Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 25.1
Bible en Swahili de l’est


Proverbes de Salomon

Les relations

1 Hizi nazo ni mithali za Sulemani, ambazo watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda, walizinakili.
Proverbes 1.1 1 Rois 4.32 Esaïe 37.2 Esaïe 1.1 Proverbes 10.1
2 Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo; Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo.
Deutéronome 29.29 Romains 11.33-11.34 1 Rois 3.9-3.28 Job 29.16 Job 42.3
3 Mbingu huenda juu sana, na nchi huenda chini; Lakini mioyo ya wafalme haichunguziki.
Romains 8.39 1 Rois 4.29 Psaumes 103.11 Esaïe 7.11 1 Pierre 1.7
4 Ondoa takataka katika fedha, Na chombo kitatokea kwa mtakasaji;
2 Timothée 2.20-2.21 Ezéchiel 22.18 Proverbes 17.3 Esaïe 1.25-1.27 Malachie 3.2-3.3
5 Mwondoe asiye haki mbele ya mfalme, Na kiti chake cha enzi kitathibitika katika haki.
Proverbes 20.8 Proverbes 16.12 Proverbes 20.28 Proverbes 29.14 Esaïe 9.7
6 Usijitukuze mbele ya uso wa mfalme; Wala usisimame mahali pa watu wakuu;
Proverbes 27.2 Proverbes 25.27 Psaumes 131.1 1 Samuel 9.20-9.22 1 Samuel 15.17
7 Kwa maana ni heri kuambiwa, Njoo huku mbele; Kuliko kuwekwa nyuma machoni pa mkuu. Yale uliyoyaona kwa macho,
Luc 14.7-14.11 Luc 18.14 1 Pierre 5.5 Apocalypse 4.1 Proverbes 16.19
8 Usitoke nje kwa haraka ili kuyashindania; Usije ukakosa kujua la kutenda hatimaye, Mwenzako atakapokuwa amekuaibisha.
Matthieu 5.25 Proverbes 17.14 Proverbes 30.33 Proverbes 18.6 Proverbes 14.12
9 Ujitetee na mwenzako peke yake; Bali usiifunue siri ya mtu mwingine;
Proverbes 11.13 Matthieu 18.5-18.17 Proverbes 20.19
10 Yeye asikiaye asije akakutukana; Na aibu yako isiondoke.
Psaumes 119.39
11 Neno linenwalo wakati wa kufaa, Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.
Proverbes 15.23 Esaïe 50.4 Ecclésiaste 12.10 Proverbes 24.26
12 Kipuli cha dhahabu, na pambo la dhahabu safi; Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo.
Psaumes 141.5 Proverbes 15.5 Proverbes 20.12 Job 42.11 Proverbes 1.8-1.9
13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao; Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao.
Proverbes 13.17 Proverbes 26.6 Philippiens 2.25-2.30 Proverbes 25.25
14 Kama mawingu na upepo pasipo mvua; Ndivyo alivyo yeye ajisifiaye karama kwa uongo.
Proverbes 20.6 1 Rois 22.11 2 Pierre 2.15-2.19 Jude 1.12-1.13 Luc 18.10-18.14
15 Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa; Na ulimi laini huvunja mfupa.
Ecclésiaste 10.4 Proverbes 15.1 Proverbes 16.14 1 Samuel 25.24-25.44 1 Samuel 25.14
16 Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha; Usije ukashiba na kuitapika.
Proverbes 25.27 Proverbes 24.13-24.14 Ephésiens 5.18 Juges 14.8-14.9 Esaïe 7.22
17 Mguu wako usiingie katika nyumba ya jirani yako ila kwa kiasi; Asije akakukinai na kukuchukia.
Juges 19.18-19.21 Genèse 19.2-19.3
18 Mtu amshuhudiaye jirani yake uongo Ni nyundo, na upanga, na mshale mkali.
Psaumes 57.4 Proverbes 12.18 Jérémie 9.8 Psaumes 120.3-120.4 Psaumes 52.2
19 Kumtumaini asiye mwaminifu wakati wa taabu Ni kama jino lililovunjika, au mguu ulioteguka.
Esaïe 30.1-30.3 Job 6.14-6.20 2 Chroniques 28.20-28.21 Esaïe 36.6 2 Timothée 4.16
20 Amwimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito, Ni kama yeye avuaye nguo wakati wa baridi; Ni kama siki juu ya magadi.
Romains 12.15 Ecclésiaste 3.4 Deutéronome 24.12-24.17 Daniel 6.18 Psaumes 137.3-137.4
21 Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa;
Exode 23.4-23.5 Romains 12.20-12.21 Matthieu 5.44 Proverbes 24.17 Luc 10.33-10.36
22 Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na Bwana atakupa thawabu.
2 Samuel 16.12 1 Corinthiens 15.18 Matthieu 10.13
23 Upepo wa kusi huleta mvua; Vile vile asingiziaye huleta uso wa ghadhabu.
Psaumes 101.5 Job 37.22 Psaumes 15.3 Romains 1.30 Proverbes 26.20
24 Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.
Proverbes 21.9 Proverbes 19.13 Proverbes 21.19 Proverbes 27.15-27.16
25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu, Ndivyo ilivyo habari njema itokayo katika nchi ya mbali.
Proverbes 15.30 Psaumes 42.1-42.2 Jérémie 18.14 Luc 2.10-2.11 Psaumes 63.1
26 Mwenye haki amwangukiapo mtu mbaya Ni kama chemchemi iliyochafuka, Na kisima kilichokanyagwa.
Matthieu 23.34-23.37 Ezéchiel 34.18-34.19 Ezéchiel 32.2 Matthieu 26.69-26.74 Apocalypse 17.6
27 Haifai kula asali nyingi mno; Vile vile mtu kutafuta utukufu wake mwenyewe si utukufu.
Proverbes 27.2 Philippiens 2.3 2 Corinthiens 12.1 Jean 5.44 Proverbes 25.16
28 Asiyetawala roho yake Ni mfano wa mji uliobomolewa, usio na kuta.
Proverbes 16.32 1 Samuel 20.30 2 Chroniques 32.5 1 Samuel 25.17 Néhémie 1.3

Cette Bible est dans le domaine public.