Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 9.6
Bible en Swahili de l’est


Visite de la reine de Séba

1 Na malkia wa Sheba aliposikia habari za Sulemani, alikuja ili amjaribu Sulemani kwa maswali ya fumbo huko Yerusalemu, mwenye wafuasi wengi, na ngamia wachukuao manukato, na dhahabu nyingi sana, na vito vya thamani; alipomfikilia Sulemani, akamwambia mambo yote aliyokuwa nayo moyoni mwake.
Matthieu 12.42 Luc 11.31 1 Rois 10.1-10.13 2 Chroniques 9.9 Genèse 10.7
2 Naye Sulemani akamfumbulia maswali yake yote; wala halikuwako neno alilofichiwa Sulemani, asimwambie.
Proverbes 18.4 Proverbes 13.20 1 Rois 3.12 Jacques 1.5 Colossiens 2.3
3 Naye malkia wa Sheba alipoona hekima ya Sulemani, na nyumba aliyoijenga,
2 Chroniques 3.1-3.4 1 Rois 6.1-6.7 1 Rois 10.3 Actes 11.23
4 na vyakula vya mezani mwake, na kikao cha watumishi wake, na usimamizi wao wangoje wake, na mavazi yao; na wanyweshaji wake, na mavazi yao; na daraja yake ya kupandia mpaka nyumba ya Bwana; roho yake ilizimia.
Cantique 5.8 1 Rois 10.5 2 Rois 16.18 Proverbes 9.5 Luc 12.37
5 Akamwambia mfalme, Ndizo kweli habari zile nilizozisikia katika nchi yangu za mambo yako na za hekima yako.
1 Rois 10.6
6 Lakini mimi sikuyasadiki maneno yao, hata nilipokuja na kuona kwa macho yangu; wala, tazama, ukuu wa hekima yako sikuambiwa nusu; wewe umezidi kuliko habari nilizozisikia.
Jean 20.25-20.29 Cantique 5.9-5.16 Psaumes 31.19 1 Corinthiens 2.9 Zacharie 9.17
7 Heri watu wako, na heri hawa watumishi wako, wasimamao mbele yako sikuzote, wakisikia hekima yako.
Proverbes 3.3 Proverbes 13.20 Proverbes 10.21 Proverbes 8.34 Luc 11.28
8 Na ahimidiwe Bwana, Mungu wako, aliyependezwa nawe, ili akuweke juu ya kiti chake cha enzi, kuwa mfalme wake Bwana, Mungu wako; kwa kuwa Mungu wako amewapenda Israeli, kuwathibitisha milele, kwa hiyo amekufanya kuwa mfalme juu yao, ufanye hukumu na haki.
2 Chroniques 2.11 1 Chroniques 29.23 Deutéronome 7.8 Psaumes 22.8 2 Samuel 15.25-15.26
9 Basi akampa mfalme talanta mia na ishirini za dhahabu, na manukato mengi mengi sana, na vito vya thamani; wala haukuja wingi wa manukato, kama hayo aliyopewa mfalme Sulemani na malkia wa Sheba.
1 Rois 9.14 Psaumes 72.15 2 Chroniques 9.24 1 Rois 10.10 Psaumes 72.10
10 Tena watumishi wa Hiramu, pamoja na watumishi wa Sulemani, walioleta dhahabu kutoka Ofiri, wakaleta miti ya msandali, na vito vya thamani.
2 Chroniques 8.18 1 Rois 10.11 1 Rois 9.27-9.28 1 Rois 10.22
11 Mfalme akayafanya kwa miti hiyo ya msandali madari ya nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme, na vinubi na vinanda vya hao waimbaji; wala haijatokea kama hiyo katika nchi ya Yuda.
1 Rois 10.12 Apocalypse 5.8 1 Chroniques 25.1 1 Chroniques 23.5 Psaumes 92.1-92.3
12 Mfalme Sulemani akampa malkia wa Sheba haja yake yote, kila alilotaka, zaidi ya vile alivyomletea mfalme. Basi akarudi, akaenda zake katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
1 Rois 10.13 Ephésiens 3.20 Psaumes 20.4

