Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 119.12
Bible en Swahili de l’est


La Parole de Dieu

1 Heri walio kamili njia zao, Waendao katika sheria ya Bwana.
Psaumes 128.1 Ezéchiel 11.20 Luc 1.6 Jacques 1.25 Proverbes 11.20
2 Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.
Jean 14.23 Ezéchiel 36.27 Psaumes 119.10 Psaumes 119.22 Deutéronome 4.29
3 Naam, hawakutenda ubatili, Wamekwenda katika njia zake.
1 Jean 3.9 1 Jean 5.18
4 Wewe umetuamuru mausia yako, Ili sisi tuyatii sana.
1 Jean 5.3 Deutéronome 30.16 Deutéronome 5.29-5.33 Jérémie 7.23 Deutéronome 11.13
5 Ningependa njia zangu ziwe thabiti, Nizitii amri zako.
2 Thessaloniciens 3.5 Psaumes 51.10 Romains 7.22-7.24 Psaumes 119.32 Psaumes 119.44-119.45
6 Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote.
Psaumes 119.80 1 Jean 2.28 Job 22.26 Jacques 2.10 Daniel 12.2-12.3
7 Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako
Psaumes 119.12 Psaumes 119.33-119.34 1 Chroniques 29.13-29.17 Psaumes 119.171 Psaumes 25.8-25.10
8 Nitazitii amri zako, Usiniache kabisa
Psaumes 51.11 Josué 24.15 Psaumes 119.106 Psaumes 71.18 Philippiens 4.13
9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.
Jacques 1.21-1.25 2 Timothée 2.22 Psaumes 25.7 Josué 1.7 Psaumes 34.11
10 Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
2 Chroniques 15.15 Psaumes 119.118 1 Samuel 7.3 Psaumes 23.3 Psaumes 119.21
11 Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
Psaumes 37.31 Psaumes 40.8 Jérémie 15.16 Psaumes 119.97 Colossiens 3.16
12 Ee Bwana, umehimidiwa, Unifundishe amri zako.
Psaumes 119.124 Psaumes 119.108 Psaumes 119.64 Jean 14.26 1 Jean 2.27
13 Kwa midomo yangu nimezisimulia Hukumu zote za kinywa chako.
Psaumes 71.15-71.18 Psaumes 40.9-40.10 Psaumes 118.17 Psaumes 119.172 Actes 4.20
14 Nimeifurahia njia ya shuhuda zako Kana kwamba ni mali mengi.
Psaumes 119.111 Psaumes 119.162 Jérémie 15.16 Psaumes 119.77 Job 23.12
15 Nitayatafakari mausia yako, Nami nitaziangalia njia zako.
Psaumes 1.2 Psaumes 119.23 Psaumes 119.48 Psaumes 119.97 Psaumes 119.148
16 Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako.
Hébreux 10.16-10.17 Psaumes 119.92-119.93 Psaumes 119.35 Psaumes 119.47 Psaumes 119.70
17 Umtendee mtumishi wako ukarimu, Nipate kuishi, nami nitalitii neno lako.
Psaumes 13.6 Psaumes 116.7 1 Jean 2.29 Psaumes 119.132 Psaumes 119.65
18 Unifumbue macho yangu niyatazame Maajabu yatokayo katika sheria yako.
Ephésiens 1.17-1.18 Esaïe 29.18 Actes 26.18 Esaïe 32.3 Hébreux 10.1
19 Mimi ni mgeni katika nchi, Usinifiche maagizo yako.
1 Chroniques 29.15 2 Corinthiens 5.6 Genèse 47.9 Esaïe 63.17 Psaumes 39.12
20 Roho yangu imepondeka kwa kutamani Hukumu zako kila wakati.
Psaumes 63.1 Psaumes 84.2 Psaumes 119.131 Psaumes 42.1-42.2 Psaumes 119.40
21 Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako.
Psaumes 119.10 Psaumes 119.118 Psaumes 119.78 Deutéronome 28.15 Exode 10.3
22 Uniondolee laumu na dharau, Kwa maana nimezishika shuhuda zako.
Psaumes 39.8 Psaumes 119.39 1 Pierre 2.20 Psaumes 37.3 1 Samuel 25.10
23 Wakuu nao waliketi wakaninena, Lakini mtumishi wako atazitafakari amri zako.
1 Samuel 22.7-22.13 1 Samuel 20.31 Psaumes 2.1-2.2 Luc 23.10-23.11 Luc 22.66
24 Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.
