Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 50.14
Bible en Swahili de l’est


Les sacrifices agréables à Dieu

1 Mungu, Mungu Bwana, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hata machweo yake.
Psaumes 113.3 Josué 22.22 Matthieu 25.32 Psaumes 49.1-49.2 Esaïe 9.6
2 Tokea Sayuni, ukamilifu wa uzuri, Mungu amemulika.
Psaumes 48.2 Psaumes 80.1 Deutéronome 33.2 Lamentations 2.15 Apocalypse 1.16
3 Mungu wetu atakuja wala hatanyamaza, Moto utakula mbele zake, na tufani yavuma sana ikimzunguka pande zote.
Daniel 7.10 Nombres 16.35 Lévitique 10.2 Habakuk 3.5 2 Thessaloniciens 1.8-1.9
4 Ataziita mbingu zilizo juu, Na nchi pia awahukumu watu wake.
Esaïe 1.2 Deutéronome 31.28 Deutéronome 32.1 Jean 5.22-5.23 Michée 6.1-6.2
5 Nikusanyieni wacha Mungu wangu Waliofanya agano nami kwa dhabihu.
Hébreux 13.20 Hébreux 12.24 Matthieu 26.28 1 Thessaloniciens 3.13 Hébreux 9.10-9.23
6 Na mbingu zitatangaza haki yake, Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu.
Psaumes 75.7 Psaumes 97.6 Apocalypse 19.2 Psaumes 89.5 2 Corinthiens 5.10
7 Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena, Mimi nitakushuhudia, Israeli; Mimi ndimi niliye MUNGU, Mungu wako.
Psaumes 81.8 Exode 20.2 Jérémie 2.4-2.5 Deutéronome 31.19-31.21 Deutéronome 26.17-26.18
8 Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako, Na kafara zako ziko mbele zangu daima.
Hébreux 10.4-10.10 Psaumes 40.6-40.8 Osée 6.6 Psaumes 51.16 Esaïe 1.11-1.31
9 Sitatwaa ng’ombe katika nyumba yako, Wala beberu katika mazizi yako.
Michée 6.6-6.8 Esaïe 43.23-43.24 Hébreux 10.4-10.6 Psaumes 69.31 Actes 17.25
10 Maana kila hayawani ni wangu, Na makundi juu ya milima elfu.
Job 40.15-40.24 Genèse 8.17 Genèse 9.2-9.3 Psaumes 104.14 Psaumes 104.24-104.25
11 Nawajua ndege wote wa milima, Na wanyama wote wa mashamba ni wangu
Genèse 1.20-1.22 Matthieu 6.26 Job 39.13-39.18 Luc 12.24 Matthieu 10.29-10.31
12 Kama ningekuwa na njaa singekuambia, Maana ulimwengu ni wangu, navyo viujazavyo.
Exode 19.5 Deutéronome 10.14 1 Corinthiens 10.26-10.28 Psaumes 104.24 Genèse 1.28-1.30
13 Je! Nile nyama ya mafahali! Au ninywe damu ya mbuzi!
14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.
Deutéronome 23.21 Hébreux 13.15 Psaumes 56.12 Psaumes 107.21-107.22 Psaumes 76.11
15 Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.
Psaumes 107.28 Psaumes 91.15 Zacharie 13.9 Psaumes 81.7 Psaumes 107.19
16 Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia, Una nini wewe kuitangaza sheria yangu, Na kuliweka agano langu kinywani mwako?
Psaumes 78.36-78.38 Esaïe 55.6-55.7 2 Pierre 2.15 Ezéchiel 18.27 Actes 19.13-19.16
17 Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Néhémie 9.26 Proverbes 12.1 Proverbes 1.7 1 Rois 14.9 2 Timothée 4.3-4.4
18 Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, Ukashirikiana na wazinzi.
1 Timothée 5.22 Romains 1.32 Lévitique 20.10 Esaïe 5.23 Hébreux 13.4
19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako watunga hila.
Psaumes 10.7 Psaumes 64.3-64.5 Jacques 3.5-3.9 Psaumes 55.12 Psaumes 36.3-36.4
20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.
Matthieu 10.21 1 Timothée 3.11 Apocalypse 12.10 Luc 22.65 Psaumes 31.18
21 Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza; Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe. Walakini nitakukemea; Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.
Psaumes 90.8 Esaïe 57.11 Ecclésiaste 8.11-8.12 Romains 2.4-2.5 Proverbes 29.1
22 Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane mwenye kuwaponya.
Psaumes 7.2 Psaumes 9.17 Job 8.13 Psaumes 10.4 2 Samuel 22.42
23 Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.
Psaumes 91.16 Jacques 3.13 Philippiens 1.27 Psaumes 25.14 Actes 13.26

Cette Bible est dans le domaine public.