28 Job 27.8-27.9
16 Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya;
Tite 2.11-2.14 2 Corinthiens 7.1 1 Pierre 3.11 Jacques 4.8 Apocalypse 7.14
17 jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane.
Jérémie 22.3 Sophonie 2.3 Esaïe 1.23 Psaumes 82.3-82.4 Proverbes 31.9
18 Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.
Psaumes 51.7 Esaïe 43.24-43.26 Apocalypse 7.14 Esaïe 41.21 Esaïe 44.22
19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi;
Deutéronome 30.15-30.16 Esaïe 3.10 Joël 2.26 Osée 14.1-14.4 Matthieu 21.28-21.32
20 bali kama mkikataa na kuasi mtaangamizwa kwa upanga; maana kinywa cha Bwana kimenena haya.
Esaïe 58.14 Esaïe 40.5 Esaïe 65.12 Michée 4.4 Tite 1.2
21 Mji huu uliokuwa mwaminifu umekuwaje kahaba! Yeye aliyejaa hukumu ya haki; haki ilikaa ndani yake, bali sasa wauaji!
Luc 13.34 Ezéchiel 22.1-22.23 Esaïe 48.2 Jérémie 2.20-2.21 Actes 7.52
22 Fedha yako imekuwa takataka, divai yako imechanganywa na maji.
Ezéchiel 22.18-22.22 Jérémie 6.28-6.30 Osée 4.18 Lamentations 4.1-4.2 2 Corinthiens 2.17
23 Wakuu wako ni waasi, na rafiki za wevi; kila mtu hupenda rushwa, hufuata malipo; hawampatii yatima haki yake, wala maneno ya mjane hayawawasilii.
Michée 7.3 Zacharie 7.10 Exode 23.8 Esaïe 3.14 Actes 4.5-4.11
24 Kwa hiyo, asema Bwana, Bwana wa majeshi, Mwenye enzi, wa Israeli, Nitapata faraja kwa hao wanipingao, nitatwaa kisasi kwa adui zangu;
Deutéronome 28.63 Esaïe 60.16 Esaïe 49.26 Hébreux 10.13 Deutéronome 32.43
25 nami nitakuelekezea wewe mkono wangu, na kukutakasa takataka zako kabisa, na kukuondolea bati lako lote;
Malachie 3.3 Sophonie 3.11 Esaïe 6.11-6.13 Jérémie 9.7 Zacharie 13.7-13.9
26 nami nitarejeza upya waamuzi wako kama walivyokuwa hapo kwanza, na washauri wako kama hapo mwanzo; baada ya hayo utaitwa, Mji wa haki, mji mwaminifu.
Jérémie 33.7 Zacharie 8.3 Esaïe 62.1-62.2 Esaïe 32.1-32.2 Nombres 12.3
27 Sayuni itakombolewa kwa hukumu, na waongofu wake kwa haki.
1 Corinthiens 1.30 Esaïe 63.4 Romains 11.26-11.27 Ephésiens 1.7-1.8 Tite 2.14
28 Lakini kuharibika kwao wakosao nao wenye dhambi kutatokea wakati mmoja, nao wamwachao Bwana watateketezwa.
Esaïe 30.13 2 Thessaloniciens 1.8-1.9 Job 31.3 Psaumes 1.6 1 Rois 9.6-9.9
29 Kwa maana watatahayarika kwa sababu ya mialoni mliyoitamani, nanyi mtaaibishwa kwa sababu ya bustani mlizozichagua.
Esaïe 66.17 Esaïe 57.5 Esaïe 65.3 Osée 4.13 Esaïe 31.7
30 Maana mtakuwa kama mwaloni ambao majani yake yakauka, na kama bustani isiyo na maji.
Jérémie 17.5-17.6 Esaïe 5.6 Jérémie 31.12 Ezéchiel 17.9-17.10 Ezéchiel 17.24
31 Na mtu hodari atakuwa kama makumbi, na kazi yake kama cheche ya moto; nao watawaka pamoja, wala hapana atakayewazima.
Esaïe 66.24 Matthieu 3.10 Apocalypse 19.20 Marc 9.43-9.49 Esaïe 5.24

Cette Bible est dans le domaine public.