Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 1.11
Bible en Swahili de l’est


La jeune femme

1 Wimbo ulio bora, wa Sulemani.
2 Kubusu na anibusu kwa kinywa chake. Maana pambaja zako zapita divai;
Psaumes 63.3-63.5 Cantique 1.4 Cantique 4.10 Esaïe 55.1-55.2 Cantique 8.1-8.2
3 Manukato yako yanukia vizuri; Jina lako ni kama marhamu iliyomiminwa; Kwa hiyo wanawali hukupenda.
Ecclésiaste 7.1 Cantique 4.10 Jean 12.3 Psaumes 45.14 Exode 30.23-30.28
4 Nivute nyuma yako, na tukimbie; Mfalme ameniingiza vyumbani mwake. Tutafurahi na kukushangilia; Tutazinena pambaja zako kuliko divai; Ndiyo, ina haki wakupende.
Jean 6.44 Psaumes 45.14-45.15 Osée 11.4 Ephésiens 2.6 Psaumes 119.32

La jeune femme

5 Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, Enyi binti za Yerusalemu, Mfano wa hema za Kedari, Kama mapazia yake Sulemani.
Psaumes 120.5 Cantique 5.8 Cantique 2.14 Cantique 5.16 Cantique 4.3
6 Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi, Kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mamangu walinikasirikia, Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu; Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda.
Psaumes 69.8 Cantique 8.11-8.12 Michée 7.6 Marc 4.6 Matthieu 10.22
7 Nijulishe, ee mpendwa wa nafsi yangu, Ni wapi utakapolisha kundi lako, Ni wapi utakapolilaza adhuhuri. Kwa nini niwe kama aliyefungiwa kidoto, Karibu na makundi ya wenzako?
Cantique 3.1-3.4 Psaumes 23.1-23.2 Esaïe 13.20 Cantique 5.8 Matthieu 10.37

Les filles de Jérusalem

8 Usipojua, wewe uliye mzuri katika wanawake, Shika njia uzifuate nyayo za kondoo, Na kuwalisha wana-mbuzi wako Karibu na hema za wachungaji.
Cantique 6.1 Cantique 5.9 1 Corinthiens 11.1 Jérémie 6.16 Psaumes 45.13

Le jeune homme

9 Mpenzi wangu, nimekulinganisha Na farasi katika magari ya Farao.
Cantique 2.13 Cantique 2.2 Cantique 2.10 Cantique 5.2 Esaïe 31.1
10 Mashavu yako ni mazuri kwa mashada, Shingo yako kwa mikufu ya vito.
Ezéchiel 16.11-16.13 Cantique 5.13 1 Pierre 3.4 2 Pierre 1.3-1.4 Esaïe 3.18-3.21

Les filles de Jérusalem

11 Tutakufanyizia mashada ya dhahabu, Yenye vifungo vya fedha.
Psaumes 149.4 Philippiens 3.21 Ephésiens 5.25-5.27 Cantique 8.9 Genèse 1.26

La jeune femme

12 Muda mfalme alipoketi juu ya matakia, Nardo yangu ilitoa harufu yake.
Jean 12.3 Matthieu 22.11 Philippiens 4.18 Apocalypse 8.3-8.4 Apocalypse 3.20
13 Mpendwa wangu ni kama mfuko wa manemane Ukilazwa usiku maziwani mwangu.
Psaumes 45.8 Jean 19.39 Cantique 3.5 Cantique 5.1 Cantique 2.7
14 Mpendwa wangu ni kama kishada cha hina, Katika mizabibu huko Engedi.
Cantique 2.3 Cantique 4.13-4.14 Cantique 1.13 1 Samuel 23.29-24.1 Josué 15.62

Le jeune homme

15 Tazama, u mzuri, mpenzi wangu, U mzuri, macho yako ni kama ya hua.
Cantique 4.1 Cantique 5.12 Cantique 4.7 Cantique 5.2 Cantique 6.4

La jeune femme

16 Tazama, u mzuri, mpendwa wangu, Wapendeza, na kitanda chetu ni majani;
Cantique 2.3 Zacharie 9.17 Cantique 5.10-5.16 Cantique 3.7 Psaumes 45.2
17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, Na viguzo vyetu ni miberoshi.
Hébreux 11.10 2 Chroniques 2.8-2.9 Cantique 7.5 1 Pierre 2.4-2.5 Cantique 8.9

Cette Bible est dans le domaine public.