Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 26.10
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 9 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Jinsi ulivyomsaidia huyo asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono usio na nguvu!
Job 12.2 1 Rois 18.27 Job 4.3-4.4 Esaïe 35.3-35.4 Esaïe 41.5-41.7
3 Jinsi ulivyomshauri huyo asiye na hekima! Na kutangaza ujuzi wa kweli kwa wingi!
Actes 20.27 Job 33.33 Job 13.5 Job 15.8-15.10 Psaumes 71.15-71.18
4 Je! Umetamka maneno kwa nani? Kisha ni roho ya nani iliyotoka kwako?
1 Rois 22.23-22.24 Job 32.18 Ecclésiaste 12.7 Job 20.3 Apocalypse 16.13-16.14
5 Hao waliokufa watetema Chini ya maji na hao wayakaao.
Genèse 6.4 Psaumes 88.10 Job 41.1-41.34 Ezéchiel 29.3-29.5 Psaumes 104.25-104.26
6 Kaburi li wazi mbele yake, Uharibifu nao hauna kifuniko.
Proverbes 15.11 Psaumes 139.8 Job 28.22 Hébreux 4.13 Amos 9.2
7 Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu, Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu.
Job 9.8 Psaumes 104.2-104.5 Genèse 1.1-1.2 Esaïe 40.22 Proverbes 8.23-8.27
8 Huyafunga maji ndani ya mawingu yake mazito; Na hilo wingu halipasuki chini yake.
Proverbes 30.4 Jérémie 10.13 Esaïe 5.6 Job 38.37 Job 38.9
9 Husitiri uso wa kiti chake cha enzi, Na kulitandaza wingu lake juu yake.
Psaumes 97.2 Exode 20.21 Habakuk 3.3-3.5 Exode 33.20-33.23 1 Rois 8.12
10 Amepiga duara kuwa ni mpaka juu ya uso wa maji, Hata hapo mwanga na giza vinapopakana.
Proverbes 8.29 Job 38.8-38.11 Psaumes 33.7 Jérémie 5.22 Esaïe 54.9-54.10
11 Nguzo za mbingu zatetemeka, Na kustaajabu kwa kukemea kwake.
1 Samuel 2.8 Aggée 2.21 Job 15.15 Psaumes 18.7 2 Pierre 3.10
12 Huichafua bahari kwa uwezo wake, Na kumtema Rahabu kwa akili zake.
Esaïe 51.15 Jérémie 31.35 Esaïe 51.9 Job 9.13 Psaumes 89.9-89.10
13 Hizo mbingu hupambwa kwa roho yake; Mkono wake umemchoma nyoka aendaye mbio.
Esaïe 27.1 Psaumes 74.13-74.14 Psaumes 104.30 Genèse 1.2 Psaumes 33.6-33.7
14 Tazama, hivi ni viunga tu vya njia zake; Na jinsi yalivyo madogo manong’ono tusikiayo katika habari zake! Lakini ngurumo za uweza wake ni nani awezaye kuelewa nazo?
Job 11.7-11.9 1 Corinthiens 13.9-13.12 Psaumes 139.6 Job 40.9 Esaïe 40.26-40.29

Cette Bible est dans le domaine public.