Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 30.8
Bible en Swahili de l’est


Proverbes d’Agur

La relation avec Dieu

1 Maneno ya Aguri bin Yake; mausia mtu huyu aliyomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.
Proverbes 31.1 2 Pierre 1.19-1.21
2 Hakika nimekuwa kama mnyama, wala si mtu; Wala sina ufahamu wa mwanadamu;
Psaumes 73.22 1 Corinthiens 3.18 Jacques 1.5 1 Corinthiens 8.2 Romains 11.25
3 Wala sikujifunza hekima; Wala sina maarifa ya kumjua Mtakatifu.
Proverbes 9.10 Matthieu 16.17 Esaïe 6.3 Matthieu 11.27 Romains 11.33
4 Ni nani aliyepanda mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo kwa makonzi yake? Ni nani aliyeyafunga maji ndani ya nguo yake? Ni nani aliyefanya imara ncha zote za nchi? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua?
Jean 3.13 Esaïe 7.14 Deutéronome 30.12 Job 38.4-38.41 Apocalypse 19.12
5 Kila neno la Mungu limehakikishwa; Yeye ni ngao yao wamwaminio.
Psaumes 18.30 Psaumes 12.6 Psaumes 84.11 Psaumes 3.3 Psaumes 119.140
6 Usiongeze neno katika maneno yake; Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.
Deutéronome 4.2 Deutéronome 12.32 Apocalypse 22.18-22.19 Job 13.7-13.9 1 Corinthiens 15.15
7 Mambo haya mawili nimekuomba; Usininyime [matatu] kabla sijafa.
2 Rois 2.9 Psaumes 27.4 Psaumes 21.2 Luc 10.42 1 Rois 3.5-3.9
8 Uniondolee ubatili na uongo; Usinipe umaskini wala utajiri; Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.
Matthieu 6.11 1 Timothée 6.6-6.8 Psaumes 62.9-62.10 Luc 11.3 Psaumes 119.29
9 Nisije nikashiba nikakukana, Nikasema, Bwana ni nani? Wala nisiwe maskini sana nikaiba, Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.
Deutéronome 31.20 Osée 13.6 Job 31.24-31.28 Deutéronome 8.10-8.14 Ezéchiel 16.49-16.50
10 Usimchongee mtumwa kwa bwana wake; Asije akakulaani, ukaonekana una hatia.
Deutéronome 15.9 2 Chroniques 24.22-24.24 2 Samuel 19.26-19.27 Proverbes 24.23-24.24 Ecclésiaste 7.21
11 Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao.
Proverbes 20.20 Proverbes 30.17 Deutéronome 27.16 Proverbes 30.12-30.14 Lévitique 20.9
12 Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe; Ambao hawakuoshwa uchafu wao.
Luc 18.11 Proverbes 16.2 Jérémie 2.35 Esaïe 65.5 Psaumes 36.2
13 Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana.
Proverbes 6.17 Esaïe 2.11 Proverbes 21.4 Ezéchiel 28.9 Psaumes 131.1
14 Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni kama visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.
Psaumes 57.4 Psaumes 3.7 Psaumes 14.4 Job 29.17 Amos 8.4
15 Mruba anao binti wawili, Waliao, Nipe! Nipe! Kuna vitu vitatu visivyoshiba kamwe, Naam, vinne visivyosema, Basi!
Proverbes 30.29 Proverbes 30.21 Proverbes 6.16 Osée 4.18 Amos 1.13
16 Kuzimu; na tumbo lisilozaa; Nchi isiyoshiba maji; na moto usiosema, Basi!
Proverbes 27.20 Habakuk 2.5 Genèse 30.1
17 Jicho la mtu amdhihakiye babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling’oa, Na vifaranga vya tai watalila.
Proverbes 23.22 Deutéronome 21.18-21.21 Proverbes 30.11 2 Samuel 18.9-18.10 Genèse 9.21-9.27
18 Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu.
Job 42.3 Psaumes 139.6
19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.
Job 39.27 Esaïe 40.31 Exode 22.16
20 Hivyo ndivyo mwendo wa mwanamke mzinifu; Hula, akapangusa kinywa chake, Akasema, Sikufanya uovu.
Proverbes 7.13-7.23 Nombres 5.11-5.30 Proverbes 5.6
21 Kwa ajili ya mambo matatu nchi hutetemeka, Naam, kwa ajili ya manne haiwezi kuvumilia.
22 Mtumwa apatapo kuwa mfalme; Mpumbavu ashibapo chakula;
Proverbes 19.10 Ecclésiaste 10.7 1 Samuel 25.36-25.38 1 Samuel 30.16 1 Samuel 25.25
23 Mwanamke mwenye kuchukiza aolewapo; Na mjakazi aliye mrithi wa bibi yake.
Proverbes 21.19 Proverbes 21.9 Proverbes 19.13 Proverbes 27.15 Proverbes 29.21
24 Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana.
Job 12.7
25 Chungu ni watu wasio na nguvu; Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.
Proverbes 6.6-6.8
26 Wibari ni watu dhaifu; Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.
Psaumes 104.18 Lévitique 11.5
27 Nzige hawana mfalme; Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.
Exode 10.4-10.6 Joël 2.25 Psaumes 105.34 Joël 1.6-1.7 Exode 10.13-10.15
28 Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme.
29 Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza, Naam, wanne walio na mwendo mzuri.
30 Simba aliye hodari kupita wanyama wote; Wala hajiepushi na aliye yote;
Juges 14.18 Nombres 23.24
31 Jimbi aendaye tambo; na beberu; Na mfalme ambaye haasiki.
Proverbes 16.14 Proverbes 20.2 Daniel 3.15-3.18
32 Ikiwa umefanya kipumbavu kwa kujikuza; Au ikiwa umewaza mabaya; Basi weka mkono wako juu ya kinywa chako.
Job 21.5 Job 40.4 Michée 7.16-7.17 Proverbes 17.28 Ecclésiaste 8.3-8.4
33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi; Na kupiga pua hutokeza damu; kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.
Proverbes 29.22 Proverbes 15.18 Proverbes 16.28 Proverbes 28.25 Proverbes 17.14

Cette Bible est dans le domaine public.