Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 17.12
Bible en Swahili de l’est


Règne de Josaphat

1 Na Yehoshafati mwanawe akatawala mahali pake, akajitia nguvu juu ya Israeli.
1 Rois 15.24 Ephésiens 6.10 Matthieu 1.8 2 Chroniques 32.5 2 Chroniques 12.1
2 Akaweka jeshi katika miji yote yenye maboma ya Yuda, akatia na askari walinzi katika nchi ya Yuda, na katika miji ya Efraimu, aliyoitwaa Asa babaye.
2 Chroniques 15.8 2 Chroniques 11.11-11.12 2 Chroniques 11.5
3 Naye Bwana alikuwa pamoja na Yehoshafati, kwa kuwa alikwenda katika njia za kwanza za Daudi babaye, asiyatafute mabaali;
Exode 4.12 Psaumes 46.7 Josué 1.9 Matthieu 1.23 2 Chroniques 15.8-15.13
4 lakini alimtafuta Mungu wa baba yake, akaenda katika amri zake, wala si katika matendo ya Israeli.
1 Rois 12.28 2 Rois 17.19 1 Thessaloniciens 4.1 Osée 4.15 Luc 1.6
5 Kwa hiyo Bwana akauthibitisha ufalme mkononi mwake; Yehoshafati akaletewa zawadi na Yuda wote; basi akawa na mali na heshima tele.
2 Chroniques 18.1 1 Samuel 10.27 1 Pierre 5.10 Matthieu 6.33 Job 42.12
6 Ukainuliwa moyo wake katika njia za Bwana; na zaidi ya hayo akapaondoa mahali pa juu, na maashera, katika Yuda.
2 Chroniques 15.17 2 Chroniques 20.33 1 Rois 22.43 2 Chroniques 19.3 Psaumes 18.21-18.22
7 Tena, katika mwaka wa tatu wa kutawala kwake, akawatuma wakuu wake, yaani, Ben-haili, na Obadia, na Zekaria, na Nethaneli, na Mikaya, ili kufundisha mijini mwa Yuda;
2 Chroniques 35.3 2 Chroniques 15.3 Néhémie 9.3 Deutéronome 33.10 Néhémie 8.7-8.8
8 na pamoja nao Walawi, yaani, Shemaya, na Nethania, na Zebadia, na Asaheli, na Shemiramothi, na Yehonathani, na Adonia, na Tobia, na Tob-adonia, Walawi; na pamoja nao Elishama na Yehoramu, makuhani.
2 Chroniques 19.8 Esdras 7.1-7.6 Malachie 2.7
9 Wakafundisha katika Yuda, wenye kitabu cha torati ya Bwana; wakazunguka katika miji yote ya Yuda, wakafundisha kati ya watu.
Deutéronome 6.4-6.9 Actes 13.15 Matthieu 11.1 Josué 1.7-1.8 Matthieu 15.2-15.9
10 Hofu ya Bwana ikaziangukia falme za nchi zote zilizozunguka Yuda, wasipigane vita na Yehoshafati.
2 Chroniques 14.14 Genèse 35.5 Exode 34.24 Exode 15.14-15.16 Josué 2.9-2.11
11 Na baadhi ya Wafilisti walimletea Yehoshafati zawadi, na fedha ya kodi; Waarabu nao wakamletea makundi, kondoo waume saba elfu na mia saba, na mabeberu saba elfu na mia saba.
2 Chroniques 26.8 2 Chroniques 9.14 2 Samuel 8.2 2 Rois 3.4 2 Chroniques 17.5
12 Ukuu wake Yehoshafati ukazidi sana; akajenga katika Yuda ngome na miji ya hazina.
2 Chroniques 32.5 2 Chroniques 26.6-26.9 2 Chroniques 14.6-14.7 1 Chroniques 29.25 2 Chroniques 27.4
13 Naye alikuwa na kazi nyingi katika miji ya Yuda; na watu wa vita, watu mashujaa humo Yerusalemu.
2 Chroniques 26.10-26.15 1 Chroniques 27.25-27.31
14 Na hivi ndivyo walivyohesabiwa kwa mbari za baba zao; wa Yuda, maakida wa maelfu; Adna jemadari, na pamoja naye watu mashujaa mia tatu elfu;
2 Chroniques 14.8 Genèse 15.5 Genèse 12.2 2 Chroniques 11.1 Genèse 13.16
15 na wa pili wake Yehohanani akida, na pamoja naye mia mbili na themanini elfu;
16 na baada yake Amasia mwana wa Zikri, aliyejitoa kwa Bwana kwa moyo, na pamoja naye mia mbili elfu, watu mashujaa;
Juges 5.9 Juges 5.2 1 Chroniques 29.9 2 Corinthiens 8.3-8.5 Psaumes 110.3
17 na wa Benyamini; Eliada mtu shujaa, na pamoja naye mia mbili elfu wenye nyuta na ngao;
2 Samuel 1.21-1.22 2 Chroniques 14.8
18 na wa pili wake Yehozabadi, na pamoja naye mia na themanini elfu waliojiweka tayari kwa vita.
19 Hao ndio waliomngojea mfalme, zaidi ya hao mfalme aliowaweka katika miji yenye maboma katika Yuda yote.
2 Chroniques 17.2 2 Chroniques 17.12 2 Chroniques 11.12 2 Chroniques 11.23

Cette Bible est dans le domaine public.