Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 19
Bible en Swahili de l’est


1 Yehoshafati mfalme wa Yuda akarudi Yerusalemu nyumbani kwake kwa amani.
2 Chroniques 18.31-18.32
2 Yehu mwana wa Hanani mwonaji akatoka kwenda kumlaki, akamwambia mfalme Yehoshafati, Je! Imekupasa kuwasaidia waovu, na kuwapenda wamchukiao Bwana? Kwa ajili ya hayo ghadhabu i juu yako itokayo kwa Bwana.
2 Chroniques 16.7 2 Chroniques 20.34 1 Rois 16.1 2 Chroniques 32.25 2 Chroniques 18.3
3 Walakini yameonekana mema ndani yako, kwa kuwa umeyaondoa maashera katika nchi, na moyo wako umeukaza kumtafuta Mungu.
2 Chroniques 12.12 Esdras 7.10 1 Rois 14.13 2 Chroniques 30.19 2 Chroniques 12.14

Réforme de la justice

4 Na Yehoshafati akakaa Yerusalemu; akatoka tena kwenda kati ya watu toka Beer-sheba mpaka milima ya Efraimu, akawarudisha kwa Bwana, Mungu wa baba zao.
2 Chroniques 15.8-15.13 Josué 17.15 Juges 19.1 Luc 1.17 Juges 20.1
5 Akasimamisha makadhi katika nchi, katikati ya miji yote yenye maboma ya Yuda, mji kwa mji;
Deutéronome 16.18-16.20 1 Pierre 2.13-2.14 Romains 13.1-13.5 2 Chroniques 19.8
6 akawaambia hao makadhi, Angalieni myafanyayo; kwa kuwa hammfanyii mwanadamu hukumu, ila Bwana; naye yupo pamoja nanyi katika neno la hukumu.
Deutéronome 1.17 1 Chroniques 28.10 Luc 21.8 Psaumes 82.1-82.6 Luc 12.15
7 Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu; angalieni mkaifanye; kwa maana kwa Bwana, Mungu wetu, hapana uovu, wala kujali nafsi za watu, wala kupokea zawadi.
Genèse 18.25 Deutéronome 32.4 Romains 2.11 Job 34.19 Deutéronome 16.18-16.19
8 Tena katika Yerusalemu Yehoshafati akasimamisha wa Walawi na makuhani, na wakuu wa mbari za mababa wa Israeli wawe kwa hukumu ya Bwana, na kwa mateto. Nao wakarudi Yerusalemu.
2 Chroniques 17.8-17.9 Deutéronome 25.1 Deutéronome 17.8-17.13 Exode 18.19-18.26 Deutéronome 21.5
9 Akawaagiza, akasema, Ndivyo mtakavyotenda kwa hofu ya Bwana, kwa uaminifu, na kwa moyo kamili.
2 Samuel 23.3 Esaïe 11.3-11.5 2 Chroniques 19.7 Deutéronome 1.16-1.17 Esaïe 32.1
10 Na kila mara watakapowajia na teto ndugu zenu wakaao mijini mwao, kati ya damu na damu, kati ya torati na amri, sheria na hukumu, mtawaonya, wasiingie hatiani mbele za Bwana, mkajiliwa na ghadhabu ninyi na ndugu zenu; fanyeni haya wala hamtakuwa na hatia.
Deutéronome 17.8-17.13 1 Thessaloniciens 5.14 Ezéchiel 33.6 Josué 22.18-22.20 Ezéchiel 3.18-3.21
11 Tena angalieni, Amaria, kuhani mkuu, yu juu yenu kwa maneno yote ya Bwana; naye Zebadia, mwana wa Ishmaeli, jemadari wa nyumba ya Yuda, kwa maneno yote ya mfalme; Walawi nao watakuwa wasimamizi mbele yenu. Jitieni nguvu, mtende, naye Bwana awe pamoja nao walio wema
2 Chroniques 19.8 1 Chroniques 26.30 Josué 1.6 1 Chroniques 22.11 Psaumes 37.23

Cette Bible est dans le domaine public.