Richesses de Salomon

13 Basi uzani wa dhahabu iliyomfikia Sulemani mwaka mmoja, ndio talanta mia sita sitini na sita za dhahabu;
Psaumes 72.15 Psaumes 72.10 1 Rois 10.14-10.28 Psaumes 68.29
14 mbali na ile waliyoileta wachuuzi na wafanya biashara; tena wafalme wote wa Arabuni, na maliwali wa nchi wakamletea Sulemani dhahabu na fedha.
Psaumes 68.29 Psaumes 72.10
15 Mfalme Sulemani akafanya ngao mia mbili za dhahabu iliyofuliwa; ngao moja hupata shekeli mia sita za dhahabu iliyofuliwa.
1 Rois 10.16-10.17 2 Chroniques 12.9-12.10
16 Na vigao mia tatu vya dhahabu iliyofuliwa; kigao kimoja hupata shekeli mia tatu za dhahabu; mfalme akaviweka katika nyumba ya mwitu wa Lebanoni.
1 Rois 7.2
17 Tena mfalme akafanya kiti cha enzi kikubwa cha pembe, akakifunikiza kwa dhahabu iliyo safi.
Psaumes 45.8 Apocalypse 20.11 1 Rois 10.18-10.20
18 Kiti kile kilikuwa na daraja sita, tena na kikao cha miguu cha dhahabu, navyo vilikuwa vimeshikamana na kiti; na mikono huko na huko mahali pa kuketi, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
Apocalypse 5.5 Nombres 24.9 Nombres 23.24 Genèse 49.9-49.10
19 Na simba kumi na wawili wamesimama juu ya daraja sita, huko na huko; wala hakikufanyika kwa mfano wake katika ufalme wo wote.
Apocalypse 21.12 Matthieu 19.28
20 Na vyombo vyote vya kunywea vya mfalme Sulemani vilikuwa vya dhahabu, na vyombo vyote vya nyumba ya mwitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu iliyosafika; fedha haikuhesabiwa kuwa kitu siku za Sulemani.
1 Rois 10.21 Jérémie 31.5 Daniel 5.2-5.3 Esther 1.7 2 Chroniques 9.27
21 Kwa kuwa mfalme alikuwa na merikebu zilizokwenda Tarshishi pamoja na watumishi wa Hiramu; mara moja katika miaka mitatu huja merikebu za Tarshishi, zikileta dhahabu, na fedha, na pembe, na nyani, na tausi.
1 Rois 22.48 2 Chroniques 20.36-20.37 1 Rois 10.22 Job 39.13
22 Basi mfalme Sulemani akawapita wafalme wote wa duniani kwa mali, na kwa hekima.
2 Chroniques 1.12 1 Rois 3.12-3.13 Colossiens 2.2-2.3 Matthieu 12.42 1 Rois 10.23-10.24
23 Wafalme wote wa duniani wakamtafuta Sulemani uso wake, ili waisikie hekima yake, Mungu aliyomtia moyoni.
1 Rois 4.34 Ephésiens 1.17 Daniel 5.11 Jacques 1.16-1.17 Luc 21.15
24 Wakaleta kila mtu zawadi yake, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na mavazi, na silaha, na manukato, na farasi, na nyumbu, hesabu yake ya mwaka kwa mwaka.
2 Chroniques 9.9 1 Samuel 10.27 1 Rois 9.14 1 Rois 10.25 1 Rois 10.10
25 Sulemani akawa na mazizi ya farasi na magari elfu nne, na wapandao farasi kumi na mbili elfu, aliowaweka katika miji ya magari, na pamoja na mfalme huko Yerusalemu.
1 Rois 4.26 2 Chroniques 1.14 1 Rois 10.26 Deutéronome 17.16
26 Akatawala juu ya wafalme wote toka Mto hata nchi ya Wafilisti, na hata mpaka wa Misri.
1 Rois 4.21 Genèse 15.18 Exode 23.31 1 Rois 4.24 Daniel 7.14
27 Mfalme akafanya fedha humo Yerusalemu kuwa kama mawe, na mierezi akaifanya kuwa kama mikuyu iliyomo Shefela, kwa kuwa mingi.
2 Chroniques 1.15-1.17 1 Rois 10.27-10.29 2 Chroniques 9.20 Luc 19.4 1 Chroniques 27.28
28 Wakamletea Sulemani farasi kutoka Misri, na kutoka nchi zote.
2 Chroniques 1.16 2 Chroniques 9.25 Esaïe 2.7-2.8 Esaïe 31.1 1 Rois 10.28

Mort de Salomon

29 Basi mambo yake Sulemani yaliyosalia, ya kwanza, na ya mwisho, je! Hayakuandikwa katika tarehe ya Nathani nabii, katika unabii wa Ahiya, Mshiloni, na katika maono ya Ido mwonaji juu ya Yeroboamu mwana wa Nebati?
1 Chroniques 29.29 1 Rois 11.29 1 Rois 11.41-11.43 2 Samuel 12.1 2 Chroniques 13.22
30 Akatawala Sulemani katika Yerusalemu juu ya Israeli wote miaka arobaini.
1 Rois 11.42-11.43
31 Naye Sulemani akalala na baba zake, akazikwa mjini mwa Daudi babaye; akatawala Rehoboamu mwanawe badala yake.
1 Rois 2.10 2 Samuel 7.12 1 Rois 1.21

Cette Bible est dans le domaine public.