Psaumes 119.16 Psaumes 119.77 Psaumes 119.97-119.100 Esaïe 8.20 Psaumes 119.162
25 Nafsi yangu imeambatana na mavumbi, Unihuishe sawasawa na neno lako.
Psaumes 44.25 Psaumes 119.159 Psaumes 119.93 Psaumes 119.149 Psaumes 143.11
26 Nalizisimulia njia zangu ukanijibu, Unifundishe amri zako.
Psaumes 86.11 Psaumes 25.4 Psaumes 27.11 Psaumes 143.8-143.10 Psaumes 25.8-25.9
27 Unifahamishe njia ya mausia yako, Nami nitayatafakari maajabu yako.
Psaumes 105.2 Apocalypse 15.3 Psaumes 145.5-145.6 Josué 4.6-4.7 Psaumes 78.4
28 Nafsi yangu imeyeyuka kwa uzito, Unitie nguvu sawasawa na neno lako.
Psaumes 107.26 Psaumes 22.14 Josué 2.24 Deutéronome 33.25 Psaumes 27.14
29 Uniondolee njia ya uongo, Unineemeshe kwa sheria yako.
Jérémie 31.33-31.34 Hébreux 8.10-8.11 Jonas 2.8 Apocalypse 22.15 Psaumes 141.3-141.4
30 Nimeichagua njia ya uaminifu, Na kuziweka hukumu zako mbele yangu.
2 Jean 1.4 Luc 10.42 Psaumes 119.111 Deutéronome 11.18-11.20 Psaumes 119.173
31 Nimeambatana na shuhuda zako, Ee Bwana, usiniaibishe.
Jean 8.31 Actes 11.23 Deutéronome 10.20 Deutéronome 11.22 Psaumes 119.115
32 Nitakwenda mbio katika njia ya maagizo yako, Utakaponikunjua moyo wangu.
1 Rois 4.29 Jean 8.32 1 Corinthiens 9.24-9.26 Esaïe 60.5 2 Corinthiens 6.11
33 Ee Bwana, unifundishe njia ya amri zako, Nami nitaishika hata mwisho.
1 Jean 2.27 Psaumes 119.12 Philippiens 1.6 Apocalypse 2.26 Jean 6.45
34 Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, Naam, nitaitii kwa moyo wangu wote.
Matthieu 7.24 Psaumes 119.73 Proverbes 2.5-2.6 Jacques 1.5 Psaumes 119.69
35 Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako, Kwa maana nimependezwa nayo.
Proverbes 8.20 Romains 7.22 Psaumes 119.27 Psaumes 119.36 Esaïe 2.3
36 Unielekeze moyo wangu na shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa.
Luc 12.15 1 Rois 8.58 Marc 7.21-7.22 Hébreux 13.5 Ezéchiel 33.31
37 Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia yako.
Esaïe 33.15 Proverbes 4.25 Nombres 15.39 Psaumes 119.25 Proverbes 23.5
38 Umthibitishie mtumishi wako ahadi yako, Inayohusu kicho chako.
Jérémie 32.39-32.41 2 Corinthiens 1.20 Psaumes 103.13 Psaumes 103.11 Psaumes 119.49
39 Uniondolee laumu niiogopayo, Maana hukumu zako ni njema.
Psaumes 119.22 Tite 2.8 1 Timothée 3.7 Psaumes 57.3 2 Samuel 12.14
40 Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.
Psaumes 119.20 Philippiens 3.13-3.14 Jean 10.10 2 Corinthiens 7.1 Psaumes 119.107
41 Ee Bwana, fadhili zako zinifikie na mimi, Naam, wokovu wako sawasawa na ahadi yako.
Psaumes 119.58 Psaumes 119.76-119.77 Luc 2.28-2.32 Psaumes 106.4-106.5 Psaumes 119.132
42 Nami nitamjibu neno anilaumuye, Kwa maana nalitumainia neno lako.
Actes 27.25 Psaumes 56.4 1 Chroniques 28.3-28.6 Proverbes 27.11 Matthieu 27.40-27.43
43 Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe, Maana nimezingojea hukumu zako.
Psaumes 7.6-7.9 Psaumes 119.120 1 Pierre 2.23 Psaumes 119.52 Psaumes 50.16
44 Nami nitaitii sheria yako daima, Naam, milele na milele.
Apocalypse 7.15 Psaumes 119.33-119.34 Apocalypse 22.11
45 Nami nitakwenda panapo nafasi, Kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
Proverbes 4.12 Psaumes 119.94 2 Pierre 2.19 Jacques 1.25 Psaumes 119.133
46 Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu.
Actes 26.1-26.2 Matthieu 10.18-10.19 Psaumes 138.1 Daniel 4.1-4.3 Actes 26.24-26.29
47 Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, Ambayo nimeyapenda.
