Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 140.6
Bible en Swahili de l’est


Prière pour être protégé des persécuteurs

1 Ee Bwana, uniokoe na mtu mbaya, Unihifadhi na mtu wa jeuri.
Psaumes 18.48 Psaumes 71.4 Psaumes 17.13 Psaumes 140.4 Habakuk 1.2-1.3
2 Waliowaza mabaya mioyoni mwao, Kila siku huondokesha vita.
Psaumes 56.6 Psaumes 36.4 Psaumes 21.11 Proverbes 12.20 Psaumes 64.5-64.6
3 Wamenoa ndimi zao kama nyoka, Sumu ya fira i chini ya midomo yao.
Psaumes 58.4 Psaumes 57.4 Psaumes 64.3-64.4 Jérémie 9.5 Jérémie 9.3
4 Ee Bwana, unilinde na mikono ya mtu asiye haki; Unihifadhi na mtu wa jeuri; Waliowaza kuzipotosha hatua zangu.
Psaumes 71.4 Psaumes 36.11 Psaumes 17.8-17.9 Proverbes 18.5 Psaumes 55.1-55.3
5 Wenye kiburi wamenifichia mtego na kamba; Wametandika wavu kando ya njia; Wameniwekea matanzi.
Psaumes 35.7 Psaumes 142.3 Psaumes 57.6 Jérémie 18.22 Psaumes 36.11
6 Nimemwambia Bwana, Ndiwe Mungu wangu; Ee Bwana, uisikie sauti ya dua zangu.
Psaumes 16.2 Psaumes 142.5 Psaumes 31.14 Psaumes 116.1 Psaumes 64.1
7 Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu, Umenifunika kichwa changu siku ya vita.
Psaumes 144.10 2 Samuel 8.6 Psaumes 27.1 Esaïe 12.2 1 Samuel 17.36-17.37
8 Ee Bwana, usimpe asiye haki tamaa zake, Usiifanikishe hila yake, wasije wakajiinua.
Psaumes 27.12 Job 5.12-5.13 Psaumes 10.2-10.3 Psaumes 94.20-94.21 2 Samuel 15.31
9 Nao wainuapo vichwa watu wanaonizunguka, Madhara ya midomo yao yawafunike.
Psaumes 7.16 Proverbes 18.7 Proverbes 12.13 Matthieu 27.25 Psaumes 64.8
10 Makaa ya moto yawaangukie, watupwe motoni, Na katika mashimo, wasipate kusimama tena.
Psaumes 11.6 Psaumes 21.9 Proverbes 28.17 Psaumes 120.4 Genèse 19.24
11 Msingiziaji hatawekwa imara katika nchi, Mtu wa jeuri, uovu humwinda kumwangamiza.
Psaumes 34.21 Psaumes 9.16 Proverbes 13.21 Proverbes 6.17 Proverbes 12.13
12 Najua ya kuwa Bwana atamfanyia mnyonge hukumu, Na wahitaji haki yao.
Psaumes 9.4 1 Rois 8.45 1 Rois 8.49 Psaumes 35.10 Psaumes 72.4
13 Hakika wenye haki watalishukuru jina lako, Wenye adili watakaa mahali ulipo Wewe.
Psaumes 16.11 Psaumes 11.7 Esaïe 3.10 1 Thessaloniciens 4.17 Psaumes 97.12

Cette Bible est dans le domaine public.