Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 7.1
Bible en Swahili de l’est


Les filles de Jérusalem

1 Siti msharifu, jinsi zilivyo nzuri Hatua zako katika mitalawanda. Mapaja yako ya mviringo ni kama johari, Kazi ya mikono ya fundi mstadi;
Psaumes 45.13 Exode 28.15 Luc 15.22 Daniel 2.32 Exode 35.35

Le jeune homme

2 Kitovu chako ni kama bilauri iliyoviringana, Na isikose divai iliyochanganyika; Tumbo lako ni mfano wa chungu ya ngano, Iliyozungukwa na ugo wa nyinyoro;
Romains 7.4 Psaumes 45.16 Esaïe 46.3 Proverbes 3.8 Cantique 5.14
3 Maziwa yako mawili ni kama wana-paa wawili, Ambao ni mapacha ya paa;
Cantique 4.5 Cantique 6.6
4 Shingo yako ni kama huo mnara wa pembe; Macho yako kama viziwa vya Heshboni, Karibu na mlango wa Beth-rabi; Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni, Unaoelekea Dameski;
Cantique 4.4 Psaumes 144.12 Cantique 5.14-5.15 1 Rois 10.22 Esaïe 54.4
5 Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli, Na nywele za kichwa chako kama urujuani, Mfalme amenaswa na mashungu yake.
Esaïe 35.2 Cantique 4.1 Michée 7.14 Ephésiens 1.22 Colossiens 2.19
6 Jinsi yalivyo mazuri, yalivyo matamu, Mapenzi katikati ya anasa!
Cantique 1.15-1.16 Cantique 4.10 Psaumes 45.11 Cantique 7.10 Cantique 4.7
7 Kimo chako kimefanana na mtende, Na maziwa yako na vichala.
Cantique 4.5 Cantique 7.3 Ephésiens 3.17 Ephésiens 4.13 Cantique 8.8
8 Nilisema, Nitapanda huo mtende, Na kuyashika makuti yake. Maziwa yako na yawe kama vichala vya mzabibu, Na harufu ya pumzi yako kama mapera;
Cantique 2.3 Jean 14.21-14.23 2 Corinthiens 2.14 Cantique 1.3 Jérémie 32.41
9 Na kinywa chako kama divai iliyo bora, Kwa mpendwa wangu inashuka taratibu, Ikitiririka midomoni mwao walalao.
Cantique 5.16 Actes 2.46-2.47 Colossiens 4.6 Apocalypse 14.13 Colossiens 3.16-3.17
10 Mimi ni wake mpendwa wangu, Na shauku yake ni juu yangu.
Cantique 2.16 Psaumes 45.11 Cantique 6.3 Galates 2.20 Actes 27.23
11 Njoo, mpendwa wangu, twende mashambani, Tufanye maskani katika vijiji.
Cantique 4.8 Cantique 2.10-2.13 Cantique 1.4
12 Twende mapema hata mashamba ya mizabibu, Tuone kama mzabihu umechanua, Na maua yake yamefunuka; Kama mikomamanga imetoa maua; Huko nitakupa pambaja zangu.
Cantique 6.11 Ephésiens 6.24 Esaïe 18.5 Psaumes 63.3-63.8 Hébreux 2.15
13 Mitunguja hutoa harufu yake; Juu ya milango yetu yako matunda mazuri, Mapya na ya kale, ya kila namna, Niliyokuwekea, mpendwa wangu.
Genèse 30.14 Matthieu 13.52 Cantique 4.13 Jean 15.8 Esaïe 23.18

Cette Bible est dans le domaine public.