Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 1.5
Bible en Swahili de l’est


Premier livre

Deux hommes, deux destinées

1 Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Psaumes 26.4-26.5 Proverbes 4.14-4.15 Jérémie 15.17 Proverbes 13.20 Matthieu 7.13-7.14
2 Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
Josué 1.8 Psaumes 119.35 Psaumes 119.11 Psaumes 119.92 Psaumes 112.1
3 Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
Jérémie 17.8 Ezéchiel 47.12 Ezéchiel 19.10 Psaumes 92.14 Genèse 39.3
4 Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Job 21.18 Matthieu 3.12 Esaïe 17.13 Psaumes 35.5 Esaïe 29.5
5 Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.
Psaumes 5.5 Malachie 3.18 Luc 21.36 Matthieu 25.46 Matthieu 25.32
6 Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.
2 Timothée 2.19 Nahum 1.7 Jean 10.14 Psaumes 37.18-37.24 Proverbes 15.9

Cette Bible est dans le domaine public.