Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 11.9
Bible en Swahili de l’est


Activité saine et réjouissance

1 Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi.
Proverbes 19.17 Matthieu 10.42 Hébreux 6.10 Ecclésiaste 11.6 Esaïe 32.20
2 Uwagawie sehemu watu saba, hata wanane; Maana hujui baa gani litakalokuwa juu ya nchi.
1 Timothée 6.18-6.19 Psaumes 112.9 Job 5.19 Proverbes 6.16 Ephésiens 5.16
3 Mawingu yakiwa yamejaa mvua, Yataimimina juu ya nchi; Na mti ukianguka kuelekea kusini, au kaskazini, Paangukapo ule mti, papo hapo utalala.
Psaumes 65.9-65.13 Esaïe 55.10-55.11 1 Rois 18.45 1 Jean 3.17 Luc 13.7
4 Mwenye kuuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna.
Proverbes 22.13 Proverbes 3.27 Proverbes 20.4
5 Kama vile wewe usipojua njia ya upepo ni ipi, wala jinsi mifupa ikuavyo tumboni mwake mja mzito; kadhalika huijui kazi ya Mungu, afanyaye mambo yote.
Jean 3.8 Ecclésiaste 8.17 Psaumes 92.5 Psaumes 40.5 Psaumes 139.13-139.16
6 Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiuzuie mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa,kama ni hii au hii,au kama zote zitafaa sawasawa.
Ecclésiaste 9.10 2 Timothée 4.2 Jean 4.36-4.38 Aggée 1.6-1.11 Actes 11.20-11.21
7 Kweli nuru ni tamu, tena ni jambo la kupendeza macho kutazama jua.
Ecclésiaste 7.11 Matthieu 5.45 Psaumes 56.13 Job 33.28 Ecclésiaste 6.5
8 Naam, mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie yote; lakini na azikumbuke siku zijazo za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Mambo yote yajayo ni ubatili.
Job 14.10 Joël 2.2 Job 18.18 Ecclésiaste 2.1-2.11 Jean 12.35

Le moment favorable pour rechercher Dieu

9 Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni.
Ecclésiaste 12.14 Ecclésiaste 3.17 Romains 14.10 Job 31.7 Ecclésiaste 2.10
10 Kwa hiyo ondoa majonzi moyoni mwako, nawe uuondoe ubaya mwilini mwako; kwa maana ujana ni ubatili, na utu uzima pia.
2 Timothée 2.22 2 Corinthiens 7.1 Psaumes 39.5 Proverbes 22.15 Job 13.26

Cette Bible est dans le domaine public.