Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 26.16
Bible en Swahili de l’est


Les relations avec le stupide

1 Kama theluji wakati wa joto, na mvua wakati wa mavuno; Kadhalika heshima haimpasi mpumbavu.
Psaumes 12.8 Proverbes 26.8 Proverbes 17.7 Psaumes 15.4 Proverbes 28.16
2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpigi mtu.
Nombres 23.8 2 Samuel 16.12 1 Samuel 14.28-14.29 Néhémie 13.2 Deutéronome 23.4-23.5
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, Na fimbo kwa mgongo wa mpumbavu.
Psaumes 32.9 Proverbes 10.13 1 Corinthiens 4.21 Proverbes 17.10 Proverbes 19.25
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Usije ukafanana naye.
Proverbes 17.14 2 Samuel 19.41-19.43 1 Pierre 2.21-2.23 1 Pierre 3.9 Proverbes 26.5
5 Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Asije akawa mwenye hekima machoni pake.
Romains 12.16 Proverbes 28.11 Matthieu 16.1-16.4 Matthieu 22.15-22.32 Romains 11.25
6 Apelekaye ujumbe kwa mkono wa mpumbavu Hujikata miguu, na kunywa hasara.
Proverbes 13.17 Proverbes 10.26 Proverbes 25.13 Nombres 13.31
7 Miguu yake achechemeaye huwa dhaifu; Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Matthieu 7.4-7.5 Proverbes 26.9 Psaumes 50.16-50.21 Psaumes 64.8 Luc 4.23
8 Kama mfuko wa vito katika chungu ya mawe; Kadhalika mtu amheshimuye mpumbavu.
Proverbes 26.1 Proverbes 30.22 Proverbes 19.10
9 Kama mwiba uingiao katika mkono wa mlevi; Kadhalika mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Proverbes 23.35
10 Fundi stadi hufanyiza vitu vyote; Bali amwajiriye mpumbavu ni kama awaajiriye watu wapitao.
Proverbes 11.31 Romains 2.6
11 Kama vile mbwa arudiavyo matapiko yake; Kadhalika mpumbavu afanya upumbavu tena.
Exode 8.15 2 Pierre 2.22 Matthieu 12.45
12 Je! Wamwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.
Proverbes 29.20 Matthieu 21.31 1 Corinthiens 3.18-3.19 Romains 12.16 Proverbes 28.11
13 Mtu mvivu husema, Simba yuko njiani, Simba yuko katika njia kuu.
Proverbes 22.13 Proverbes 19.15 Proverbes 15.19
14 Kama vile mlango ugeukavyo katika bawaba zake; Kadhalika mtu mvivu katika kitanda chake.
Hébreux 6.12 Proverbes 6.9-6.10 Proverbes 12.27 Proverbes 12.24 Proverbes 24.33
15 Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini; Kwamchosha kuupeleka tena kinywani pake.
Proverbes 19.24
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake, Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.
1 Pierre 3.15 Proverbes 26.12 Proverbes 12.15
17 Mtu apitaye na kujisumbua kwa ugomvi usio wake; Ni kama mtu ashikaye mbwa kwa masikio yake.
Proverbes 20.3 Proverbes 17.11 2 Timothée 2.23-2.24 Luc 12.14 Proverbes 18.6
18 Kama mtu mwenye wazimu atupaye mienge, Na mishale, na mauti;
Esaïe 50.11 Proverbes 25.18 Genèse 49.23 Proverbes 7.23
19 Ndivyo alivyo amdanganyaye mwenzake, Na kusema, Je! Sikufanya mzaha tu?
Ephésiens 5.4 Proverbes 10.23 Proverbes 14.9 2 Pierre 2.13 Proverbes 15.21
20 Moto hufa kwa kukosa kuni; Na bila mchongezi fitina hukoma.
Proverbes 16.28 Proverbes 22.10 Jacques 3.6 Proverbes 26.22
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, Na kama kuni juu ya moto; Ndivyo mtu mgomvi achocheavyo uadui.
Proverbes 15.18 Proverbes 29.22 1 Rois 12.2-12.3 1 Rois 12.20 2 Samuel 20.1
22 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo. Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.
Proverbes 18.8 Proverbes 20.19 Ezéchiel 22.9
23 Midomo ijipendekezayo pamoja na moyo mbaya Ni kama kigae kilichofunikizwa taka za fedha.
Luc 22.47-22.48 Luc 11.39 Ezéchiel 33.31 Proverbes 25.4 Proverbes 10.18
24 Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake; Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.
Proverbes 12.20 Proverbes 12.5 Proverbes 12.17 Proverbes 10.18 Psaumes 41.6
25 Anenapo maneno mazuri usimsadiki; Kwa maana ana machukizo saba moyoni mwake.
Proverbes 6.16-6.19 Jérémie 12.6 Psaumes 28.3 Jérémie 9.2-9.8 Matthieu 24.23
26 Ingawa chuki hufunikizwa kwa hila; Uovu wake utadhihirika mbele ya kusanyiko.
Genèse 4.8 2 Samuel 13.22-13.28 Psaumes 55.21-55.23 1 Samuel 18.21 2 Samuel 3.27-3.30
27 Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe; Naye abingirishaye jiwe litamrudia.
Proverbes 28.10 Esther 7.10 Psaumes 9.15 Psaumes 7.15-7.16 Psaumes 10.2
28 Ulimi unenao uongo huwachukia wale uliowajeruhi; Na kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
Proverbes 29.5 Jean 8.40 Jean 10.32-10.33 Jean 15.22-15.24 Jean 8.44-8.49

Cette Bible est dans le domaine public.