Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 21.7
Bible en Swahili de l’est


Dénombrement et peste

1 Tena shetani akasimama juu ya Israeli, akamshawishi Daudi kuwahesabu Israeli.
Job 2.4-2.6 Zacharie 3.1 Job 2.1 Job 1.6-1.12 Luc 11.53
2 Basi Daudi akamwambia Yoabu, na wakuu wa watu, Nendeni kawahesabu Israeli toka Beer-sheba mpaka Dani; mkanipashe habari, nipate kujua jumla yao.
1 Chroniques 27.23-27.24 2 Samuel 24.2-24.4 2 Chroniques 30.5 1 Samuel 3.20 2 Corinthiens 12.7
3 Naye Yoabu akasema, Bwana na awaongeze watu wake mara mia hesabu yao ilivyo; lakini, bwana wangu mfalme, si wote watumishi wa bwana wangu? Mbona basi bwana wangu analitaka neno hili? Mbona awe sababu ya hatia kwa Israeli?
Esaïe 26.15 Deutéronome 1.11 1 Rois 14.16 1 Chroniques 19.13 Exode 32.21
4 Lakini neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akaenda zake, akapita kati ya Israeli wote, akafika Yerusalemu.
Actes 5.29 2 Samuel 24.3-24.8 Daniel 3.18 Exode 1.17 Ecclésiaste 8.4
5 Naye Yoabu akamtolea Daudi jumla ya hesabu ya watu. Na hao wote wa Israeli walikuwa watu elfu mara elfu, na mia elfu, wenye kufuta panga; na wa Yuda watu mia nne na sabini elfu, wenye kufuta panga.
2 Samuel 24.9 1 Chroniques 27.23
6 Lakini Lawi na Benyamini hakuwahesabu miongoni mwao; kwa sababu neno la mfalme limemchukiza Yoabu.
2 Samuel 11.15-11.21 2 Samuel 3.27 2 Samuel 20.9-20.10 Nombres 1.47-1.49 1 Chroniques 27.24
7 Neno hilo likawa baya machoni pa Mungu; kwa hiyo akawapiga Israeli.
Josué 7.13 1 Rois 15.5 Josué 7.5 2 Samuel 11.27 2 Samuel 24.1
8 Naye Daudi akamwambia Mungu, Nimekosa sana, kwa kuwa nimelifanya jambo hili; lakini sasa uuondolee mbali, nakusihi, uovu wa mtumwa wako; kwani nimefanya upumbavu kabisa.
2 Samuel 12.13 1 Jean 1.9 Psaumes 32.5 Genèse 34.7 2 Samuel 24.10
9 Naye Bwana akanena na Gadi, mwonaji wake Daudi, akisema,
1 Samuel 9.9 1 Chroniques 29.29 2 Samuel 24.11
10 Nenda ukanene na Daudi, ukisema, Bwana asema hivi, Nakuwekea mambo matatu; katika haya ujichagulie moja, nikutendee hilo.
Proverbes 3.12 Proverbes 1.29-1.31 2 Samuel 12.10-12.12 Josué 24.15 Nombres 20.12
11 Basi Gadi akamwendea Daudi, akamwambia, Bwana asema hivi, Kubali upendavyo;
Proverbes 19.20
12 miaka mitatu ya njaa; au miezi mitatu kuangamia mbele ya adui zako, ukipatwa na upanga wa watesi wako; au siku tatu upanga wa Bwana, yaani tauni katika nchi, na malaika wa Bwana akiharibu kati ya mipaka yote ya Israeli. Haya basi ufikiri ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma.
Lévitique 26.36-26.37 Jérémie 47.6 Lévitique 26.17 2 Samuel 21.1 2 Samuel 24.13-24.14
13 Naye Daudi akamwambia Gadi, Nimeingia katika mashaka sana; basi sasa na nianguke katika mkono wa Bwana; kwa kuwa rehema zake ni nyingi sana; wala nisianguke katika mkono wa wanadamu.
Psaumes 130.7 Psaumes 86.15 Esaïe 63.15 Jonas 4.2 Habakuk 3.2
14 Basi Bwana akawaletea Israeli tauni; nao wakaanguka wa Israeli watu sabini elfu.
Nombres 16.46-16.49 Exode 12.30 2 Rois 19.35 1 Chroniques 27.24 Nombres 25.9
15 Naye Mungu akatuma malaika aende Yerusalemu ili auangamize; naye alipokuwa tayari kuangamiza, Bwana akatazama, akaghairi katika mabaya, akamwambia malaika aharibuye, Basi yatosha; sasa ulegeze mkono wako. Naye malaika wa Bwana akasimama karibu na kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi.
Genèse 6.6 Exode 32.14 1 Rois 19.4 Matthieu 23.37-23.38 Psaumes 90.13
