Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 24.15
Bible en Swahili de l’est


Règne de Joas

1 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala; akatawala miaka arobaini huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Sibia wa Beer-sheba.
2 Rois 11.21-12.15 1 Chroniques 3.11
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana siku zote za Yehoyada kuhani.
2 Chroniques 26.4-26.5 2 Chroniques 25.2 2 Rois 12.2 Marc 4.16-4.17 Psaumes 78.36-78.37
3 Yehoyada akamwoza wake wawili, naye akazaa wana na binti.
Genèse 21.21 Genèse 24.4 Matthieu 19.4-19.8 Genèse 4.19 2 Chroniques 24.15
4 Ikawa baada ya haya, Yoashi alikuwa na nia ya kuitengeneza nyumba ya Mungu.
5 Akawakusanya makuhani na Walawi, akawaambia, Nendeni mijini mwa Yuda, mkakusanye katika Israeli wote fedha, ili kuitengeneza nyumba ya Mungu wenu mwaka kwa mwaka, mkafanye bidii kuliharakisha neno hili. Walakini Walawi hawakuliharakisha.
2 Chroniques 29.3 2 Rois 12.4-12.7 2 Chroniques 34.8-34.9 2 Chroniques 21.2
6 Mfalme akamwita Yehoyada mkuu wao, akamwambia, Mbona hukuwataka Walawi waitoze Yuda na Yerusalemu kodi ya Musa mtumishi wa Bwana, na ya kusanyiko la Israeli, kwa ajili ya hema ya ushuhuda?
Exode 30.12-30.16 Nombres 1.50 Nombres 17.7-17.8 Actes 7.44 Nombres 18.2
7 Kwa kuwa wana wa Athalia, yule mwanamke mwovu, walikuwa wameibomoa nyumba ya Mungu; na vitakatifu vyote vya nyumba ya Bwana wamewapatia mabaali.
2 Chroniques 21.17 Apocalypse 2.20 Osée 2.8-2.9 2 Rois 12.4 Osée 2.13
8 Basi mfalme akaamuru, nao wakafanyiza kasha, wakaliweka nje langoni pa nyumba ya Bwana.
2 Rois 12.8-12.9 Marc 12.41
9 Wakapiga mbiu katika Yuda na Yerusalemu, kumletea Bwana kodi aliyoiweka Musa mtumishi wa Mungu, juu ya Israeli jangwani.
2 Chroniques 24.6 Matthieu 17.24-17.27
10 Wakafurahi maakida wote na watu wote, wakaleta na kutia ndani ya kasha, hata wakaisha.
1 Chroniques 29.9 2 Corinthiens 8.2 2 Corinthiens 9.7 Esaïe 64.5 Actes 2.45-2.47
11 Ikawa wakati walipoletewa kasha wasimamizi wa mfalme kwa mkono wa Walawi, nao wakaona ya kwamba kuna fedha nyingi, huja karani wa mfalme, na msimamizi wake kuhani mkuu, wakatoa yaliyomo kashani, kisha hulichukua kasha, na kulirudisha mahali pake. Ndivyo walivyofanya siku kwa siku, wakakusanya fedha tele.
2 Rois 12.10-12.12 1 Corinthiens 16.2
12 Na mfalme na Yehoyada waliwapa hao waliofanya kazi ya utumishi wa nyumba ya Bwana; nao wakawaajiri waashi na maseremala ili kuitengeza nyumba ya Bwana, na hao pia wafuao chuma na shaba ili kuitengeza nyumba ya Bwana.
2 Chroniques 34.9-34.11 1 Rois 5.15
13 Hivyo mafundi wakafanya kazi yao, nao wakaimaliza, wakaisimamisha nyumba ya Mungu kama ilivyopasa, wakaifanya imara.
Aggée 2.3 1 Chroniques 22.5 Néhémie 4.7 Marc 13.1-13.2
14 Nao walipokwisha, wakaleta mbele ya mfalme na Yehoyada fedha iliyobaki, vikafanyizwa kwayo vyombo vya nyumba ya Bwana, vyombo vya utumishi, navyo vya kutolea, na miiko, na vyombo vya dhahabu na fedha. Wakatoa sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya Bwana, daima, siku zote za Yehoyada.
