Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 20.3
Bible en Swahili de l’est


Prise de Rabba

1 Hata ikawa, mwanzo wa mwaka mpya, wakati watokapo wafalme kwenda vitani, Yoabu akawaongoza mashujaa wa jeshi, akaiteka nyara nchi ya wana wa Amoni, akaja akauhusuru Raba. Lakini Daudi akakaa Yerusalemu. Naye Yoabu akaupiga Raba akauangamiza.
2 Samuel 11.1 Deutéronome 3.11 Amos 1.14 Ezéchiel 21.20 1 Rois 20.26
2 Kisha Daudi akamtwalia mfalme wao taji toka kichwani pake, akaona ya kwamba uzani wake ni talanta ya dhahabu, na kulikuwa na vito vya thamani ndani yake; akavikwa Daudi kichwani; akazitoa nyara za mji, nyingi sana.
2 Samuel 8.11-8.12 2 Samuel 12.30-12.31 1 Chroniques 18.11
3 Na hao watu waliokuwamo akawatoa, akawakata-kata kwa misumeno, na kwa sululu za chuma, na kwa mashoka. Ndivyo alivyofanya Daudi kwa miji yote ya wana wa Amoni. Nao wakarudi Yerusalemu Daudi na watu wote.
Josué 9.23 Juges 8.16-8.17 Exode 1.14 1 Chroniques 19.2-19.5 2 Samuel 12.31

Exploits contre les Philistins

4 Ikawa baada ya hayo, kulitokea vita na Wafilisti huko Gobu; ndipo Sibekai, Mhushathi, alipomwua Safu, mmojawapo wa Warefai; nao wakashindwa.
2 Samuel 21.18-21.22 Josué 12.12 Josué 16.3 2 Samuel 21.15 1 Chroniques 11.29
5 Kulikuwa na vita tena na Wafilisti; na Elhanani, mwana wa Yairi akamwua Lahmi nduguye Goliathi, Mgiti ,ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji.
2 Samuel 21.19 1 Samuel 21.9 1 Samuel 22.10 1 Samuel 17.4 1 Samuel 17.7
6 Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambapo palikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole vya mikono na miguu ishirini na vinne, kila mguu sita, na kila mkono sita; naye alizaliwa na Mrefai.
2 Samuel 21.20
7 Naye huyo alipowatukana Israeli, Yonathani, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua.
1 Samuel 16.9 1 Chroniques 2.13 1 Samuel 17.36 1 Samuel 17.26 1 Samuel 17.10
8 Hao walizaliwa kwake huyo Mrefai wa Gathi,nao wakaanguka kwa mkono wa Daudi , na kwa mkono wa watumishi wake.
Jérémie 9.23 Romains 8.31 Ecclésiaste 9.11 Josué 14.12

Cette Bible est dans le domaine public.