Psaumes 119.127 Psaumes 119.97 Psaumes 119.48 Psaumes 119.16 Job 23.11-23.12
48 Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, Nami nitazitafakari amri zako.
Psaumes 119.15 Psaumes 1.2 Jean 13.17 Psaumes 10.12 Ezéchiel 44.12
49 Likumbuke neno ulilomwambia mtumishi wako, Kwa sababu umenitumainisha.
Psaumes 71.14 2 Samuel 7.25 Psaumes 106.45 Psaumes 119.74 Psaumes 119.81
50 Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imenihuisha.
Romains 15.4 Psaumes 28.7 Psaumes 42.8 Psaumes 42.11 Hébreux 6.17-6.19
51 Wenye kiburi wamenidharau mno, Sikujiepusha na sheria zako.
Job 23.11 Psaumes 44.18 Jérémie 20.7 Psaumes 119.157 Actes 20.23-20.24
52 Nimezikumbuka hukumu zako za kale, Ee Bwana, nikajifariji.
Deutéronome 1.35-1.36 Psaumes 103.18 Psaumes 105.5 Deutéronome 4.3-4.4 Psaumes 77.5
53 Ghadhabu imenishika kwa sababu ya wasio haki, Waiachao sheria yako.
Esdras 9.3 Psaumes 119.158 Psaumes 119.136 Habakuk 3.16 Philippiens 3.18
54 Amri zako zimekuwa nyimbo zangu, Katika nyumba ya ugeni wangu.
Genèse 47.9 Psaumes 10.1 Psaumes 89.1 Hébreux 11.13-11.16
55 Wakati wa usiku nimelikumbuka jina lako, Ee Bwana, nikaitii sheria yako.
Psaumes 42.8 Psaumes 63.6 Esaïe 26.9 Actes 16.25 Genèse 32.24-32.28
56 Hayo ndiyo niliyokuwa nayo, Kwa sababu nimeyashika mausia yako.
Psaumes 18.18-18.22 Psaumes 119.165 1 Jean 3.19-3.24
57 Bwana ndiye aliye fungu langu, Nimesema kwamba nitayatii maneno yake.
Psaumes 16.5 Lamentations 3.24 Josué 24.24-24.27 Psaumes 66.14 Psaumes 142.5
58 Nimekuomba radhi kwa moyo wangu wote, Unifadhili sawasawa na ahadi yako.
Psaumes 119.41 Psaumes 119.10 Psaumes 86.1-86.3 Psaumes 119.65 Matthieu 24.35
59 Nalizitafakari njia zangu, Na miguu yangu nalizielekezea shuhuda zako.
Ezéchiel 18.30 Jérémie 31.18-31.19 Ezéchiel 18.28 Aggée 1.7 Jérémie 8.4-8.6
60 Nalifanya haraka wala sikukawia, Kuyatii maagizo yako.
Psaumes 95.7-95.8 Galates 1.16 Ezéchiel 10.6-10.8 Ecclésiaste 9.10 Proverbes 27.1
61 Kamba za wasio haki zimenifunga, Sikuisahau sheria yako.
Psaumes 119.176 Proverbes 24.29 Job 1.17 Osée 6.9 Psaumes 140.5
62 Katikati ya usiku nitaamka nikushukuru, Kwa sababu ya hukumu zako za haki.
Deutéronome 4.8 Psaumes 119.7 Psaumes 119.75 Psaumes 19.9 Psaumes 119.164
63 Mimi ni mwenzao watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yako.
Psaumes 101.6 Proverbes 13.20 2 Corinthiens 6.14-6.17 Psaumes 119.79 Psaumes 119.115
64 Bwana, dunia imejaa fadhili zako, Unifundishe amri zako.
Psaumes 33.5 Psaumes 119.12 Esaïe 48.17-48.18 Psaumes 119.26 Esaïe 2.3
65 Umemtendea mema mtumishi wako, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
Psaumes 13.6 Psaumes 23.5-23.6 Psaumes 16.5-16.6 Psaumes 18.35 1 Chroniques 29.14
66 Unifundishe akili na maarifa, Maana nimeyaamini maagizo yako.
Philippiens 1.9 Jacques 3.13-3.18 Psaumes 119.160 Psaumes 72.1-72.2 Néhémie 9.13-9.14
67 Kabla sijateswa mimi nalipotea, Lakini sasa nimelitii neno lako.
Jérémie 31.18-31.19 Psaumes 119.71 Psaumes 119.75 Proverbes 1.32 2 Samuel 11.2-11.27
