Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 94.14
Bible en Swahili de l’est


Jugement des méchants

1 Ee Bwana, Mungu wa kisasi, Mungu wa kisasi, uangaze,
Nahum 1.2 Deutéronome 32.35 Esaïe 35.4 Romains 12.19 Psaumes 80.1
2 Mwenye kuihukumu nchi, ujitukuze, Uwape wenye kiburi stahili zao.
Psaumes 31.23 Genèse 18.25 Psaumes 7.6 Daniel 4.37 Psaumes 50.6
3 Bwana, hata lini wasio haki, Hata lini wasio haki watashangilia?
Job 20.5 Apocalypse 6.10 Psaumes 43.2 Esther 7.10 Psaumes 74.9-74.10
4 Je! Wote watendao uovu watatoa maneno, Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?
Psaumes 31.18 Psaumes 52.1 Matthieu 12.34 Daniel 7.11 Psaumes 10.2-10.7
5 Ee Bwana, wanawaseta watu wako; Wanautesa urithi wako;
Esaïe 3.15 Apocalypse 17.6 Jérémie 50.11 Esaïe 52.5 Psaumes 7.2
6 Wanamwua mjane na mgeni; Wanawafisha yatima.
Esaïe 10.2 Jérémie 7.6 Ezéchiel 22.7 Jérémie 22.3 Malachie 3.5
7 Nao husema, Bwana haoni; Mungu wa Yakobo hafikiri.
Job 22.12-22.13 Psaumes 59.7 Ezéchiel 9.9 Luc 18.3-18.4 Ezéchiel 8.12
8 Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini; Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?
Psaumes 92.6 Psaumes 49.10 Jérémie 8.6-8.8 Romains 3.11 Tite 3.3
9 Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? Aliyelifanya jicho asione?
Exode 4.11 Proverbes 20.12 Psaumes 44.21 Psaumes 11.4 Jérémie 23.23-23.24
10 Awaadibuye mataifa asikemee? Amfundishaye mwanadamu asijue?
Job 35.11 Esaïe 28.26 Psaumes 44.2 Esaïe 37.36 Esaïe 10.12
11 Bwana anajua mawazo ya mwanadamu, Ya kuwa ni ubatili.
1 Corinthiens 3.20 1 Corinthiens 1.21 Psaumes 49.10-49.13 Job 11.11-11.12 1 Corinthiens 1.25
12 Ee Bwana, heri mtu yule umwadibuye, Na kumfundisha kwa sheria yako;
Proverbes 3.11-3.12 Job 5.17 Hébreux 12.5-12.11 Psaumes 119.71 1 Corinthiens 11.32
13 Upate kumstarehesha siku za mabaya, Hata asiye haki atakapochimbiwa shimo.
Psaumes 55.23 Psaumes 9.15 Apocalypse 14.13 2 Pierre 2.9 Habakuk 3.16
14 Kwa kuwa Bwana hatawatupa watu wake, Wala hutauacha urithi wake,
1 Samuel 12.22 Psaumes 37.28 Romains 11.1-11.2 Deutéronome 32.9 Romains 8.38-8.39
15 Maana hukumu itairejea haki, Na wote walio wanyofu wa moyo wataifuata.
Michée 7.9 Job 23.11-23.12 Esaïe 42.3 Psaumes 37.34 Psaumes 97.2
16 Ni nani atakayesimama Kwa ajili yangu juu ya wabaya? Ni nani atakayenisaidia Juu yao wafanyao maovu?
1 Rois 18.39-18.40 Jérémie 5.1 Jean 7.50-7.51 Psaumes 17.13 Nombres 10.35
17 Kama Bwana asingalikuwa msaada wangu, Nafsi yangu kwa upesi ingalikaa penye kimya.
Psaumes 124.1-124.2 Psaumes 31.17 Psaumes 118.13 Psaumes 13.3 Psaumes 125.1
18 Niliposema, Mguu wangu unateleza; Ee Bwana, fadhili zako zilinitegemeza.
Psaumes 38.16 Psaumes 37.23-37.24 Psaumes 121.3 Psaumes 119.116-119.117 Esaïe 41.10
19 Katika wingi wa mawazo ya moyoni mwangu, Faraja zako zaifurahisha roho yangu.
Psaumes 77.2-77.10 Psaumes 61.2 Habakuk 3.16-3.18 1 Pierre 1.7-1.8 Romains 5.2-5.5
20 Je! Kiti cha udhalimu kishirikiane nawe, Kitungacho madhara kwa njia ya sheria?
Psaumes 58.2 Amos 6.3 Esaïe 10.1 1 Samuel 22.12 Daniel 6.7-6.9
21 Huishambulia nafsi yake mwenye haki, Na kuihukumu damu isiyo na hatia.
Proverbes 17.15 Matthieu 27.1 Exode 23.7 Psaumes 59.3 Psaumes 2.1-2.3
22 Lakini Bwana amekuwa ngome kwangu, Na Mungu wangu mwamba wangu wa kukimbilia.
Psaumes 18.2 Psaumes 59.9 Psaumes 62.2 Psaumes 9.9 Psaumes 59.16-59.17
23 Naye atawarudishia uovu wao, Atawaangamiza katika ubaya wao, Naam, Bwana, Mungu wetu, atawaangamiza.
Psaumes 7.16 Proverbes 2.22 Psaumes 9.16-9.17 1 Samuel 26.10-26.11 Esther 7.10

Cette Bible est dans le domaine public.