16 Daudi akainua macho yake, akamwona huyo malaika wa Bwana amesimama kati ya nchi na mbingu, naye alikuwa na upanga wazi mkononi, umenyoshwa juu ya Yerusakmu. Ndipo Daudi na wazee wakaanguka kifulifuli, nao wamevaa nguo za magunia.
1 Rois 21.27 Nombres 14.5 Genèse 3.24 Nombres 16.22 Exode 14.19-14.20
17 Daudi akamwambia Mungu, Je! Si mimi niliyeamuru watu wahesabiwe? Naam, mimi ndimi niliyekosa, na kufanya yaliyo maovu sana; lakini kondoo hawa, wamefanya nini? Mkono wako, nakusihi, Ee Bwana, Mungu wangu, na uwe juu yangu, na juu ya nyumba ya babangu; wala si juu ya watu wako, hata wao wapigwe.
Exode 20.5 1 Jean 3.16 Josué 22.18 Esaïe 39.7-39.8 1 Rois 22.17
18 Ndipo huyo malaika wa Bwana akamwamuru Gadi kwamba amwambie Daudi, ya kuwa Daudi akwee, akamwinulie Bwana madhabahu katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi.
2 Chroniques 3.1 2 Samuel 24.18 1 Chroniques 21.11 Actes 8.26-8.40 1 Chroniques 21.15
19 Basi Daudi akakwea sawasawa na neno la Gadi, alilolinena kwa jina la Bwana.
2 Rois 5.10-5.14 Jean 2.5 Actes 9.6
20 Arauna alipogeuka, na kumwona yule malaika, ndipo yeye na wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha. Naye Arauna alikuwa akipura ngano.
Juges 6.11
21 Basi Daudi alipokuwa akimjia Arauna, Arauna akatazama, akamwona Daudi, akatoka katika kile kiwanja, akamsujudia Daudi kifulifuli hata nchi.
2 Samuel 24.18-24.20 1 Samuel 25.23
22 Ndipo Daudi akamwambia Arauna, Unipe mahali pa kiwanja hiki, ili kwamba nimjengee Bwana madhabahu hapa; kwa thamani yake kamili utanipa; ili kwamba tauni izuiliwe katika watu.
Nombres 16.48 1 Rois 21.2 2 Samuel 24.21 Nombres 25.8
23 Arauna akamwambia Daudi, Ujitwalie, na bwana wangu mfalme na afanye yaliyo mema machoni pake; tazama, ng’ombe kwa sadaka za kuteketezwa, na vyombo vya kupuria kwa kuni, na ngano kwa sadaka ya unga, nazitoa; zote nazitoa.
2 Samuel 24.22-24.23 1 Rois 19.21 Esaïe 28.27-28.28 Jérémie 32.8 1 Samuel 6.14
24 Mfalme Daudi akamwambia Arauna, La, sivyo, lakini kweli nitazinunua kwa thamani yake kamili; kwani sitamtwalia Bwana kilicho chako, wala kutoa sadaka ya kuteketezwa isiyo na gharama.
Malachie 1.12-1.14 Romains 12.17 Genèse 14.23 Deutéronome 16.16-16.17 Genèse 23.13
25 Basi Daudi akampimia Arauna thamani ya mahali pale shekeli mia sita za dhahabu kwa uzani
2 Samuel 24.24-24.25
26 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu huko, akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akamlingana Bwana; naye akamwitikia kutoka mbinguni kwa moto juu ya madhabahu hiyo ya sadaka ya kuteketezwa.
Lévitique 9.24 Juges 6.21 Psaumes 99.9 1 Samuel 7.8-7.9 1 Rois 18.38
27 Bwana naye akamwamuru malaika; naye akaurudisha upanga wake alani mwake tena.
Psaumes 103.20 1 Chroniques 21.15-21.16 Ezéchiel 21.30 1 Chroniques 21.20 Jérémie 47.6
28 Wakati huo, Daudi alipoona ya kwamba Bwana amemwitikia katika kiwanja cha Arauna, Myebusi, ndipo hutoa dhabihu huko.
29 Kwa maana ile maskani ya Bwana, aliyoifanya Musa jangwani, na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, vilikuwapo wakati huo mahali pa juu pa Gibeoni.
1 Chroniques 16.39 2 Chroniques 1.3 1 Rois 3.4-3.15 2 Chroniques 1.13 Exode 40.1-40.38
30 Wala Daudi hakuweza kwenda mbele yake ili kumwuliza Mungu; kwa sababu aliona hofu kwa ajili ya upanga wa yule malaika wa Bwana.
Job 23.15 1 Chroniques 21.16 Jérémie 5.22 Job 21.6 1 Chroniques 13.12

Cette Bible est dans le domaine public.