68 Wewe U mwema na mtenda mema, Unifundishe amri zako.
Psaumes 106.1 Psaumes 107.1 Psaumes 119.12 Matthieu 19.17 Psaumes 86.5
69 Wenye kiburi wamenizulia uongo, Kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako.
Job 13.4 Jérémie 43.2-43.3 Psaumes 119.58 Matthieu 6.24 Actes 24.13
70 Mioyo yao imenenepa kama shahamu, Mimi nimeifurahia sheria yako.
Esaïe 6.10 Actes 28.27 Psaumes 17.10 Psaumes 119.16 Psaumes 73.7
71 Ilikuwa vema kwangu kuwa naliteswa, Nipate kujifunza amri zako.
Psaumes 94.12-94.13 Psaumes 119.67 1 Corinthiens 11.32 Hébreux 12.10-12.11 Esaïe 27.9
72 Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.
Psaumes 19.10 Proverbes 8.10-8.11 Psaumes 119.162 Psaumes 119.127 Proverbes 16.16
73 Mikono yako ilinifanya ikanitengeneza, Unifahamishe nikajifunze maagizo yako.
Psaumes 139.14-139.16 Psaumes 138.8 Psaumes 111.10 Psaumes 119.125 Psaumes 100.3
74 Wakuchao na wanione na kufurahi, Kwa sababu nimelingojea neno lako.
Genèse 32.11-32.12 Psaumes 34.2-34.6 Psaumes 66.16 Psaumes 119.42 Malachie 3.16
75 Najua ya kuwa hukumu zako ni za haki, Ee Bwana, na kwa uaminifu umenitesa.
Apocalypse 3.19 Hébreux 12.10-12.11 Psaumes 119.7 Jérémie 12.1 Psaumes 25.10
76 Nakuomba, fadhili zako ziwe faraja kwangu, Sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
2 Corinthiens 1.3-1.5 Psaumes 106.4-106.5 Psaumes 86.5
77 Rehema zako zinijie nipate kuishi, Maana sheria yako ni furaha yangu.
Psaumes 119.41 Psaumes 119.24 Psaumes 119.174 Hébreux 8.10-8.12 Psaumes 51.1-51.3
78 Wenye kiburi waaibike, maana wamenidhulumu kwa uongo, Mimi nitayatafakari mausia yako.
Psaumes 119.21 1 Pierre 2.20 Jean 15.25 Psaumes 69.4 Psaumes 35.7
79 Wakuchao na wanirudie, Nao watazijua shuhuda zako.
Psaumes 119.63 Psaumes 119.74 Psaumes 7.7 Psaumes 142.7
80 Moyo wangu na uwe mkamilifu katika amri zako, Nisije mimi nikaaibika.
Deutéronome 26.16 Psaumes 119.6 Jean 1.47 Proverbes 4.23 2 Chroniques 12.14
81 Nafsi yangu imefifia kwa kuutamani wokovu wako, Nimelingojea neno lako.
Psaumes 84.2 Apocalypse 3.15-3.16 Cantique 5.8 Psaumes 42.1-42.2 Psaumes 119.77
82 Macho yangu yamefifia kwa kuitazamia ahadi yako, Nisemapo, Lini utakaponifariji?
Psaumes 69.3 Psaumes 119.123 Lamentations 2.11 Psaumes 90.13-90.15 Deutéronome 28.32
83 Maana nimekuwa kama kiriba katika moshi, Sikuzisahau amri zako.
Job 30.30 Psaumes 119.61 Psaumes 119.16 Psaumes 119.176 Psaumes 102.3-102.4
84 Siku za mtumishi wako ni ngapi, Lini utakapowahukumu wale wanaonifuatia?
Psaumes 7.6 Apocalypse 6.10-6.11 Job 7.6-7.8 Psaumes 39.4-39.5 Psaumes 89.47-89.48
85 Wenye kiburi wamenichimbia mashimo, Ambao hawaifuati sheria yako.
Psaumes 35.7 Psaumes 7.15 Jérémie 18.20 Psaumes 119.78 Psaumes 58.1-58.2
86 Maagizo yako yote ni amini, Wananifuatia bure, unisaidie.
Psaumes 119.78 Psaumes 35.19 Psaumes 109.26 Psaumes 119.138 Romains 7.12
87 Walikuwa karibu na kunikomesha katika nchi, Lakini sikuyaacha mausia yako.
Matthieu 10.28 1 Samuel 20.3 1 Samuel 26.9 1 Samuel 26.24 Esaïe 58.2
88 Unihuishe kwa fadhili zako, Nami nitazishika shuhuda za kinywa chako.
Psaumes 119.25 Psaumes 78.5 Psaumes 25.10 Psaumes 132.12 Psaumes 119.159
89 Ee Bwana, neno lako lasimama Imara mbinguni hata milele.
1 Pierre 1.25 Matthieu 5.18 Psaumes 119.160 Psaumes 89.2 Matthieu 24.34-24.35
90 Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa.