Nombres 28.2-28.29 2 Rois 12.13-12.14 Exode 29.38-29.42 Proverbes 27.22 1 Rois 7.50
15 Lakini Yehoyada akawa mzee, mwenye umri mwingi, akafa; alipokufa alikuwa na umri wa miaka mia na thelathini.
Genèse 15.15 1 Chroniques 23.1 Genèse 47.9 Genèse 25.8 Psaumes 91.16
16 Wakamzika katika mji wa Daudi kati ya wafalme, kwa sababu ametenda mema katika Israeli, na kwa Mungu, na katika nyumba yake.
Hébreux 6.10 1 Samuel 2.30 2 Chroniques 23.1-23.21 1 Rois 2.10 Actes 2.29
17 Hata baada ya kufa kwake Yehoyada, wakuu wa Yuda wakamwendea mfalme, wakamsujudia. Naye mfalme akawasikiliza maneno yao.
Deutéronome 31.27 Proverbes 26.28 Proverbes 7.21-7.23 Actes 20.29-20.30 Proverbes 20.19
18 Wakaiacha nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zao; wakatumikia maashera na sanamu; ghadhabu ikawajia Yuda na Yerusalemu kwa sababu ya hiyo hatia yao.
2 Chroniques 24.4 2 Chroniques 19.2 Josué 22.20 2 Chroniques 29.8 2 Chroniques 28.13
19 Hata hivyo akawapelekea manabii, ili kuwarudisha kwa Bwana; nao wakawashuhudia; lakini hawakukubali kuwasikiliza.
Esaïe 55.3 Psaumes 95.7-95.8 Luc 20.9-20.15 Esaïe 51.4 Esaïe 28.23
20 Na roho ya Mungu ikamjia Zekaria, mwana wa Yehoyada, kuhani; naye akasimama juu ya watu, akawaambia, Mungu asema hivi, Kwani ninyi kuzihalifu amri za Bwana, hata msiweze kufanikiwa? Kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.
Nombres 14.41 2 Chroniques 20.14 1 Chroniques 12.18 2 Chroniques 15.1-15.2 Matthieu 23.35
21 Basi, wakafanya shauri juu yake, wakampiga kwa mawe kwa amri ya mfalme katika ua wa nyumba ya Bwana.
Actes 7.58-7.59 Néhémie 9.26 Matthieu 23.34-23.37 Jérémie 18.18 Jérémie 38.4-38.6
22 Basi hivyo mfalme Yoashi hakuukumbuka wema, ambao Yehoyada, baba yake, alimfanyia, bali alimwua mwanawe. Naye alipokufa, alisema, Bwana na ayaangalie haya, akayatakie kisasi.
Genèse 9.5 Psaumes 10.14 Luc 11.51 Apocalypse 18.20 Apocalypse 19.2
23 Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote.
2 Rois 12.17-12.18 2 Chroniques 24.17-24.18 Deutéronome 32.35 Psaumes 2.10-2.11 Psaumes 58.10-58.11
24 Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu.
Esaïe 30.17 Lévitique 26.25 Lévitique 26.37 2 Chroniques 22.8 Deutéronome 28.25
25 Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.
2 Chroniques 28.27 2 Chroniques 24.21-24.22 2 Rois 12.20-12.21 Apocalypse 16.6 2 Chroniques 21.18-21.20
26 Na hawa ndio waliomfanyia fitina, Zabadi mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, na Yehozabadi mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabi.
2 Rois 12.21
27 Basi kwa habari ya wanawe, na ukubwa wa mizigo aliolemewa, na majengo ya nyumba ya Mungu, tazama, hayo yameandikwa katika maelezo ya kitabu cha wafalme. Na Amazia mwanawe akatawala mahali pake.
2 Chroniques 13.22 2 Rois 12.21 2 Chroniques 16.11 2 Chroniques 9.29 2 Chroniques 25.1

Cette Bible est dans le domaine public.