Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 30.28
Bible en Swahili de l’est


1 Lakini sasa hao walio wadogo wangu hunifanyia mzaha, Ambao baba zao niliwadharau hata kuwaweka na mbwa wa kundi langu.
Job 12.4 Psaumes 35.15-35.16 Psaumes 69.12 Tite 1.12 Job 19.13-19.19
2 Naam, uwezo wa mikono yao utanifaa nini? Watu ambao nguvu zao zimekoma.
3 Wamekonda kwa uhitaji na njaa; Huguguna nchi kavu, penye giza la ukiwa na uharibifu.
Job 24.5 Hébreux 11.38 Job 24.13-24.16
4 Hung’oa mboga ya chumvi kwenye kichaka; Na mizizi ya mretemu ni chakula chao.
2 Rois 4.38-4.39 Amos 7.14 Luc 15.16
5 Hufukuzwa watoke kati ya watu; Huwapigia kelele kama kumpigia mwivi.
Daniel 4.25 Psaumes 109.10 Genèse 4.12-4.14 Daniel 4.32-4.33
6 Lazima hukaa katika mianya ya mabonde, Katika mashimo ya nchi na ya majabali.
Juges 6.2 1 Samuel 22.1-22.2 Esaïe 2.19 Apocalypse 6.15
7 Hulia kama punda vichakani; Hukusanyika chini ya upupu.
Job 6.5 Genèse 16.12 Job 11.12
8 Wao ni wana wa wapumbavu, naam, watoto wa wahuni; Walifukuzwa kwa mijeledi watoke katika nchi.
Psaumes 49.10-49.13 2 Chroniques 22.3 Marc 6.24 2 Rois 8.27 Proverbes 1.7
9 Na sasa mimi nimekuwa wimbo wao, Naam, nimekuwa simo kwao.
Lamentations 3.63 Job 17.6 Lamentations 3.14 Psaumes 69.11-69.12 Psaumes 35.15-35.16
10 Wao hunichukia, na kujitenga nami, Hawaachi kunitemea mate usoni.
Matthieu 26.67 Esaïe 50.6 Nombres 12.14 Psaumes 88.8 Deutéronome 25.9
11 Kwani ameilegeza kamba yake, na kunitesa, Wala hawajizuii tena mbele yangu.
Psaumes 32.9 Job 12.18 Matthieu 27.39-27.44 Matthieu 26.67-26.68 Psaumes 35.21
12 Kwa mkono wangu wa kuume huinuka kundi; Huisukuma miguu yangu kando, Na kunipandishia njia zao za uharibifu.
Job 19.12 Esaïe 3.5 Psaumes 140.4-140.5 Job 19.18
13 Waiharibu njia yangu, Wauzidisha msiba wangu, Watu wasio na msaidizi.
Esaïe 3.12 Psaumes 69.26 Zacharie 1.15
14 Wanijilia kama wapitao katika ufa mpana; Katikati ya magofu wanishambulia.
Job 22.16 Psaumes 18.4 Esaïe 8.7-8.8 Psaumes 69.14-69.15
15 Vitisho vimenigeukia; Huifukuza heshima yangu kama upepo; Na kufanikiwa kwangu kumepita kama wingu.
Osée 13.3 Esaïe 44.22 Job 6.4 Job 9.27-9.28 Job 7.14
16 Sasa nafsi yangu inamwagika ndani yangu; Siku za mateso zimenishika.
Psaumes 22.14 Psaumes 42.4 Esaïe 53.12 Psaumes 40.12 Job 3.24
17 Wakati wa usiku mifupa yangu huchomeka ndani yangu, Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki.
Job 33.19-33.21 Esaïe 38.13 Job 7.4 Psaumes 38.2-38.8 Psaumes 6.2-6.6
18 Kwa ugonjwa wangu kuwa na nguvu nyingi Mavazi yangu yameharibika; Hunikaza kama shingo ya kanzu yangu.
Job 2.7 Job 7.5 Psaumes 38.5 Job 19.20 Esaïe 1.5-1.6
19 Yeye amenibwaga topeni, Nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Genèse 18.27 Job 9.31 Job 42.6 Job 2.8 Psaumes 69.14
20 Nakulilia wewe, wala huniitikii; Nasimama, nawe wanitazama tu.
Job 19.7 Matthieu 15.23 Lamentations 3.44 Psaumes 80.4-80.5 Job 27.9
21 Wewe umegeuka kuwa mkali kwangu; Nawe waniudhi kwa uweza wa mkono wako.
Job 10.14-10.17 Job 16.9-16.14 Job 19.6-19.9 Job 23.6 Job 13.25-13.28
22 Waniinua juu hata upeponi, na kunipandisha juu yake; Nawe waniyeyusha katika dhoruba.
Job 27.21 Job 21.18 Osée 4.19 Job 9.17 Psaumes 18.10
23 Kwani najua kuwa utanileta hata kifoni, Niifikilie nyumba waliyoandikiwa wenye uhai wote.
Ecclésiaste 12.5-12.7 Genèse 3.19 Ecclésiaste 9.5 Job 10.8 Job 21.33
24 Je! Mtu katika kuanguka kwake hanyoshi mkono? Na kulilia msaada katika msiba wake?
Matthieu 27.39-27.44 Juges 5.31 Psaumes 35.25 Job 19.7
25 Je! Mimi sikulia kwa ajili ya huyo aliyekuwa katika taabu? Nafsi yangu, je! Haikusononeka kwa ajili ya wahitaji?
Psaumes 35.13-35.14 Romains 12.15 Jérémie 13.17 2 Corinthiens 9.9 Job 31.16-31.21
26 Hapo nilipotazamia mema, ndipo yakaja mabaya; Nami nilipongojea mwanga, likaja giza.
Jérémie 8.15 Jérémie 14.19 Job 3.25-3.26 Job 18.6 Job 29.18
27 Matumbo yangu yatokota, wala hayaachi; Siku za taabu zimenijilia.
Lamentations 2.11 Lamentations 1.20 Jérémie 31.20 Psaumes 22.4 Jérémie 4.19
28 Naenda nikiomboleza pasipo jua; Nasimama katika mkutano, na kuulilia msaada.
Psaumes 42.9 Psaumes 43.2 Psaumes 38.6 Lamentations 3.1-3.3 Esaïe 53.3-53.4
29 Mimi ni ndugu yao mbwa-mwitu, Ni mwenzao mbuni.
Michée 1.8 Psaumes 102.6 Malachie 1.3 Esaïe 13.21-13.22 Psaumes 44.19
30 Ngozi yangu ni nyeusi, nayo yanitoka, Na mifupa yangu imeteketea kwa hari.
Psaumes 102.3 Lamentations 4.8 Psaumes 119.83 Lamentations 5.10 Lamentations 3.4
31 Kwa hiyo kinanda changu kimegeuzwa kuwa maombolezo, Na filimbi yangu kuwa sauti yao waliao.
Lamentations 5.15 Esaïe 24.7-24.9 Esaïe 22.12 Psaumes 137.1-137.4 Ecclésiaste 3.4

Cette Bible est dans le domaine public.