Psaumes 148.6 Ecclésiaste 1.4 Psaumes 36.5 Psaumes 89.1-89.2 Michée 7.20
91 Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, Maana vitu vyote ni watumishi wako.
Jérémie 33.25 Esaïe 48.13 Deutéronome 4.19 Psaumes 148.5-148.6 Josué 10.12-10.13
92 Kama sheria yako isingalikuwa furaha yangu, Hapo ningalipotea katika taabu zangu.
Psaumes 27.13 Romains 15.4 Proverbes 6.22-6.23 Psaumes 119.143 Psaumes 119.24
93 Hata milele sitayasahau maagizo yako, Maana kwa hayo umenihuisha.
Psaumes 119.16 Jean 6.63 1 Pierre 1.23 Psaumes 119.50
94 Mimi ni wako, uniokoe, Kwa maana nimejifunza mausia yako.
Josué 10.4-10.6 Esaïe 44.5 Actes 27.23-27.24 Esaïe 64.8-64.10 Psaumes 119.173
95 Wasio haki wameniotea ili kunipoteza, Nitazitafakari shuhuda zako.
2 Samuel 17.1-17.4 Psaumes 119.111 1 Samuel 23.20-23.23 Psaumes 10.8-10.10 Psaumes 119.31
96 Nimeona ukamilifu wote kuwa na mwisho, Bali agizo lako ni pana mno.
Hébreux 4.12-4.13 2 Samuel 18.17 1 Samuel 17.49-17.51 Ecclésiaste 2.11 Psaumes 39.5-39.6
97 Sheria yako naipenda mno ajabu, Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.
Psaumes 1.2 Psaumes 119.127 Psaumes 119.48 Josué 1.8 Psaumes 119.159
98 Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu, Kwa maana ninayo sikuzote.
Deutéronome 4.6 Psaumes 119.11 1 Samuel 18.5 1 Samuel 18.14 Psaumes 119.104-119.105
99 Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.
Deutéronome 4.6-4.8 Jérémie 8.8-8.9 2 Chroniques 30.22 2 Chroniques 29.15-29.36 Matthieu 23.24-23.36
100 Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.
Job 12.12 Job 32.7-32.10 Job 15.9-15.10 Job 28.28 Jérémie 8.8-8.9
101 Nimeiepusha miguu yangu na kila njia mbaya, Ili nilitii neno lako.
Proverbes 1.15 1 Pierre 2.1-2.2 Psaumes 119.59-119.60 Esaïe 55.7 Psaumes 18.23
102 Sikujiepusha na hukumu zako, Maana Wewe mwenyewe umenifundisha.
Psaumes 18.21 Proverbes 5.7 1 Jean 2.19 Ephésiens 4.20-4.24 Jérémie 32.40
103 Mausia yako ni matamu sana kwangu, Kupita asali kinywani mwangu.
Proverbes 8.11 Proverbes 24.13-24.14 Psaumes 19.10 Psaumes 63.5 Cantique 5.1
104 Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.
Psaumes 119.128 Proverbes 8.13 Psaumes 101.3 Psaumes 36.4 Psaumes 119.98
105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
Proverbes 6.23 Psaumes 43.3 2 Pierre 1.19 Psaumes 18.28 Psaumes 19.8
106 Nimeapa nami nitaifikiliza, Kuzishika hukumu za haki yako.
Néhémie 10.29 2 Rois 23.3 2 Chroniques 15.13-15.14 Psaumes 119.115 Matthieu 5.33
107 Nimeteswa mno; Ee Bwana, unihuishe sawasawa na neno lako.
Psaumes 119.25 Psaumes 119.88 Psaumes 22.14-22.18 Psaumes 143.11 Psaumes 6.1
108 Ee Bwana, uziridhie sadaka za kinywa changu, Na kunifundisha hukumu zako.
Osée 14.2 Hébreux 13.15 Psaumes 119.12 Nombres 29.39 Psaumes 119.26
109 Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima, Lakini sheria yako sikuisahau.
