Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 69.8
Bible en Swahili de l’est


Prière du juste opprimé

1 Ee Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu.
Psaumes 69.14-69.15 Psaumes 42.7 Psaumes 45.1 Esaïe 43.2 Psaumes 69.2
2 Ninazama katika matope mengi, Pasipowezekana kusimama. Nimefika penye maji ya vilindi, Mkondo wa maji unanigharikisha.
Psaumes 40.2 Jérémie 38.22 Ezéchiel 27.26-27.34 Matthieu 7.25 Psaumes 32.6
3 Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofu Kwa kumngoja Mungu wangu.
Esaïe 38.14 Psaumes 119.82 Psaumes 6.6 Deutéronome 28.32 Psaumes 119.123
4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua.
Psaumes 35.19 Jean 15.25 Psaumes 40.12 Esaïe 53.4-53.7 Psaumes 109.3-109.5
5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu, Wala hukufichwa dhambi yangu.
Psaumes 44.20-44.21 Psaumes 38.9 Psaumes 19.12 Jérémie 16.17 Psaumes 17.3
6 Wanaokungoja Wewe wasiaibishwe, Kwa ajili yangu, Bwana, MUNGU wa majeshi. Wanaokutafuta Wewe wasifedheheshwe, Kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli.
Actes 13.17 Psaumes 35.26 Luc 24.19-24.21 Actes 4.7 Esaïe 49.23
7 Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, Fedheha imenifunika uso wangu.
Jérémie 15.15 Esaïe 50.6 Psaumes 44.22 Psaumes 22.6-22.8 Matthieu 27.38-27.44
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu.
Psaumes 31.11 Psaumes 38.11 Jean 1.11 Job 19.13-19.19 Matthieu 10.21-10.22
9 Maana wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.
Romains 15.3 Psaumes 119.139 Jean 2.14-2.17 Psaumes 89.50-89.51 1 Chroniques 29.3
10 Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.
Psaumes 35.13 Luc 7.33-7.34 Psaumes 102.8-102.9 Psaumes 109.24-109.25
11 Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao.
1 Rois 9.7 Job 17.6 Jérémie 24.9 Esaïe 22.12 Esaïe 20.2
12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki.
Deutéronome 16.18 Psaumes 35.15-35.16 Matthieu 27.41-27.42 Daniel 5.2-5.4 Daniel 5.23
13 Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.
Esaïe 49.8 2 Corinthiens 6.2 Genèse 24.27 Matthieu 26.36-26.46 Psaumes 51.1
14 Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji.
Psaumes 144.7 Psaumes 69.1-69.2 Jérémie 38.6-38.13 Lamentations 3.55 Psaumes 35.19
15 Mkondo usinigharikishe, wala vilindi visinimeze, Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu.
Matthieu 12.40 Actes 2.31 Actes 2.24 Psaumes 124.4-124.5 Psaumes 16.10
16 Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa kadiri ya rehema zako unielekee.
Psaumes 63.3 Psaumes 25.16 Psaumes 109.21 Psaumes 51.1 Psaumes 36.7
17 Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi.
Psaumes 27.9 Psaumes 102.2 Psaumes 13.1 Matthieu 27.46 Psaumes 70.1
18 Uikaribie nafsi yangu, uikomboe, Kwa sababu ya adui zangu unifidie.
Psaumes 22.1 Job 6.23 Psaumes 49.15 Psaumes 111.9 Deutéronome 32.27
19 Wewe umejua kulaumiwa kwangu, Na kuaibika na kufedheheka kwangu, Mbele zako Wewe wako watesi wangu wote.
Hébreux 12.2 1 Pierre 2.23 Esaïe 53.3 Psaumes 2.2-2.4 Jean 8.49
20 Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu.
Job 16.2 Esaïe 63.5 Psaumes 142.4 Marc 14.50 Matthieu 26.37-26.38
21 Wakanipa uchungu kuwa chakula changu; Nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki.
Matthieu 27.34 Marc 15.23 Matthieu 27.48 Luc 23.36 Marc 15.36
22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; Naam, wakiwa salama na iwe tanzi.
Romains 11.8-11.10 1 Pierre 2.8 1 Thessaloniciens 5.3 Malachie 2.2 Proverbes 1.32
23 Macho yao yatiwe giza wasione, Na viuno vyao uvitetemeshe daima.
Daniel 5.6 Romains 11.10 Esaïe 6.9-6.10 Jérémie 30.6 Jean 12.39-12.40
24 Uimwage ghadhabu yako juu yao, Na ukali wa hasira yako uwapate.
Psaumes 79.6 Osée 5.10 Deutéronome 28.15-28.68 Exode 15.15 Deutéronome 32.20-32.26
25 Matuo yao na yawe ukiwa, Pasiwe na mtu wa kukaa hemani mwao.
Actes 1.20 Matthieu 23.38 Jérémie 7.12-7.14 Luc 13.35 Esaïe 6.11
26 Maana wanamwudhi mtu uliyempiga Wewe, Wanasimulia maumivu ya hao uliowatia jeraha.
Esaïe 53.4 Zacharie 1.15 Zacharie 13.7 Esaïe 53.10 2 Chroniques 28.9
27 Uwaongezee uovu juu ya uovu, Wala wasiingie katika haki yako.
Esaïe 26.10 Néhémie 4.5 Romains 1.28 Exode 8.15 Matthieu 27.4-27.5
28 Na wafutwe katika chuo cha uhai, Wala pamoja na wenye haki wasiandikwe.
Luc 10.20 Philippiens 4.3 Exode 32.32-32.33 Ezéchiel 13.9 Apocalypse 3.5
29 Nami niliye maskini na mtu wa huzuni, Mungu, wokovu wako utaniinua.
Psaumes 59.1 2 Corinthiens 8.9 Psaumes 70.5 Psaumes 109.31 Psaumes 109.22
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, Nami nitamtukuza kwa shukrani.
Psaumes 28.7 Psaumes 34.3 Psaumes 118.28-118.29 Psaumes 50.14 Psaumes 118.21
31 Nayo yatampendeza Bwana kuliko ng’ombe, Au ndama mwenye pembe na kwato.
Psaumes 50.13-50.14 Ephésiens 5.19-5.20 Hébreux 13.15 Psaumes 50.23 1 Pierre 2.5
32 Walioonewa watakapoona watafurahi; Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe.
Psaumes 22.26 Psaumes 34.2 Psaumes 25.9 Psaumes 22.29 Esaïe 61.1-61.3
33 Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji, Wala hawadharau wafungwa wake.
Psaumes 68.6 Psaumes 10.17 Psaumes 72.12-72.14 Psaumes 146.7 Psaumes 102.17
34 Mbingu na nchi zimsifu, Bahari na vyote viendavyo ndani yake.
Psaumes 96.11 Esaïe 49.13 Esaïe 55.12 Genèse 1.20 Psaumes 148.1-148.14
35 Maana Mungu ataiokoa Sayuni, na kuijenga miji ya Yuda, Na watu watakaa ndani yake na kuimiliki.
Psaumes 51.18 Esaïe 44.26 Esaïe 46.13 Jérémie 33.10-33.11 Ezéchiel 36.35-36.36
36 Wazao wa watumishi wake watairithi, Nao walipendao jina lake watakaa humo.
Psaumes 102.28 Psaumes 37.29 Actes 2.39 Psaumes 90.16-90.17 Jacques 1.12

Cette Bible est dans le domaine public.