Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 29.9
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema,
Job 27.1 Nombres 23.7 Job 13.12
2 Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa katika miezi ya kale, Kama katika siku hizo Mungu aliponilinda;
Jérémie 31.28 Psaumes 37.28 Job 1.1-1.5 Job 1.10 Job 7.3
3 Hapo taa yake ilipomulika juu yangu kichwani, Nami nilitembea gizani kwa njia ya mwanga wake;
Psaumes 18.28 Job 18.6 Ephésiens 5.8 Jean 8.12 Jean 12.46
4 Kama nilivyokuwa katika siku zangu za kukomaa, Hapo siri ya Mungu ilipokuwa hemani mwangu;
Psaumes 25.14 Proverbes 3.32 Job 15.8 Job 1.10 Psaumes 91.1
5 Wakati Mwenyezi alipokuwa akali pamoja nami, Nao watoto wangu walipokuwa wakinizunguka;
Psaumes 128.3 Psaumes 127.3-127.5 Deutéronome 33.27-33.29 Cantique 2.4 Psaumes 30.7
6 Wakati hatua zangu zilipokuwa zikioshwa kwa siagi, Nalo jabali liliponimiminia mito ya mafuta!
Psaumes 81.16 Job 20.17 Deutéronome 32.13-32.14 Genèse 49.11 Deutéronome 33.24
7 Wakati nilipotoka kwenda mjini, hata langoni, Nilipokitengeza kiti changu katika njia kuu,
Deutéronome 16.18 Zacharie 8.16 Ruth 4.1-4.2 Job 31.21 Ruth 4.11
8 Hao vijana waliniona wakajificha, Nao wazee wakaniondokea na kusimama;
Lévitique 19.32 Romains 13.7 1 Pierre 5.5 Proverbes 16.31 Tite 3.1
9 Wakuu wakanyamaa wasinene, Na kuweka mikono yao vinywani mwao;
Job 21.5 Job 40.4 Proverbes 10.19 Jacques 1.19 Proverbes 30.32
10 Sauti yao masheki ilinyamaa, Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao.
Psaumes 137.6 Ezéchiel 3.26
11 Maana sikio liliponisikia, ndipo likanibarikia; Na jicho liliponiona, likanishuhudia.
Luc 4.22 Proverbes 29.2 Luc 11.27 Job 31.20
12 Kwa sababu nalimwokoa maskini aliyenililia; Yatima naye, na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia.
Psaumes 72.12 Proverbes 21.13 Deutéronome 10.18 Exode 22.22-22.24 Psaumes 68.5
13 Baraka yake yeye aliyekuwa karibu na kupotea ilinijia; Nikaufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
Job 31.19-31.20 Job 22.9 Esaïe 27.13 Philémon 1.7 2 Timothée 1.16-1.18
14 Nalijivika haki, ikanifunika, Adili yangu ilikuwa kama joho na kilemba.
Psaumes 132.9 Esaïe 61.10 Esaïe 59.17 Ephésiens 6.14 Job 27.6
15 Nalikuwa macho kwa kipofu, Nalikuwa miguu kwa aliyechechemea.
Nombres 10.31 Matthieu 11.5 1 Corinthiens 12.12-12.31
16 Nalikuwa baba kwa mhitaji, Na daawa ya mtu nisiyemjua naliichunguza.
Proverbes 29.7 Psaumes 68.5 Proverbes 25.2 Esther 2.7 Job 31.18
17 Nami nilizivunja taya za wasio haki, Na kumpokonya mawindo katika meno yake.
Psaumes 3.7 Proverbes 30.14 1 Samuel 17.35 Psaumes 124.6 Psaumes 58.8
18 Ndipo niliposema, Nitakufa ndani ya kioto changu, Nami nitaziongeza siku zangu kama mchanga;
Job 5.26 Job 42.16-42.17 Psaumes 30.6-30.7 Genèse 32.12 Psaumes 91.16
19 Shina langu limeenea hata kufika majini, Na umande hukaa usiku kucha katika matawi yangu;
Jérémie 17.8 Psaumes 1.3 Job 18.16 Osée 14.5-14.7
20 Utukufu wangu utakuwa mpya kwangu, Na uta wangu hurejezwa upya mkononi mwangu.
Genèse 49.24 Esaïe 40.31 Psaumes 103.5 Psaumes 3.3 Genèse 45.13
21 Watu walitega masikio kunisikiliza, na kungoja, Wakanyamaa kimya wapate sikia mashauri yangu.
Job 29.9-29.10 Job 32.11-32.12
22 Hawakunena tena baada ya kusikia maneno yangu; Matamko yangu yakadondoka juu yao.
Deutéronome 32.2 Esaïe 52.15 Matthieu 22.46 Ezéchiel 20.46 Cantique 4.11
23 Walikuwa wakiningojea kama kungojea mvua; Wakafunua vinywa vyao sana kama mvua ya masika.
Zacharie 10.1 Osée 6.3 Psaumes 72.6
24 Walipokata tamaa nikacheka nao; Na mwanga wa uso wangu hawakuuangusha.
Psaumes 4.6 Psaumes 126.1 Psaumes 89.15 Luc 24.41 Genèse 45.26
25 Niliwachagulia njia, nikakaa kama mkuu wao. Nikakaa kama mfalme katika jeshi la askari, Mfano wa awafarijiye hao waombolezao.
Juges 11.8 2 Corinthiens 1.3-1.4 Genèse 41.40 Genèse 14.14-14.17 Esaïe 35.3-35.4

Cette Bible est dans le domaine public.