Juges 12.3 Job 13.14 Psaumes 119.117 1 Corinthiens 15.31 1 Samuel 20.3
110 Watendao uovu wamenitegea mtego, Lakini sikuikosa njia ya mausia yako.
Psaumes 141.9 Psaumes 140.5 Psaumes 10.8-10.18 Proverbes 1.11-1.12 Psaumes 119.10
111 Shuhuda zako nimezifanya urithi wa milele, Maana ndizo changamko la moyo wangu.
Deutéronome 33.4 Psaumes 19.8 Psaumes 119.92 Psaumes 119.14 Psaumes 119.127
112 Nimeuelekeza moyo wangu nizitende amri zako, Daima, naam, hata milele.
Psaumes 119.33 Psaumes 119.36 2 Chroniques 19.3 Psaumes 141.4 Apocalypse 2.10
113 Watu wa kusita-sita nawachukia, Lakini sheria yako naipenda.
2 Corinthiens 10.5 Jacques 1.8 Jérémie 4.14 Marc 7.21 Psaumes 94.11
114 Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea.
Psaumes 91.1-91.2 Psaumes 32.7 Esaïe 32.2 Psaumes 3.3 Psaumes 119.81
115 Enyi watenda mabaya, ondokeni kwangu, Niyashike maagizo ya Mungu wangu.
Psaumes 6.8 Matthieu 7.23 1 Corinthiens 15.33 Psaumes 139.19 Psaumes 119.106
116 Unitegemeze sawasawa na ahadi yako, nikaishi, Wala usiniache niyaaibikie matumaini yangu.
Romains 5.5 Psaumes 25.2 Psaumes 37.17 Psaumes 37.24 Psaumes 94.18
117 Unisaidie nami nitakuwa salama, Nami nitaziangalia amri zako daima.
Psaumes 119.6 Psaumes 119.111-119.112 Psaumes 139.10 Jean 10.28-10.29 Psaumes 71.6
118 Umewakataa wote wazikosao amri zako, Kwa maana hila zao ni uongo.
Psaumes 119.10 Psaumes 119.21 Psaumes 119.29 Psaumes 95.10 Malachie 4.3
119 Wabaya wa nchi pia umewaondoa kama takataka, Ndiyo maana nimezipenda shuhuda zako.
Malachie 3.2-3.3 Jérémie 6.30 Psaumes 119.111 Matthieu 7.23 Matthieu 3.12
120 Mwili wangu unatetemeka kwa kukucha Wewe, Nami ninaziogopa hukumu zako.
Habakuk 3.16 1 Chroniques 24.30 2 Chroniques 34.27 Philippiens 2.12 1 Chroniques 24.16-24.17
121 Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea.
2 Samuel 8.15 Psaumes 57.3-57.4 Psaumes 7.3-7.5 Psaumes 75.2 Psaumes 18.20-18.24
122 Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema, Wenye kiburi wasinionee.
Job 17.3 Hébreux 7.22 Philémon 1.18-1.19 Esaïe 38.14 Proverbes 22.26-22.27
123 Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako, Na ahadi ya haki yako.
Psaumes 69.3 Psaumes 143.7 Lamentations 4.17 Psaumes 119.81-119.82 Psaumes 130.6
124 Kama zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako, Na amri zako unifundishe.
Psaumes 119.12 Psaumes 119.76-119.77 Psaumes 119.26 Psaumes 119.132 Daniel 9.18
125 Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe, Nipate kuzijua shuhuda zako.
Psaumes 116.16 2 Corinthiens 3.5-3.6 Psaumes 119.11 Jacques 1.5 Romains 6.22
126 Wakati umewadia Bwana atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako.
Malachie 2.8 Jérémie 8.8 Habakuk 1.4 Matthieu 15.6 Romains 4.14
127 Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi.
Psaumes 19.10 Matthieu 13.45-13.46 Proverbes 16.16 Proverbes 3.13-3.18 Proverbes 8.11
128 Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.
Psaumes 119.104 Romains 7.22 Psaumes 119.6 Romains 7.12 Psaumes 119.118
129 Shuhuda zako ni za ajabu, Ndiyo maana roho yangu imezishika.
Psaumes 139.6 Psaumes 119.146 Psaumes 119.31 Psaumes 119.2 Psaumes 119.18
130 Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, Na kumfahamisha mjinga.
Proverbes 6.23 Psaumes 19.7 Psaumes 119.105 Actes 26.18 2 Corinthiens 4.6
131 Nalifunua kinywa changu nikatweta, Maana naliyatamani maagizo yako.
Psaumes 42.1 Psaumes 119.20 Psaumes 119.162 Job 29.23 1 Pierre 2.2
132 Unigeukie, unirehemu mimi, Kama iwahusuvyo walipendao jina lako.
Psaumes 106.4 Esaïe 63.7-63.9 Exode 4.31 Psaumes 119.124 Psaumes 25.18
133 Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako, Uovu usije ukanimiliki.
Psaumes 19.13 Psaumes 17.5 Psaumes 119.116 Psaumes 32.8 Romains 6.12-6.14
134 Unikomboe na dhuluma ya mwanadamu, Nipate kuyashika mausia yako.
Psaumes 56.1-56.2 Psaumes 119.122 Luc 1.74-1.75 Ezéchiel 11.17-11.20 Actes 9.31
135 Umwangazie mtumishi wako uso wako, Na kunifundisha amri zako.
Psaumes 4.6 Psaumes 80.3 Psaumes 80.19 Psaumes 119.12 Psaumes 80.7
136 Macho yangu yachuruzika mito ya maji, Kwa sababu hawaitii sheria yako.
Ezéchiel 9.4 Jérémie 9.1 Jérémie 9.18 Jérémie 14.17 Psaumes 119.158
137 Ee Bwana, Wewe ndiwe mwenye haki, Na hukumu zako ni za adili.
Jérémie 12.1 Esdras 9.15 Daniel 9.7 Daniel 9.14 Néhémie 9.33
138 Umeziagiza shuhuda zako kwa haki, Na kwa uaminifu mwingi.
Psaumes 19.7-19.9 Psaumes 119.86 Psaumes 119.144 Deutéronome 4.8 Deutéronome 4.45
139 Juhudi yangu imeniangamiza, Maana watesi wangu wameyasahau maneno yako.
Jean 2.17 Psaumes 69.9 1 Rois 19.10 Matthieu 12.3-12.5 Matthieu 21.42
140 Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda.
Psaumes 12.6 Psaumes 19.8 1 Pierre 2.2 Psaumes 18.30 Romains 7.22
141 Mimi ni mdogo, nadharauliwa, Lakini siyasahau mausia yako.
Psaumes 22.6 Proverbes 3.1 2 Corinthiens 8.9 Psaumes 119.109 Luc 9.58
142 Haki yako ni haki ya milele, Na sheria yako ni kweli.
Psaumes 19.9 Psaumes 119.151 Psaumes 36.6 Psaumes 119.144 Daniel 9.24
143 Taabu na dhiki zimenipata, Maagizo yako ni furaha yangu.
Psaumes 18.4-18.5 Psaumes 88.3-88.18 Psaumes 130.1 Psaumes 119.47 Psaumes 119.77
144 Haki ya shuhuda zako ni ya milele, Unifahamishe, nami nitaishi.
Jérémie 4.22 Esaïe 27.11 Proverbes 10.21 Psaumes 119.169 Daniel 12.10
145 Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee Bwana, uitike; Nitazishika amri zako.
Psaumes 119.10 1 Samuel 1.15 Psaumes 61.1-61.2 Psaumes 119.106 Psaumes 119.44
146 Nimekuita Wewe, uniokoe, Nami nitazishika shuhuda zako.
Psaumes 119.134 Tite 3.4-3.8 Tite 2.14 Matthieu 1.21 Juges 10.15-10.16
147 Kutangulia mapambazuko naliomba msaada, Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
Psaumes 5.3 Psaumes 130.5-130.6 Marc 1.35 Psaumes 21.3 Psaumes 88.13
148 Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku, Ili kuitafakari ahadi yako.
Psaumes 63.6 Lamentations 2.19 Psaumes 63.1 Psaumes 119.62 Psaumes 139.17-139.18
149 Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
Psaumes 119.25 Psaumes 69.16 Psaumes 51.1 Psaumes 119.156 Psaumes 119.154
150 Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki, Wamekwenda mbali na sheria yako.
Psaumes 27.2 Ephésiens 2.13-2.14 Psaumes 50.17 Proverbes 28.9 Psaumes 22.16
151 Ee Bwana, Wewe U karibu, Na maagizo yako yote ni kweli.
Psaumes 145.18 Psaumes 119.142 Matthieu 1.23 Psaumes 46.1 Psaumes 75.1
152 Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako, Ya kuwa umeziweka zikae milele.
Luc 21.33 Psaumes 119.144 Psaumes 119.160 Psaumes 89.34-89.37 Ecclésiaste 3.14
153 Uyaangalie mateso yangu, uniokoe, Maana sikuisahau sheria yako.
Lamentations 5.1 Psaumes 119.16 Lamentations 2.20 Exode 3.7-3.8 Psaumes 9.13
154 Unitetee na kunikomboa, Unihuishe sawasawa na ahadi yako.
1 Samuel 24.15 Michée 7.9 Psaumes 35.1 Jérémie 51.36 Job 5.8
155 Wokovu u mbali na wasio haki, Kwa maana hawajifunzi amri zako.
Job 5.4 Esaïe 57.19 Job 21.14-21.15 Psaumes 10.4 Proverbes 1.7
156 Ee Bwana, rehema zako ni nyingi, Unihuishe sawasawa na hukumu zako.
2 Samuel 24.14 Esaïe 63.7 1 Chroniques 21.13 Psaumes 51.1 Psaumes 86.13
157 Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, Lakini sikujiepusha na shuhuda zako.
Psaumes 119.51 Job 23.11 Actes 20.23-20.24 Esaïe 42.4 Psaumes 56.2
158 Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa, Kwa sababu hawakulitii neno lako.
Psaumes 139.21 Psaumes 119.136 Psaumes 119.53 Ezéchiel 9.4 Marc 3.5
159 Uangalie niyapendavyo mausia yako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na fadhili zako.
Néhémie 5.19 Néhémie 13.22 2 Rois 20.3 Psaumes 119.153 Psaumes 119.97
160 Jumla ya neno lako ni kweli, Na kila hukumu ya haki yako ni ya milele.
Psaumes 119.142 Proverbes 30.5 Psaumes 119.144 Psaumes 119.152 Matthieu 5.18
161 Wakuu wameniudhi bure, Ila moyo wangu unayahofia maneno yako.
1 Samuel 26.18 Psaumes 119.23 1 Samuel 24.9-24.15 Genèse 39.9 2 Rois 22.19
162 Naifurahia ahadi yako, Kama apataye mateka mengi.
Psaumes 119.111 Jérémie 15.16 Psaumes 119.72 1 Samuel 30.16 Esaïe 9.3
163 Nimeuchukia uongo, umenikirihi, Sheria yako nimeipenda.
Psaumes 119.128 Proverbes 6.16-6.19 Psaumes 119.113 Romains 12.9 Amos 5.15
164 Mara saba kila siku nakusifu, Kwa sababu ya hukumu za haki yako.
Psaumes 119.62 Apocalypse 19.2 Psaumes 55.17 Psaumes 48.11 Psaumes 97.8
165 Wana amani nyingi waipendao sheria yako, Wala hawana la kuwakwaza.
Esaïe 32.17 1 Jean 2.10 Esaïe 57.21 Esaïe 8.13-8.15 Esaïe 26.3
166 Ee Bwana, nimeungojea wokovu wako, Na maagizo yako nimeyatenda.
Genèse 49.18 Psaumes 119.174 Psaumes 119.81 Psaumes 4.5 Psaumes 24.3-24.5
167 Nafsi yangu imezishika shuhuda zako, Nami nazipenda mno.
Hébreux 10.16 Romains 7.22 Psaumes 119.111 Psaumes 119.6-119.8 Psaumes 40.8
168 Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, Maana njia zangu zote zi mbele zako.
Proverbes 5.21 Psaumes 139.3 Job 34.21 Psaumes 44.20-44.21 Jérémie 23.24
169 Ee Bwana, kilio changu na kikukaribie, Unifahamishe sawasawa na neno lako.
Psaumes 18.6 Proverbes 2.3-2.5 Psaumes 119.144-119.145 1 Chroniques 22.12 Daniel 2.21
170 Dua yangu na ifike mbele zako, Uniponye sawasawa na ahadi yako.
Psaumes 119.41 Psaumes 89.20-89.25 Psaumes 31.2 2 Samuel 7.25 Psaumes 28.2
171 Midomo yangu na itoe sifa, Kwa kuwa unanifundisha mausia yako.
Psaumes 119.7 Psaumes 50.23 Psaumes 71.23-71.24 Psaumes 51.15 Psaumes 71.17
172 Ulimi wangu na uiimbe ahadi yako, Maana maagizo yako yote ni ya haki.
Psaumes 119.138 Romains 7.14 Ephésiens 4.29 Psaumes 40.9-40.10 Psaumes 37.30
173 Mkono wako na uwe tayari kunisaidia, Maana nimeyachagua mausia yako.
Josué 24.22 Luc 10.42 Psaumes 37.24 Psaumes 119.40 1 Rois 3.11-3.12
174 Ee Bwana, nimeutamani wokovu wako, Na sheria yako ndiyo furaha yangu.
Psaumes 119.24 Psaumes 119.16 Psaumes 119.81 Psaumes 119.111 Psaumes 119.166-119.167
175 Nafsi yangu na iishi, ipate kukusifu, Na hukumu zako zinisaidie.
Esaïe 55.3 Psaumes 51.14-51.15 1 Corinthiens 11.31-11.32 Psaumes 119.75 Esaïe 38.19
176 Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea; Umtafute mtumishi wako; Kwa maana sikuyasahau maagizo yako.
Ezéchiel 34.6 Esaïe 53.6 Psaumes 119.61 Matthieu 15.24 Luc 15.4-15.7

Cette Bible est dans le domaine public.